BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

“WATANZANIA WENZANGU WANIUNGE MKONO”-RICHA September, 18, 2007

Filed under: Fashion,Miss Tanzania,Tanzania/Zanzibar,Urembo — bongocelebrity @ 11:59 AM

Takribani wiki mbili tu zilizopita, Richa Adhia (pichani) alitwaa taji maarufu la Miss Tanzania kwa mwaka huu wa 2007. Maswali mengi na majibu mengi yaliibuka kufuatia ushindi wake. Bado ni gumzo linaloendelea huku kila mmoja akiwa na maoni yake. Kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake bila tu kuvunja sheria, kumkashifu au kumtukana mtu. Hiyo ndiyo misingi ya ustaarabu.

 

Jambo moja muhimu ambalo sote hatuna budi kukubaliana nalo ni kwamba Richa Adhia ndiye atakayetuwakilisha watanzania wote katika mashindano ya urembo ya dunia (Miss World) tarehe mosi(1) Desemba mwaka huu huko Sanya nchini China.

Hivi sasa anapojiandaa kuiwakilisha Tanzania huko nchini China, tulipata fursa ya kufanya naye mahojiano mafupi kuhusiana na maandalizi yake na ujumbe alionao kwa watanzania na wadau wote wa masuala ya ulimbwende. Yafuatayo ni mahojiano kamili;

BC: Richa kwanza hongera sana kwa ushindi wako wa Miss Tanzania 2007. Ulijisikiaje baada ya kutangazwa mshindi siku ile pale Leaders Club?

RICHA: Asante nashukuru. Nilipotangazwa kuwa mshindi nilishikwa na butwaa na kwa sekunde chache niliona kama ni ndoto.

BC: Watu wengi wametuandikia wakiomba tukuulize swali hili. Kwa maoni yako unadhani ni kwanini majaji wa Miss Tanzania 2007 walikupa wewe ushindi na si wenzako mliokuwa mkichuana? Nini kilikusaidia?

RICHA : Jibu la swali hili wanalo majaji. Kilichonisaidia mimi ni kujiamini na kufuata maelekezo yote tuliyopewa na waandaaji.

BC: Unapojiandaa kuelekea China kama mwakilishi wa taifa letu la Tanzania ni mambo gani matano (5 ) mazuri kuhusu nchi yako ambayo ikitokea ukaulizwa huko China hutofikiria kwa zaidi ya nusu dakika kuyataja?

RICHA: Mazuri ni mengi lakini nayataja 5 kama ulivyo uliza.

(1)Amani na Upendo: Nchi yetu ina makabila mengi na kila kabila lina utamaduni wake. Lakini tunaishi pamoja kwa amani na upendo pia tuna uhuru wa kuabudu.

(2)Tanzanite: Ni nchi pekee duniani yenye madini ya Tanzanite.

(3)Ngorongoro crater: Hii ni maajabu ya nane ya dunia na ipo Tanzania.

(4)Mlima Kilimanjaro: Ni mlima mrefu kuliko yote Afrika. Ni kivutio kikubwa kwa watalii.

(5)Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika: Ziwa Victoria ni ziwa kubwa kuliko yote Afrika, na Ziwa Tanganyika ni ziwa lenye kina kirefu kuliko yote Afrika.

BC: Tangu tulipoandika kuhusu ushindi wako katika blog yetu, kumekuwepo na ‘mvua” ya maoni juu ya ushindi wako. Wako wanaounga mkono ushindi wako na wapo pia wanaoupinga. Wanaoupinga wanatoa sababu kama vile; kwa sababu wewe ni mtanzania mwenye asili ya Asia basi kwa ujumla utamaduni wako ni wa kihindi zaidi ya kitanzania. Unawaambia nini watu wa kundi hilo linalokupinga?

RICHA: Nashukuru sana, mimi ni Mtanzania mwenye asili ya kiasia, lakini nimezaliwa Tanzania na wazazi wangu wamezaliwa Tanzania, mama yangu anatoka Pemba na baba yangu anatoka Morogoro. Nimekulia katika utamaduni wa kitanzania, ni utamaduni pekee ninao ufahamu, ninaouthamini, na ninao upenda kwa dhati.

Nawaomba watu wa kundi hilo wanaonipinga, waungane na mimi wanipe sapoti kwa sababu ninawakilisha Watanzania wenzangu wote.

BC: Hii itakuwa sio mara yako ya kwanza kuiwakilisha Tanzania katika medani za kimataifa za masuala ya urembo. Uliwahi kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss Earth yaliyofanyikia huko Philipines mwaka jana. Hukushinda. Una mategemeo gani katika mashindano ya Miss World mwaka huu? Unategemea kujiandaa vipi kuwania taji la Miss World tofauti na ulivyojiandaa ulipokwenda kushiriki Miss Earth mwaka jana?

RICHA: Ni kweli nilishiriki shindano la Miss Earth mwaka jana [2006] na sikushinda. Lakini katika shindano kuna kushinda na kushindwa. Na asiyekubali kushindwa si mshindani.

Isitoshe nimejifunza mengi kwenye shindano la Miss Earth na nataraji nitayatumia mafunzo hayo kwenye mashindano ya Miss world mwaka huu. Nimeshaanza kujiandaa na nitajitahidi kwa uwezo wangu wote kupeperusha bendera ya taifa vizuri.

 

BC: Umejifunza mambo gani ya msingi mpaka sasa hivi baada ya kuwa Mtanzania wa kwanza mwenye asili ya kihindi [Asia] kushinda taji la Miss Tanzania ?

RICHA: Kwa ujumla, nimejifunza kuwa Tanzania ni nchi yenye haki sawa kwa kila Mtanzania bila ya kujali rangi, kabila au dini yake.

BC: Una lolote ungependa kuongezea?

RICHA : Nashukuru sana kwa maswali yako na ninawaomba Watanzania wenzangu waniunge mkono na waniombee dua niweze kuiletea sifa nchi yetu nzuri ya Tanzania.

BC : Asante sana Richa kwa muda wako.Tunakutakia kila la kheri.

 

105 Responses to ““WATANZANIA WENZANGU WANIUNGE MKONO”-RICHA”

  1. Lizzie Says:

    mimi naomba jamani muhojini tusikie sauti yake kabisa weka sound pls ili nijue nimaccept vipi huyu binti

  2. sab Says:

    muongo mkubwa mnaijua tanzania kwa raha tu, mie sikupendi na wala usitudanganye wewe ni gabacholi tu, nitafurahi zaidi ukishindwa kwanza miss huwa anakuwa ameshapangwa na nenda kauze sura,

  3. Kingo Says:

    Lizzie,sab na Fatty, kweli nyie ni watu msiyoipenda nchi yenu na nyinyi ndiyo wale wabaguzi weusi mkiwabagua weusi wenzenu, ati tu kwa sababu umetia mkorogo uwe mweupe.Nyinyi ni weusi wabaguzi wa weusi wengine,ni watu msiyojua maana, na shukuruni tu kuwa nyerere hayupo tena, lakini angeliwafundisha nini maana ya ustaarabu na upendo.Mtanzania yoyote ni mtanzania tu mkitaka na hata msitake haangaliwi sura wala rangi yake.mbona mkiwa huko ulaya mlikokuwa mnazaa na kuwaita watoto wenu kuwa ni wamarekani au waingereza?Hivi hujui kuwa huko original wenyewe ni watu weupe?? Asiyejua maana haambiwi maana.Kalagabaho!!!!!!

  4. mamak Says:

    aende zake,akashindane huko india na siyo tanzania,tupo warembo wengi sana nchini kwetu tanzania.

  5. Ike Says:

    Hivi huyu binti kwanini asianze kuwaelimisha kwanza Wahindi wenzake?..kila mara anamtaja Nyerere!..ubaguzi anaolalamikia ni punje tu jinsi watanzania weusi wanavyobaguliwa na wahindi kila siku.Tena inatia huzuni kubwa…wako mabinti wadogo waliobakwa,wapo wafanyakazi majumbani waliozurumiwa mishahara!..na manyanyaso kibao kwenye makampuni yao…heee kumbe mkuki kwa Nguruwe….
    Tanzania ubaguzi upo tena wa kumwaga..tusijidanganye at nchi ya amani!..kama unabisha jibu haya maswali machache tu.

    1) Ni wahindi wangapi walioko jela au wamefungwa kwa makosa mbalimbali?…
    jibu hapa ni kama hakuna au ni idadi ndogo tu.
    Je hii inamaana kwamba wahindi hawafanyi makosa?..

    2) Kwanini wanaamua kujitenga kwenye majumba yao ya msajili kule upanga,ocean road,na samora avenue?

    3) Mnajua walitaka kumfanya nini Mengi mwaka 1994?..au mmeshasahau?..mengi alikoswakoswa kuuliwa na wafanya biashara wa kihindi..pale tu alipoamua kurusha maonyesho ya world cup 1994 na kufungua makumpuni ya IPP!..mpo hapo?…au bado mnasema Tz ni nchi ya amani?

    4)Mnajua nini kilimpata yule mkemia mkuu wa serikali alipoamua kuanika hadharani mavyakula mabovu yaliyoletwa na wahindi na wakata wawauzie watanzania hivyo hivyo kana kwamba sisi ni mamnyama au nyani weusi?…
    Yule mkemia aliuwawa!..na kesi haipo tena… imekwisha na mambo yanaendelea kama kawaida!…

    5) Ni nani machampioni wa kuingiza madawa ya kulevya nchini?….

    Sasa wewe binti …tunakuambia nyamaza tu na uache kujifanya kana kwamba huelewi hali halisi.!..ANZA NA WAHINDI WENZAKO KWANZA KABLA YA KULALAMIKA NA KUJIFANYA MSUKUMA!

  6. Jumbe Says:

    Nyie kwanini msipinge wakati huyo muhindi anaingia kwenye mashindano na akaruhusiwa kugombea huo ubingwa wa uzuri, leo kishashinda mnaanza kupiga kelele, vijana wa kiarabu wakichezea taifa stars hampigi kelele, wakigombea umisi wakishinda mnaanza zenu za kibaguzi, acheni hizo hazitufikishi kokote. Nimegundua karibu asilimia mia ya watu wanaopinga ushindi wake huyo dada ni washamba wanaotokea mafichoni shamba huko, hawana idea yoyote kuwa kuna wahindi watanzania na wana haki ya kuwakilisha taifa letu. Acheni ushamba, chukueni mifano ya nchi zilizoendelea, kwa mfano timu ya taifa ya ufaransa asilimia tisini ni weusi na wafaransa weupe wako proud na wawakilishi wao bila ya kujali rangi.Humsikii mfaransa akimponda zidane hata siku moja wakati zidane ana asili ya kiarabu. Fungueni macho na muache ushamba wenu huo.

  7. Agnes Says:

    Jivunie Dada Richa, wala usijale maneno ya hao wenye wivu, tuko na wewe mpaka dakika ya mwisho, wenye wivu walie tu na roho ziwaume, na kama inawakereketa sana basi wakajinyonge. Mwenye wivu kila siku anaishia kuzomewa tu. Jivunie Richa asili yako na taifa lako.

  8. Napenda kuanza kwa kusema huyu binti ni mtanzania halizi na rangi yake isiwachanganye mkambagua.
    Napenda sana nchi yangu sababu ya democracy tuliyonayo wote mnaruhusiwa kutoa maoni yenu na dukuduku mlilo nalo, kama mnaona binti huyu siyo mtazania toeni sababu za kumsingi siyo to kujisemea tu kuwa huyu siyo mtanzani.
    Binti huyu hana sababu yoyote ya kupoteza muda wake kujieleza kuwa yeye ni mtazania kuvipi, kama alishajieleza kuwa amezaliwa bongo na kukulia bongo, wazazi wote walizaliwa bongo nini zaidi mnataka?
    Mtu kuwa na culture nyingine kunatatizo gani? ndio maana tanzania ni nchi maridadi sana sababu kila mtu anaruhusiwa kuwa na utamaduni wake bora avunji sheria.
    Wasukuma wana utamaduni wao, wachaga wanawakwao na hata wamakonde wana utamaduni wao na wato tunawakumbatia na kuukubali utamaduni wao, Je kwanini wahindi wasiwe na utamaduni wao…hiyo haina maana wao sio watanzania….wewe uwezi jiuliza kuwa hata leo huyo binti akienda India na wewe wote mtahitajika kuchua visa kwanini sababu wote ni watanzania.
    Karibu mara tatu marekani imewakilisha na mabinti weusi, brazil imewakilishwa na weusi, wahindi na hata wa spanish lakini wote in wabrazil.
    Kumbuka kwamba wahindi ukiongelea rangi yao wanakuwa ni minority tanzania sababu ni wachache ndo maana wanakuwa pamoja ni sawa tu kama sisi weusi tungekuwa maraia wa nchi yenye weupe wengi lazima tungefungana pamoja siyo kwamba tunajitenga ila sababu sie siyo majority.
    Nafikiri watanzania tunabidi tujifunze sana somo la civics kuelewa what is citizenship.

  9. Mpenda Haki Says:

    Kuna shida 2 kwenye mjadala huu:

    Shida ya kwanza: Mtanzania mwenye asili ya kihindi kashinda umiss. Hii ni shida kwa sababu kama angeshindwa hakuna ambaye angelalamika bila kujali kwamba, kama shida ipo kwenye ushiriki na wala sio tu ushindi. Kama mashindano hayo ni kwa watanzania wenye ngozi za kijaluo tu basi shida ilikuwa awali sio kwenye fainlai. Walalamikaji walikuwa kimya kwenye hatua zote za awali za maandalizi na hatimaye kufikia fainali, mimi nadhani wawe kimya hata baada ya ushindi. Lakini sasa hapa shida imekuwa kushinda kwake. Wale wanaolalamika kwa kigezo cha asili (najua kuna ambao wana malalamiko kwa misingi mingine)wanapaswa kujua kwamba wangepinga ushiriki wa masichana huyu na wote wenye asili hiyo tangu awali. Tuliona picha nyingi sana za warembo hawa kabla haijafikia siku ya kilele.

    2. Shida ya pili ambayo ni kubwa zaidi ni tatizo la mtanzania kutokuelewa na kuheshimu sheria. Watanzania tunavunja sheria kwenye kila jambo hata hospitali muhimbili kwenye maisha ya watu tunataka kuvunja sheria. Ndio hasa inawafanya wengi wetu kushindwa kabisa kuelewa kwamba haya mashindano yana sheria na vigezo vyake. Na sheria na vigezo hivi havifuatwi kwa sababu fulani atasikia raha au atapenda, la hasha – ni sheria za kutulinda na kutupa usawa pale ambapo tungesumbuana kwa sababu ya tofauti zetu. Kama kuna sheria yoyote inakusumbua fuata utaratibu wa kuombwa kubadilishwa badala ya kuwaadhibu wale wanaoitumia kwa manufaa. Kwa sababu mashindano haya yana sheria, basi ushauri wa bure kabisa kwa walalamikaji ni kuelewa kwamba hapa kosa haliko kwa Richa, bali kwenye sheria. Kwa hiyo malalamiko yote yaelekezwe kwa watunga sheria wa nchi hii huko kwa akina Mudhihiri na Zito Kabwe (Lakini Pole sana Mh. Mudhihir kwa ajali mbaya na tumshukuru Mungu kwa maisha yako). Kumalalamikia Richa hakusaidii chochote.

    Mwisho naomba kutoa masikitiko kwa watanzania wezangu wanaolalamika kwa sababu ya Richa na kumwita mtanzania huyu ambaye wanapaswa kujivunia eti Gabachori. Kwa kweli inasikitisha sana, na nimesikia kwamba hata hili linamsikitisha sana Baba wa Taifa huko aliko. Hili kwake lilikuwa jambo muhimu kuliko mengine yote. Usawa lilikuwa ni jambo ambalo angelipigania hata kufa. Alifanikiwa kutusaidia watanzania kwenye swala la usawa. Tukajivuna mbele ya mataifa mengine kwamba sisi ndio mainjinia wa usawa na amani. Leo tumepewa kanafasi kadogo sana kakutekeleza kwa vitendo majivuno yetu tunataka kung’atana meno au kwa sababu kwenye ushindi huo kuna vijisenti basi watanzania tunaona sio halali yake. Richa kama shida ni hivyo vijisenti vinavyoambatana na hiyo taji nakusihi dada yangu kwa uzalendo mkubwa sana toa gharama zako za matumizi na warudishie hizo zingine wale wanaolalamika wapate kuridhika na wewe utatoa mchango mkubwa tu kwa taifa letu na Mungu atakulipa kwa namna nyingine. Lakini watanzania tukumbuke kuwa tutavuna tunachopanda. Tunaomba urai kwenye nchi za watu kila siku na wengine hata kwa kusingizia ukimbizi. Tunaomba uraia Marekani, Ulaya na hata India na Uarabuni, leo tunadiriki vipi hata kufikiria tu kuwatenga watnzania wenzetu kwa sababu tu Mungu aliwapa rangi tofauti na sisi.
    Tanzania ni nchi ya wajaluo, wakurya, wahaya, wamachinga, wazaramu, waarabu, wahindi, wazungu, na wale wote wenye uraia wa kuzaliwa au kuomba kwa sheria. Itakuwa jambo la kipuuzi sana kama tutaamua kuwaambia warangi kwamba hawafai kuwa Miss Tanzania kwa sababu hawafanani rangi na wajaluo.

  10. uzaramuni Says:

    BC imekuwa kila kukicha ni mahojiano ya RICHA tu.Hamna watu wa maana wengine ambao watatupa chalenji sisi?
    Kwa nza binafsi sijaona faida za Umiss zaidi ya kiudhalilisha wanawake wetu kwa kupita uchi kwenye jukwaa.

    BC editor,tafuteni watu ambao tukipita hapa tunakuwa na hamu ya kusoma na kusoma intervews zao,naona kunaanza kuwa kama news za udaku

  11. Majita Says:

    Ningekuwa na uwezo nisiongesoma hata haya maoni kuhusu huyu gabachori.Nimeandiaka nimechoka juu ya huyu Miss Patel.
    Jamani INAKERA HUYU MISS KEMCHO KUWA MWAKILISHI WETU.SI KWA SABABU NI MHINDI BALI NI KWA SABABU HAJUI UTAMADINI HATA MMOJA WA KABILA MOJAWAPO LA TANZANIA.
    Kichefuchefu.Namwombea atolewe mapema ili nifanye sherehe.

  12. babu Says:

    acheni upumbavu wenu wote nyie mnaompinga miss tanzania, mkatae mkubali huyu ndo miss tanzania 2007 na asiyemkubali kimpango wake akajinyonge. big up richa we are behind you

  13. Dj,bob Says:

    hebu, acheni, mambo ya kipuuzi, hapa Wewe dada umeshinda mie sipingi powa safi sana. ila, mie nakula koli koli na wewe nataka kujua wewe ni Kabira gani? Naomba uniandikie kilugha kwa email au nitumie tap……p_mrld85@hotmail.com
    UZAMARUNI, wewe inaonekana unamajungu sio, acha mambo ya kijinga hujaenda class nini

  14. Dj,bob Says:

    Ila,,wewe dada umefanya mbaya sana na wahindi wenzio kitendo cha kukaa na wahindi watupu ile unaonesha na wewe unaubaguzi sasa fanya kaz acha upuuz sawa? sio unapepeta domo na wahindi tu tabis hiyo koma sawa? kama husikii bas, utapinduliwa uwezo upo?

  15. Chaus Says:

    Ah, Mi naona atuwakilishe tu jamani.labda ataleta tofauti.lakini nyie mnaopinga, kwanini hamkusema chochote toka alivyoanza miss kitongoji huko? Yani hata siwaelewi.
    ALL THE BEST RICHA!

  16. Bob_Jam Says:

    Nimesikitishwa sana na watu wanao msakama binti wa watu,yeye kama raia wa Tanzania ana haki ya kushiriki mashindano yeyote kama Watanzania wengine na kushinda nikutokana na labda talent aliyonayo sasa NYOMI ZA NINI? mbona Miss UK 2005 alishinda msichana mwenye asili ya kiarabu toka Afaghanstan na watu hawakulalamika? Hebu acheni mambo ya kizamani bana kuwa Mtanzania si lazima ume na nywele za KIPILIPILI. Huyo binti anahaki sawa kama raia yeyote,

  17. Aina Says:

    Ni kazi sana sana kuupinga ubaguzi wa rangi kwa kufuata siasa. Nyie wote mnaotaka tumuunge mkono Richa kuwa ni Mtanzania na tuache ubaguzi wa Rangi my dears ni Kazi sana tena sana.

    Jamani hawa watu weupe hawatupendi kabisa sisi weusi piga ua galagaza. Wanatupenda mara tu wanapotaka kututumia.

    Nakubali Richa ameshinda, ndio mwakilishi wa nchi yetu lakini, hakubaliki na wengi wa watanzania. Hilo halipingiki!

    Na wewe Richa unasema Tanzania ni nchi ya umoja haina ubaguzi wa rangi, haya maoni yanasomwa dunia nzima, huko China wameshajua WaTZ hatujakukubali. Maswali utakayoulizwa ujiandae kujibu. Wasiokupenda ni Watanzania pia

  18. lady rose Says:

    mimi naona ni bahati yake kwakweli. hao wanaosemani muhindi wao walikuwa wapi wasingombanie .wivu tu ni bahati yake mwacheni mbona wabunge nao wahindi msilalamike naye pia ni mtanzania kwasababu kazaliwa tanzania .tunamuombea afya njema na baraka nyingi haweze kutuwakilisha taifa letu dada usijali hayo ni majungu tu si uanjuwa tena
    keep it up my sister

  19. tanwira Says:

    Ninaukubali ushindi wa richa kama miss tz 2007,kama ni suala je richa mtanzania au si mtanzania ilibidi wakwanza kulizwa wawe majaji kulizwa ni mtanzania? na ndio mana wakampandisha kwenye steji kama sababu ni rangi je watanzania wote ni weusi?.anaepanda kwenye steji ni yule Mtanzania mwenye uraia wa tanzania.
    No comment Richa big up Wakilisha tanzania achana na wasiopenda maendeleo leo richa akipeperusha bendera ya Tanzania vizuri je itatangazwa uhindi au Tanzania itawaka.huo ni UKWELI USIOPINGIKA RICHA ATAPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA NA SIO WAHINDI..
    !!!!!!!!!!ALL THE BEST RICHA!!!! Wewe ni Mtanzania watu hawaukubali ukweli ila ukweli ni huo.
    !!!!!!!!!! TANZANIAN BY NATURE!!!!!!
    MKUBALI MKATAE JUDGEMENT ILASHAPITA HATA KAMA ITABADILIK……..IITABAKI VILE VILE RICHA NI MISS TANZANIA………

  20. naj...... Says:

    jamani kilichobakia watanzania sio kudiscuss Richa ni nani ni kilichobaki kumpigia kura ya ushindi kwani uamuzi wa majaji ndio umepita kama mligundua richa si mtanzania ni mapema kuliwakilisha kwa wahusika wanaoandaa mashindano ya umiss kwahio Dua na baraka zenu watanzani ili akatuwakilishie nchiii yetu kwani ushindi wa richa ni wa watanzania wote…na dada richa tunakuomba mungu akujalie ufanye vizuri…na uweke heshima ya mtanzania kama mtanzania mila na desturi..

  21. APB Says:

    Richa,
    I would like to have and INDIAN GIRLFRIEND,
    but it is very difficult to get them.
    Richa, I believe you visit and read this blog. Can you please assist me to get an Indian Girl friend for a “serious relationship?”
    I am a black Tanzanian.
    You can use the e-mail address ZeMdau@gmail.com to give me the “hints”.
    Or if you have your friend who will be ready to accept me, its ok.
    I will give you/her my details, including a photo, after we communicate.
    Please Dear. I am serious!

  22. EUNIE Says:

    jamani jaribuni kuwa na uungwana nyinyi nyote mnaompinga Richa. Ni faida gani mliyoipata toka mmejitokeza kumpinga kwa maneno ya kejeli yasiyo hata na chembe ya uungwana? Je toka mmeonyesha kumpinga matokeo yamebadilika? Hamuoni kuwa mnapoteza muda wenu bure kwa kitu ambacho hamuwezi kukibadilisha? Acheni Upuuzi usio na msingi Ubaguzi wa Rangi Tanzania haupo, Angeshinda mwingine Richa akawa wa tatu au wa pili au hata tano bora mngesema kama mnavyomsema? Acheni Unafiki!

  23. chriss Says:

    Kwa nianze kwa kumpongeza Miss Richa,pia kumpa pole kwa kumpoteza boyfriend wake.

    Binafsi sina tatizo sana na ushindi wake kama ameshinda baada kuwa na vigezo vyote husika. Na hata kama kanunua, ni mamiss wengi wana fanya hivyo,kwani tumeona mara nyingi washindi wanakosa vigezo, na wenye vigezo wanakosa.

    Miss Richa unatakiwa kujiuliza kwanini mimi naandamwe, Je tatizo ni rangi?
    Kwa mtizamo wangu ni matokeo ya manyanyaso wanayopata wabongo toka kwa hawa wanaojiita watanzania wenye asili ya Hindia (Ila ajabu ni kwamba wakitimiliwa hapa bongo hawaendi uko kwao India isipokuwa nchi za Canada ,England na USA”tuwe makini na hawa watu jamani”)

    Hivi tujiulize iweje uzaliwe Bongo (Dar) usijue Kiswahili,ok! basi hata kizalamo nacho ushindwe,sana saana mhindi akijua lugha ya pili ni kingereza cha kihindi na sio Kiswahili,jiulize kwanini?.Maana hata kujenga hawajengi wakati ardhi kibao.
    Hivi wanajivunia na nini hapa Tanzania?

    Hivi ni nani hapa anambangua mwenzake,mimi namshangaa sana huyo anayesema tunawabagua watu weupe(tunambagua Richa Kwa sababu ya weupe).Sisi wabongo huwa tunawafagilia sana watu weupe na ukiona kinyume ujue kuna tatizo hapo??
    Kwa sababu haiwezekanaiki mtu anakunyanyasa undelee kumfangilia vinginnevyo utakuwa na mnafiki tu.

    Dada Richa tumia nafasi hii (“Pamoja na wengine wenye asili yako ambao ni wafanyabiashara wakubwa au viongozi”)
    Kwanza kulizungumzia hili tatizo kwa maana ya kukiri kuwepo kwa hili tatizo,wewe binafsi.kwa hii itatupa matumaini kwamba tuko pamaoja nasi katika hili.
    Pili uanze kampeni ya wazi(kama ajenda mojawapo katika kufanya shughulizako za jamii kama miss TZ 2007) kuondoa tatizo hili(“najua haliwezi kuisha kwa mara moja ”).
    Vinginevyo uzalendo utatushinda, na hapo watokea akina Mtikila wengine.

    Ndugu watanzania tusamahe (“najua victims ni wengi ila nawasihi”).tugange yajayo kwani Richa akishinda sifa itarudi kwetu Bongo nasi vinginevyo.

  24. nur Says:

    mimi nilikuwa supporter mzuri wa huyu binti na kupinga mambo ya ubaguzi wa rangi. lakini kitendo chake cha kuanza kukaa katika hafla na jamii za kihindi pekee ambako hata mweusi mmoja haonekani kimenifanya nimuone hana maana tena.
    Kumbe naye ni mbaguzi! loh!
    Hao wahindi mbona hata mara moja hawajawahi kukaa na miss tanzania mwingine wakampongeza. Hapa kuna tatizo. Nadhani wahindi wana kazi kubwa mpaka wakome kubagua…..basi nao hawatabaguliwa. Wajitahidi nao wakae Buguruni, Kimara, Kibangu, Mbagala na manzese kama si kiluvya ili wakubalike kama wabongo halisi..

  25. Kinono Says:

    Namuunga mkono Nur. Hata mimi nilishangaa sana sherehe hiyo hata mweusi wa dawa hakuna. Ina maana hata Mhe. LUNDENGA hakuwepo.Ama kweli Wahindi wanakuwa marafiki na wewe wanapo kuitaji tu.
    Kumbe Richa alishindwa Miss Earth 2006, kigezo kipi kitamfanya ashinde Miss world? TUMECHEMSHA.

  26. gvm Says:

    Kwanza nakupongeza Richa,Hongera sana, wakilisha vyema Tanzania

    Pili nakupongeza ndugu yangu Chriss kwa mtazamo wako mzuri sana, nilikua natafuta point ya kusema mawazo yako, sasa umenipa mwanga.

    Kutokana na maoni haya ya wasomaji inaonekana wazi kua ubaguzi upo pande zote mbili, ila kama Richa mwenyewe bado hatujajua kama yeye naye ana vielement vya ubaguzi huo, tukubali tukatae wahindi wanatubagua sana, sijasema Richa.

    Sasa kama alivyosema ndugu Chriss, basi Richa ajitokeze hadharani na kukubali kua kuna ubaguzi na ubaguzi wenyewe unaanzia kwa wahindi wenyewe dhidi ya sisi weusi ama wazawa. Mifano ipo wazi, naamini Richa wewe unafahamu hilo kama kweli umedhamiria kupeperusha bendera ya TZ basi simamia kidete swala hilo na ndilo litakuletea sifa wewe hata kukuwezesha ushinde, ningependa hata kukuita dada Richa ila sina uhakika sana kama utafurahia, nilijaribu kumuita dada mmoja wa kihindi DADA amini usiamini nilitukanwa, eti siwezi kua na dada wa rangi yake na hadhi yake na matusi mengine ya nguoni, nilikoma,inasikitisha sana.

    Richa anza kwa kukemea vitendo hivi kisha wengine watafuata. Kingine kama ukifanya hivyo na bado wakaendelea kuchonga basi hao wana yao na si kutaka amani na upendo nchini mwetu, labda walitaka watu wao washinde na si wmwingine.

    Ushauri wangu ndio huo, jitokeze kua mwanamke Mtanzania wa kwanza mwenye asili ya kihindi kusimama na kukemea kwa vitendo udhalilishaji na unyanyasaji unaofanywa na jamii hiyo, na kisha upande wa pili tutaudhibiti, au kwa kuona efforts zako watabadilika tu, hakuna linaloshindikana.

    Tuungane sote kutokomeza UBAGUZI.

    Kama alivyosema baba wa Taifa, ukimbagua mwenzio, ubaguzi hauishii hapo utaendelea kututafuna,utaanza huyu si mtanzania, huyu si mtanganyika, mara huyu si sijui nani, mara utajikuta unambagua hata mama yako aliyekuzaa.

    UBAGUZI ADUI WA MAENDELEO, pande zote zibadilike na Richa awe mfano kwa hilo

    Ni hayo tuuu…

  27. MSEMA KWELI Says:

    Heeee jamani hebu muachine huyu msichana apumuwe kidogo maana hawatoki midomono kila siku inayoenda kwa mungu,Unajuwa nini?? bahati ya mwenzako usiilalie mlango wazi,Kitu kilioneka mbeya ya watu wote, na majaji walikuwa sio wahidi walikuwa ni waafrica tu kwa hiyo mnataka kusema pia majaji hawajafanya kazi yao ipasavyo??????????????,Alipewa swali na akajibu inavyotakiwa,wewe utaulizwa swali na ujibu utumbo unadhainia utakuwa na chance ya kupata UMISS hata kidogo,KWAHIYO MNYONGE MYONGENI HAKIYAKE MPENIII, JAMANI WATANZANIA KWANINI TUSIWE WASTARABU KIDOGO.

  28. beutness Says:

    Sijamkubali hata kidogo na atashindwa tu.

  29. Chacha marwa Says:

    Kweli Mbaazi ukikosa Maua husingizia Jua!Huyo mliomtaka ashinde kashindwa sasa mnatapatapa kwasababu zisizo na kichwa wala miguu.Nyie manaojidai wazalendo wa kweli wa nchi hii na mnaojidai kuufahamu vizuri utamaduni wa TZ na makabila yake hasa nyie mlio na Ndimi chafu na za kinafiki mnaoendeleza Wimbo huu wa Ubaguzi usio na Rhythm wala beats, wimbo ambao mashairi yake yamepandikizwa vina vya fitina na mizani yake ikiwa imesheheni kisasi cha kwanini wao (wenye asili ya Asia) wanafanikiwa na kuelea katika utajiri na sisi akina Kufa kunoga twaendelea kupiga mbizi katika Umasikini. Ninyi ni wale wale mnapoombwa kuwakilisha mavazi yenu ya sili mnakimbilia kufunga Lubega kwa staili ya wamasai huku mkijidanganya eti hilo ni vazi la Asili la mtanzania wakati mkisahau kwamba hata Kenya kuna wamasai.Hata mkitukana matusi yote yakaisha Ushindi hautabatilishwa huyu binti(tena mrembo kweli) kashinda ushindi wa kishindo (makofi tumpongeze tafadhali).Wapo wengine eti wanomba kusikia sauti yake ili wa hakikishe kama Lafudhi yake ni ya kitanzania huku wakisahu kuwa makabila ya tanzania yana accent(lafudhi) tofauti wanapo zungumza kiswahili!!Ahahahaaaaa! Lafudhi siyo kipimo cha Utanzania! Wasilize wachaga, wakuria ,wajaluo, wahaya wasukuma siwezi kutaja wote, kati ya hao nani ana lafudhi yakitanzania???????Kuhusu Utamani pamoja na upeo wangu mdogo(lakini mkubwa pia)nijuavyo ni kwamba kila kabila lina utamaduniwake ambao umejengwa katika Mila na Desturi na haya yote hutofautiana katika kabila na kabila na Tz tuna makabila zaidi ya 120 ina maana (kwa hesabu ya kichwa) tuna tamaduni zaidi ya 120! Kati ya hizi ni upi Utamaduni wa Tanzania? Jibu we msema ovyo? Hapa tunajidanya hatuna kitu kama hicho na wala hatutakuwa na utamaduni wa Tanzania kadri dunia inayozidi kuwa kijiji!!!!!!Tanzania ya leo haina tofauti na marekani ambapo watu wakila pembe ya Dunia hupatikana

  30. MSEMA KWELI Says:

    KWA HIYO KILICHO WACHOMA NI HIYO SHEREHE TU????? MMMH
    HAYA …POLENI MLIYO KASIRIKA KWA KUTO ALIKWA,KWANI MTU KUKUALIKA NI HIYARI,WEWE PIA UNAHIYARI YA KUMWALIKA MTU UNAYO MTAKA KWENYE SHEREHE YAKO, HAPO UTASEMA NI UBAGUZI HUWO,MMM JAMANI HEBU WACHENI MAJUNGU LOOW!

  31. MSEMA KWELI Says:

    HILI JIBU KWA MAJITA TU, HAWA ULIYO WATEGEMEA WOOOTE WAMEJIBU UTUMBO,KWAHIYO MNATAKA KUPELEKA VICHEKESHO KWENYE MISS WORLD KAMA WAMESHINDWA KUJIBU MASWALI MADOGO MADOGO HAPA KWAO,WAKIENDA HUKO WATAJIBU NINI?KUWA MISS TZ SIYO UZURI NI KUSOMA PIA UWE NA AKILI YA KUJIBU MASWALI IPASAVYO,EG:UNAULIZWA INTRODUCE YOUR SELF UNAANZA KUSEMA WAJALEO WAONDOKA LEO MA GOD MA GOD KAMA SIYO UJINGA NINI HIYO SI AIBU KWA WATANZANI WOTE HAYO NDIO MAJIBU KWELI YA KUJIBU KAMA SIYO UTUMBO NI NINI?UKIMCHAGUWA MTU KAMA HUYO ATAENDA KUSEMA NINI HUKO ANAPO KWENDA.HATA HUYO RICHA ANGEKUWA HAJAJIBU VIZURI PIA ASINGEUPATA HUYO UMISS

  32. young girl Says:

    Jamani muacheni binti wa watu kama ushindi anao sasa nini tena?
    Richa songa mbele ndugu yangu mana hata mimi mtanzania mwenye asili ya Asia roho inauma sana nnapoona mwenzangu unakandiwa kiasi hiki kwani hili si kosa letu kuzaliwa tanzania ni wenyewe wa tz waloamua kuzaa na wa Asia je twende wapi na tunahold tanzanian passport na tumekulia hapa tz jamani acheni ubaguzi mbona nchi zingine wanapresent weusi hebu twendeni na wakati acheni wivu lah vibaya hivo na mbona hamkucomplein toka mwanzo anavyoanza vitongoji leo hii amechukua taji ndo mnachonga mhh acheni …,

    Richa kama kawaida wakilisha Tanzania…

  33. MSEMA KWELI Says:

    SAB NAKUONEA HURUMA SANA UKITAKA USITAKE YEYE NDIO MISS TZ UMPENDE USIMPENDE KAZI BUREEEEEE,TENA NASEMA KWA WOOOTE WANAO MCHUKIA HUYU MSICHANA NI ASARA YAO,WOTE WALIYO ENDA HAWAKURUDI NA USHINDI NA KAMA HUYU PIA MUNGU HAJAMJALIA BASI ITAKUWA BAHATI MBAYA KAMA WALIYO TANGULIA, KWA HIYO UNATAKA KUNIAMBI WOTE WALIENDA HUKO NA WAKAKOSA USHINDI WALIENDA KUUZA SURA ZAO???

  34. Emmanuely lyimo Says:

    Mi napenda kutoa pongezi zangu za dhati kwa majaji walio usika na swala zima la kumtafuta miss tz, pia napenda kumpa pongezi zangu za dhati Richa kwa kunyakua taji hilo la miss Tz,Mi binafsi nilifwatilia haya mashindano kwa umakini mkubwa,tokea mwanzo hata kabla ya kwenda kambini,Napenda kumwambia Richa aongeze bidii,ubunifu,mbinu mbali mbali ili aweze kushinda.Wa Tz wenzako tuko nyuma yako,Usijali Tuna kupenda sana.

  35. Baraka Says:

    Mtanzania sio mtanzania lakini mimi nampenda na anapendeza,
    Jibu lakusema ni wahindi wacheche gerezani ninalo

    Kwasababu ni wahindi wachache sana kwenye jamii hii yetu ya weusi, Tanzania tuna mamilioni ya watu, je huyo anayesema wahindi ni wachache gerezani anajua ni wahindi wangapi wanaishi Tanzania? acheni umbea usiomifaa.
    Na kama hawako gerezani pengine nikwamba ni maadili wanayopewa majumbani kwao kwamba kuiba sio kuzuri.

    Majumba ya msajiri, mmh hebu acheni umbea, hata huko marekani kuna china town, brooklyn au black neighbourhood, watu minority lazima wawe sehemu moja ili wapeana sapoti kuhusu asili yao.
    na wengi wa waswahili hapa wanaoishi nje basi wako kwenye maeneo ambayo wanaishi waafrika wengi huko ulaya.

    Kesi ya mavyakula mabovu

    Mmeiona hio tu, ni issue ngapi zinafanywa tena na wakubwa WEUSI wa tanzania, na tena hio ya mavyakula mabovu waanzishaji wakubwa ni wakubwa wetu hawa hawa, kwani kama wangefanya kazi zao vizuri basi asingetokea mtu yeyote wa nje kuleta mavyakula mabovu.

    Madawa ya kulevya ni hivyo hivyo kama serikali yetu ya weusi isingekua na rushwa basi hao watu wasingepata mwanya wakuingiza hivyo vitu.

    Kwahio kwa hoja hizo hapo juu nikwamba watanzania WEUSI tunajiua wenyewe.

    I hope u get your answers, kama hujaelewa elewa

    Tanzania yetu ya weusi hii tunajiua wenyewe.

  36. kasera Says:

    JAMANI PIGA UA JAPOKUWA HUYO RICHA NI MZURI LAKINI HAIKUFAA YEYE KUSHINDA. KWANZA YEYE NI MHINDI HANA CHOCHOTE KINACHOONYESHA KWAMBA YEYE NI MTZ. SASA WAKIKUTANA NA MISS INDIA HUKO CHINA SI INDIA ITAKUWA NA WAWAKILISHI WAWILI……NAMTAKIA KILA KHERI LAKINI..MUNGU IBARIKI INDIA NA WAWAKILISHI WAKE WAWILI.
    kansas city

  37. gvm Says:

    Jinsi wadau mnavyozidi kutoa maoni inaonekana kama tunarumbana, napendekeza tuseme nini cha kufanya ili kurekebisha hali hii isiendelee tena, hapa kuna tatizo, na kama tatizo lipo asitafutwe mchawi nani, tutafute suluhu na si marumbano…

    Binafsi nakasirishwa sana na vitendo vya kumponda binti huyu,kwani naamini si wahindi au wazawa weusi wote wenye tabia hii ya ubaguzi, na hii inamaanisha Richa kua au kutokua kwenye kundi moja wapo katu ya hayo. Bado nasisitiza TUFANYENI KAMPENI YA KUTOKOMEZA UBAGUZI NA UNYANYASAJI TANZANIA, dada Richa aongoze vita hii.

    Hapa naomba nieleweke vizuri jamani si vinginevyo, otherwise bado namuunga mkono Richa na nakuombea mema utuwakilishe vyema.

    MUNGU YU PAMOJA NAWE, MUNGU YU PAMOJA NA WATANZANIA WOTE WENYE MIOYO SAFI…

  38. santana Says:

    Kweli Tanzania tuna Uhuru wa Bendera tu kwani hata kwenye shindano la kijinga kama umiss tumeonesha kwamba bado ni watumwa kwenye ubongo. Kama Ike alivyosema leo miss anakuwa mhindi jamii ile ile ya watu wanaoongoza kutapeli serikali yetu, kutuletea madawa ya kulevya na wanaotubagua sisi weusi kila siku kwenye biashara na kampuni na hata majumbani mwao kwa kuwabaka, kuwatesa, na kuwaita mambwa na matusi mengi mengi.

    Kila ukisikia habari ya rushwa serikalini lazma kuna mhindi kahusika; na hata siku moja usikii mhindi kalazwa jela hata aue mtu kwasababu serikali na sheria iko mikononi mwao na washanunua nchi sasa jamani kama wamenunua serikali na hata kwenye burudani za kijinga na zisizo na msingi kama hizi pia wameshanunua. Iweje mhindi aweze hata kushiriki kwenye umiss? Basi kwesho keshokutwa tutaweka mkaburu kwasababu hawana tofauti na wakaburu hawa watu wamenunua nchi na wanatesa watanzania watakavyo. Inaniuma sana ila ndo athari za kutawaliwa na kwasababu tulishatawaliwa basi tutabaki watumwa milele kwani sio serikali wala wananchi wetu ambao wanadalili ya kutukomboa!!!!!!!!!

  39. SEOUL CITY Says:

    MIMI NAOWAOMBA WATANZANIA WENZANGU WAACHE HAYO MAMBO YA UBAGUZI KWANI..HATA WATANZANIA WENYEWE WEUSI WANABAGUANA UTASKIA HUYO MSAMBAA AU MKIKUYU,NA HATA WENGINE WANAWABAGUA WATU KUTOKA ZANZIBAR ETI WAPEMBA HAO WAACHENI..HAYO NI MAMBO YAMEPITWA NA WAKATI HUO NI USHAMBA MKUBWA..WANGAPI WALISHAPITA WEUSI NA WAMEFANYA NINI?MBONA HAO WASHIRIKI WALOPITA WAZAZI WAO WENGINE SI WATANZANIA VILEVILE MBONA HAMKUSEM AU KWASBABU NI WAZUNGU…ACHENI HIZO PUMBA JENGENI NCHI HIYO UBAGUZI HAUTOWAFIKISHA POPOTE..HONGERA RICHA[MIS TANZANIA]

  40. mac b Says:

    Jamani kusema ukweli hakuna haja ya kumsakama Richa kama ameonekana anafaa basi ana haki ya kuwa Miss Tanzania. Ila naomba tuu awe balozi wetu pia kwa hawa watanzania wenye asili ya kiasia kuwa wasiwakataze mabinti wao kuolewa na watanzania weusi. Nasikia eti ikitokea binti wa kiasia amegundulika hata tuu kuwa na friendship ya boyfriend vs girlfriend na mweusi anatengwa na jamii yao. Yaani inakuwa kama vile amewadaririsha kwa kutembea na njemba nyeusi sijui wanaona ni kama nyani??? nashindwa kuelewa wakati wanaume wa kihindi hawaishi kuwafuatilia mabinti weusi tena kwa lazima au hata kuwabaka mara ingine. Sasa miss Tanzania wetu tunaomba uwaelimishe hao wahindi wabaguzi wa kina kuwa wakati wa mabadiliko ni huu sasa na sisi watanzania weusi tupewe nafasi ya kuwaoa wanawake kama wewe wenye asili ya kiasia. Mimi nitakuwa wa kwanza maana nawatamani kichizi. Tunakutakia uwakilishi mwema na wenye mafanikio kwenye Miss World!!

  41. Patel Says:

    We santana kweli we bado limbukeni wa kutupwa! kama shindano ni la kijinga kwanini inakuuma?we ndo bado mtumwa wa ubongo kama hao wahindi wanaleta madawa ya kulevya kwanini wewe mweusi unayanuna?si unaweza kuboycot?kama wanawanyanyasa majumbani kwao mnafuata nini huko? kwanini msiende kufanya kazi kwa akina masawe na chacha marwa?kama hao wahindi wanatoa rushwa je wanopokea ni akina nani kama si wewe na wenzio tunaojiita watanzania halisi!huku sheria imesema mtoaji na mpokeaji rushwa wote ni wahalifu!Jinsi usivyo na ufahamu wa kutosha eti unadai hakuna mhindi aliyelazwa jela hata kama ameua!!!!Mbona katikati ya miaka ya 90kuna mhindi alihukumiwa kunyongwa hadi kufa mjini Mwanza kwa kumuua kwa makusudi mfanya biashara tena mhindi mwenzake! we snatamaria namna gani

  42. CASHMONEYHOLLAND Says:

    KAMA KAZALIWA BONGO NIMBONGO…MZURI MZURI…KWA NYWERE TU KAWASHINDA WOTE KWANI HAITAJI ZA BANDIA…SASA HIVI MWACHENI AKALETE MISS WORLD BONGO..HATA ANGECHAGULIWA MWAJUMA TEMEKE JE ANGEFIKA WAPI IKIJA MASWALI YA KIINGEREZA…SIJUHI JINA LAKO NANI SEMA NAKUPA MIA KWA MIA TOP TEN UMEKULA CHINA.

  43. Kamongo Says:

    Mh, jamani waTz mna majungu jamani loh! Alishinda Amina Chifupa, mkalalamika weeeeee. Akafa,mkakashifu weeeeeeeeeee. Sasa kashinda huyu dada wa watu, mtasema weeeeeeeeeee, akifa ndio atatupiwa kila aina ya kashfa. Yaani waTz hiv huwa hamna kazi za kufanya badala ya kupoteza muda kwa umbea usiokuwa na maana? kashashinda sasa, mtalibadilisha hilo? Waliomchagua sio wajinga. Kama wenye ngozi nyeusi wenzetu walishindwa, ina maana hawakuwa serious na masharti ya mashindano. Maana kama kawa waTz huwa wanadhani kila kitu ni rahisi rahisi tu. mtu kashawaambia alishindana miss earth, that means anajua kila sheria na kigezo cha kumfanya mtu ashinde. Je, kati ya hao washindani wenzie kuna hata mmoja aliyewahi kushindana miss earth akapata idea of what to do ili ashinde? Hakuna! Sasa fungeni mabakuli yenu na muache kulalamika ujinga. Wahindi wenzie walimfanyie sherehe ya kumpongeza, kama mnataka na nyie mfanyieni,hakuna anayewazuia. Au mfanyieni mshindi wa pili ili iwe ngoma droooooo. Mimi ni mweusi, lakini tabia ya weusi wenzangu ndiyo inayoniuzi hadi nimeamua tu nitulie zangu huku mamtoni. na sirudi ng’o! maana majungu yasiyokuwa na mpango is not my thing at all.

  44. queen Says:

    kweli nimeamini wengi wa watanzania hatujaelimika wala hatutaki kuelimika.na kama tutaendelea hivi hivi na ujeuri wa kukataa kuelimika, basi nchi yetu itaendelea kuwa ya mwisho duniani huku ikiwaacha wachache wenye moyo wakuelimika kusonga mbele na kuihama nchi na kukimbilia nchi zingine zenye maendeleo na kutokurudi nyumbani kamwe.kitu kidogo kama uraia, mtu haelewi maana yake ni nini!watu wenye akili zao wamejaribu kuchangia hii mada kwa kila hali, lakini wapi!haliwaingii akilini.hamna kisomo.ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa acheze!inanishangaza sana.kama huyu msichana ameshinda kwa vigezo vyote kelele na lawama ni za nini?kwani majaji walikuwa wahindi?Yeye anakosa gani na amevunja sheria gani? ninachoshauri kwa wale wasiojua maana ya uraia waende shule au wanunue kitabu wasome.Bint wewe ni Mtanzania uliyezaliwa Tanzania pamoja na wazazi wako, nenda kaibebe bendera ya Taifa lako kwa kifua mbele bila kujali maneno ya walala hoi wachache wenye hasira na maisha ya shida yaliyosababishwa na roho zao mbaya na uvivu wao na umaskini wa kutokwenda shule na ujeuri wa kutotaka maendeleo yao wala ya wenzao.chuki binafsi.wanaokutukana dua zao zitageuka kukupa wewe ushindi.ninakuombea sana ushinde wabaki na aibu.Mungu akusaidie Amin.

  45. Galilo Mtemi Says:

    Yes ndugu kamongo. Waambie hao, wanatufanya tusirudi home TZ maana hakuna utakalofanya likaonekana zuri.Aliposhinda miss wa mwaka jana Wema Sepetu,walisema mbaya hakustahili kushinda. Sasa kashinda huyu mzuri, hawamtaki. Dada Richa wala usisikilize maneno ya wakosaji. U deserved the crown girl.And u r so beautful. I love u and U will win the miss world pagent. If u read this comment, know that all the Tanzanians who r in U.S.A and China too are supporting u 100%. Good luck princess.I call u princess coz U r a princess.;)

  46. Adrian Says:

    Tena mnyamaze kabisa watanzania. Akirudi na ushindi mtaanza kujigongagonga. Halafu mtaanza kujifanya mnamfagilia. tena nyamazeni kabisaaaa. Muacheni mtoto wa watu. Ni Mtanzania huyo sio tu kiduniani. Hata mbinguni, Richa ni Mtanzania.Tena mnyamaze kabisaaaaaaaaa. Dada wa watu ni mzuri na ndio kinachowakera. WaTanzania hamna jema. Ndio maana umaskini hauishi. Maana kila akijitokeza mtu wa kuwakomboa, tayari mnanyanyua midomo. Huko ni kukosa akili

  47. KANSAI JIN Says:

    Hongera sana Miss Tanzania ,
    Watanzania tumpe support huyu dada aweze kurudi na Taji la miss World . Idadi ya Wahindi waishio bongo ni ndogo sana kulinganisha na idadi ya watanzania weusi . Hivyo kwa wao kukaa pamoja mfano Upanga , nyumba za msajili si kitu cha ajabu …. hii inawapa urahisi kuishi ktk hali ya kusaidiana ,na amani zaidi hata sisi tuliopo huku ughaibuni tuna jumuia mbali mbali ….mfano ukifika maeneo ya Yokohama ( Sagamihara) utakuta kuna wabongo zaidi ya mia tatu wanaishi huko …ukifika Osaka ( maeneo ya Miki ) utakutana na Wapopo ..nigerians wanaishi huko hivyo sisi Watz ni wakati wa kubadilika.
    wahindi wana jumuiya nyingi …. lakini wengi wao ni budhidist hivyo kwa wao kukusanyika na kumpongeza Miss tanzania si kitu cha ajabu …wewe mbongo huna ulazima wa kuwepo hapo kufanya nini … ili mradi uonekane ur black person …lol.. hii ni sawa na kusikia jumuiya ya wachaga waishio dar wamekusanyika kujadili maendeleo ya kwao sasa unataka mmakonde wa newala awepo pale kufanya nini .. he can support nothin.Kwa taarifa yako wahindi wana uwezo wa asilimia kubwa ya kushinda miss beutiy popote pale ulimwenguni if are well trained
    ciao
    Kansai Vehicles ,Osaka

  48. yoa Says:

    richa ndo miss wetu mtake msitake,majitu mabaguzi ka nini!all the best richa

  49. Bob Sankofa Says:

    Bado Richa anayo support yangu, jamani inatubidi tuelewe kuwa alichoshinda Richa ni shindano la “Miss Tanzania” sio “Miss Black Tanzania”. Sitashangaa iwapo Richa atashika nafasi za juu katika Miss World na ndio hapo nadhani hata wanaompinga wataanza kuona kisawasawa. Ni hayo tu.

  50. lulu Says:

    SASA BAADALA YA KUKAZANA KUTUJULISHA KUWA YEYE NI MTANZANIA SIKU ZINASONGA MBELE, AJIANDAE NA MASHINDANO TUNAONA HATA PICHA ZAKE BADO HAZIJAFIKA KWENYE WEBSITE YA MISS WORLD ANAONA VIGEZO VYAO HUKO ILI KUINGIA FAINALI LAZIMA KUSHINDA AIDHA SPORTS, BIKINI, TOP MODEL NA TALENT SASA AJIANDAE NA KU JOG NA MAZOEZI YA KUTOSHA BASI SIJUI SWIMMING NINI MPIRA KURUKA AU ANAENDA TU KUTALII HUKO CHINA? NAONA HILI MOJA LA UTANZANIA LINA CHUKUA MWEZI MZIMA!! ASHIKE KAULIMBIU YAKE MOJA YA MAZINGIRA AIVALIE NJUGA AFANYE KAZI ZA JAMII ZA MAZINGIRA APELEKE VIDEO YAKE HUKO MISSWORLD AJIFAGILIE ACHUKUE TAJI SIO KULETA STORY ZA KILA MWAKA ZA ASIEKUBALI KUSHINDWA SI MSHINDANI NA APUNGUZE KUCHEKA CHEKA OVYO, HIYO KUSUKA NA KUVAA KHANGA NA VILEMBA POA SANA ATAONEKANA UNIQUE LA MWISHO ASIWE MWOGA EBU AFUNGUE WEBSITE YAKE AU BLOG TUPATE KUWASILIANA NAE TUMPE MAWAZO NA AYAFANYIE KAZI ALETE TAJI BONGOLAND!!AKUMBUKE MISS WORLD WOTE WALIOCHAGULIWA HAWANA MAPOZI YA OVYO WAPO HUMBLE! AJARIBU KUWASTUDY KIUNDANI SIO KUWA MATAWI YA JUU HUKO CHINA! KILA LA HERI BIBIE RICHA!

  51. Neema Says:

    Mnaomuunga mkono ni walewale mnaoogopa ngozi washamba kabisa. nyie mnawajua hao wnaojiita waTZ wakiasia walivyo na ubaguzi na dharau??? huko nikujidhalilisha waTZ, mmeshaona mambo kama hayo kwa mataia mengine ya Afrika? ukiondoa SA ambayo tayari ina mchanganyiko wa Weupe na weusi kwa asili? au hata nchi za kaskazini mwa Afrika? acheni ushamba. huyo nu mhindi akagombee huko kwao angekuwa mtanzania kwenye sherehe ya kumpongeza mliona weusi pale?? kama wanajua yule ni mTZ kwanini wasiwaalike waTZ wenzie wajumuike, MIMI SIMKUBALI KABISA inonyesha jinsi nchi yetu ilivyo dhaifu…

  52. Neema Says:

    ni kweli mnapoishi mahali ugenini lazima muishi kwa umoja mkisaidiana mkijijua kuwa NINYI SI ASILI YA NCHI ILE SI WAZAWA na nidio sababu hamshiriki kwenye mashindano ya kutafuta nafasi ya kuiwakilisha nchi. hivyo dugu yangu Kansai kumbe nawe bila kujua unakubali kabisa kuwa Richa ni MHINI sio mtanzania au sio? mi nachojua kama Watanzania huwa ni kitu kimoja na hatujali tunaishi wapi lakini tunashirikiana pasipo kujali makabila sasa hushangai wao wanajibagua, Watanzania gani haoo?

  53. Nyamf Says:

    Hana mvuto, issue apo sio uhindi angekuwa bomba kila mtu angekaa kimya!

  54. Dinah Says:

    Naheshimu yote yaliyosema hapo juu, lakini tambueni kuwa sisi watanzania weusi au mweusi popote Duniani sio wabaguzi bali tunahasira kutokana na vitendo vya ubaguzi vinavyoendeshwa dhidi yetu.

    Hawa Wahindi wasingekuwa na tabia ya kujitenga, kunyanyasa na kubagua watanzani wenye asili ya kiafrika ambayo ni WEUSI si dhani kama kuna Mtz hata mmoja angetamka neno lolote la kibaguzi.

    Kwa vile Watu hawamkubali kwa vile ni Mhindi anahisi kubaguliwa lakini sisi weusi tunavyobaguliwa na hao kaka na baba zake haoini kama tunabaguliwa sio?

    Hii haina tofauti na ile issue ya CBB kule UK, Shilpa alipobaguliwa basi wahindi wakaja juu nakuonyesha kuguswa na kuumia……mlijiuliza kwanini? Ni kwavile wao wako hivyo na hawapendi kufanyiwa vile wanavyofanya. Kwamba wanabagualakini hawataki kubaguliwa.

    Huyu Miss Tz India huenda kweli kizazi chake kilianzia hapa lakini sidhani kama ni zaidi ya miaka 60 iliyopita tofauti na Waarabu kupigania Utaifa wa bongo kutokana na historia sio wahindi.

    Kazi aliyonayo kama MissTz India sio kuwakilisha Bongo nakupeperusha Bendera bali kuelimisha wahindi wenzie waache kunyanyasa nakubagua wabongo weusi ndani ya nchi yao.

    Tuleteeni khabari za watu wengine wa maana kwani hii inatia hasira tu.

    Wanatabia ya kuua ikiwa wanahisi wanaandamwa au kuumbuliwa (Yule Mkemikali) au kushindwa kibiashara (walitaka kumuua Mengi)sasa watuue sote.

    Watz wazawa weusi wakatiumefika kutokenua-kenua tunapobaguliwa na hawa watu. Tulitawaliwa na Waingereza, Wajerumani na Waarabu miaka ile kabla sijazaliwa ila sasa hatuwezi kutawaliwa na watu wa Dunia ya 3 kama sisi ei.

    BC kazi nzuri apart from this Miss TZ India.

  55. Dinah Says:

    Manaozungumzia SA ni tofauti kabisa na Tz, Wazungu kule ni kama waarabu hapa Bongo, wanahistoria ndefu zaidi ya miaka 100 pia ni wengi wa kutosha na wanajichanganya pia hawaendelezi tamaduni za kikwao bali za KiTz tofauti na WAHINDI.

    Acheni kubabaikia Rangi wabongo weusi, fungueni macho mjikomboe……Good job Miss World means Nothing 4 most of us vinginevyo akyanani hali ingekuwa mbaya na hako ka-miss Tz india kenu kangeishia mikononi mwa pilisi.

    Oh nimesahau….Richa akishika nafasi ya juu ni kwa vile wahindi wenzie watampigia kura kama mhindi na sio kama Mtz. Hawa jamaa wako kibao na when it comes to muhindi wanahakikisha wanaunga mkono.

    Nina hakika Ma-miss wote waliopita hakuna mhindi aliyepiga kura kwa vile sio “hawakuwa wahindi”.

    Mimi sipigi kura wala kula……na since kashinda najiita Mbongo sio Mtz tena mpaka mashindano yaishe kwani ni AIBU kuwa Mtz kuwakilishwa na kahindi.

  56. mboni Says:

    richa hatumpendi kwa sababu ya uhindi wake ndio ana utanzania kwa sababu alizaliwa bongo lakini bado ni mhindi hata kama kazaliwa bongo ataenda kutuwakilisha kivipi watanzania wakati hana asili ya kitanzania ana asili ya kiasi angeenda kugombea india kwao huko huyo gabachori watanzania wazuri wenye asili ya kitanzania wameachwa kama kigezo ni kujibu maswali vizuri na sio uzuri hapo majaji wamechemsha sana

    ameshachaguliwa hatuna la kufanya ila majaji wajifunze mwakani wasituchagulie tena wahindi, kama wanataka wahindi waende huko india wakagombee huko kwao hatutaki kuona tena huo uchafu wa kihindi

  57. Salma Says:

    Mnaosema Richa hafai,HAMNA AKILI KABISAAAAAA

  58. Nefertiti Says:

    THIS IS NOTHING BUT NEO COLONIALISM……..WANATUTAWALA KIUCHUMI…BASI HATA IMAGE YA NCHI……LOH…RICHA OR WHATEVER YOUR NAME IS….YOU ARE NOT A TANZANIAN AND NEVER WILL BE IN ANY HSAPE OR FORM…JUST LIKE THIS HEHE GIRL WILL NEVER BE A HINDU OR GOA…….. LUNDENGA HONGO ZINAKUPELEKA MBALI…UNAUZA UTU WAKO PIA
    NDIO MAANA WEUSI HATUENDELEI…AENDE BASI MMAKONDE AKAGOMBEE MISS INDIA TUONE…NYOOOOO

  59. Nefertiti Says:

    SALMA UNAESEMA HATUNA AKILI..ASANTE SANA HUJAKOSEA. MWENYE AKILI WEWE NA AKINA LUNDENGA MAANA HAMJIJUI WALA HAMJIFAHAMU.
    DUNIA NZIMA MTU HUTAMBULIKA KWA RANGI YA NGOZI…NYIE MNAOJIDAI WAZALENDO KUWA WAMATUMBI SIKU HIZI NI WEUPE PE….BASI RICHA KAKUONESHENI KATIKA HAFLA ALIYOFANYIWA NA WAMATUMBI WENZIE…WEUPE KAMA YEYE….. WEWE NA AKINA LUNDENGA MLIKUWA WAPI KULA HIZO PONJORO PARTY…
    WAKE UP AND SMELL THE COFFEE….
    KWA YULE ALIYE LINGANISHA USA NA TZ ASOME HISTORIA YA NCHI.
    AMERIKA NI NCHI YA WATU WAKUJA (IMMIGRANTS INCLUDING AFRICANS BROUGHT IN SLAVERY !) HUWEZI KULINGANISHA NA TANZANIA BWANA.

    NAMPENDA MWALIMU NYERERE SANA… LAKINI KATIKA MAKOSA ALIYOTUFANYIA TANZANIA KUBWA KULIKO YOTE NI LA KUKABIDHI UCHUMI WETU KWA AKINA JAMAL AND THE INDIANS….GOD ..I COULD PUKE…..! TUNABAKIA MASIKINI KWA SABABU SISI WEUSI NI WANAFIKI TUNAJIFANYA WAZALENDO HATUONI WANAYOFANYA HAWA WAGENI (PESTS)INDIANS….TIZAMA WANAVYOJIBAGUA KWANZA…. CASTES – NI ASILI YAO HAWAWEZI KUJIZUIA.

    CALL ME A RACIST AND A BIGOT…. WHEN IT COMES TO INDIANS…I WILL TAKE IT WITH GREAT HONOR AND PRIDE.
    IF YOU ARE NOT THEIR HOUSEGIRL…OR PUPPET LIKE THE LUNDENGAS THEY WILL NOT EVEN LOOK YOUR WAY……

  60. cool Says:

    mie namsapoti dinah hawa ni wauwaji wakubwa si unaona walivyomfanyia hata amina yani huyu manji ni muuza unga namba noja we mwache jk amkumbatie sie tunamlia timing tu hapa airport

  61. jennifer Says:

    jamani kunawatu wanajua mwaga risala humu tena yenye pumba lo.. kazaneni

  62. KANSAI JIN Says:

    Watoa mada tunatoka nje ya mstari … main point ni kuwa huyu Miss Tza 2007 asiiwakilishe tanzania ktk mashindano ya dunia coz sio Mtz…Tutumie hoja zenye nguvu na siyo ghadhabu tu au kutokuwa na data kamili .
    Haya mashindano hayakuwa ya Miss Black tanzania 2007 hivyo mtu yeyote aliwakuwa na haki yake ya kushiriki provided ni Mtza . Tanzania inaundwa na matabaka mbali mbali…means that kuna watanzania asilia,wazawa ( blacks) europeans , Hindus , Asians..( hapa kuna Indians, Filippinos ,Koreans etc ) migrants
    tuangalie basi katiba yetu inasemaje kuhusu migrants wanaokuja Tza …wanapewa haki gani kushiriki ktk mambo gani ya Taifa . Tukimuangalia Miss Richa anasifa zoote yeye ni Mtanzania kwani amezaliwa ndani ya bongo yetu anayo haki ya kuiwakilisha Tza popote pale . Nchi yetu pia iko mbioni kuwa na double Citizenship hivyo hata baadaye akitaka kuwa Mdosi , mUSA, MPOPO ni sawa kwani ana haki kikatiba vile vile kama wafanyavyo wabongo wengine .
    BI Neema , Ms Mboni na Mr Dinah ref to hoja zenu tuangalie kwa mapana na marefu kuhusu suala la rangi ya ngoz ktk utaifa …. kuna kizazi kingine nacho kinakuja kwa nguvu ** HALF CAST ** je hawa tutawakatalia wasishiriki kwasababu one of their parents they colonised us
    je ni nani asiyejua kuwa wakoloni walitutesa , kutudharau , kubagua na hadi kutuuza watumwa …
    i need to hear your coments abt this too guys angalia jamaa aliyeshiriki Mr Big brothers pale RSA last year … jamaa ni half Cast .. mbona alipata support kubwa toka kwa Watz …jee wazazi wake hawa hawawatesa wabongo kwa kuwapiga mijeledi ,kuwafanyisha kazi kwa ujira mdogo .Au coz alishinda nafasi ya pili basi tuwe kimya …
    hivyo tuangalie katiba yetu ya nchi inasema nini kuhusu migrants ..wana haki ya kuiwakilisha Taifa .
    Mzee wa Kansai ,Osaka

  63. KANSAI JIN Says:

    Matatizo ktk jamiii … wengi wa watoa mada wanaelezea matatizo ktka jamii na si kwanini MISS Tanzania 2007 asishiriki kuiwakilisha taifa ktk MISS world , watoa mada wanaelezea zaidi uingizaji wa madawa wa kulevya , kutukanwa , kuwekwa mbaroni etc …. ni wajibu wetu kuwashtaki katika vyombo vya dola vilivyopo..simu za akina Tibaigana ziko nje nje kwanini tusiwaeleze vyombo vya dola kuwa kuna hiki kinatendekea badala yake kubaki na kulalamika tu ….tutumie akili zaidi.
    kina side effects mbali mbali pindi migrants wanapoingia kama uingizaji wa silaha , madawa ya kulevya hii husababisha culture shock kwa wazawa asilia … watz tusikae kimya tuwashitaki mara moja pindi tunapoona uozo unapotokea badala ya kunyamaza na kupiga domo tu . Vyombo vya dola vipo nje , watekelezaji wapo chonde chonde tuwashitaki ASAP
    She needs your support esp from Ms Neema , Dinah and Mboni too . Keep it up Ms Richa
    we love you and we are cheering for you .
    Mzee wa Kansai ,Osaka

  64. Sebastian Says:

    hebu jaribuni ninyi weusi zamieni India halafu mkagombee umiss huko india muone kama hamjatupwa kama mbwa. Unajua nyie waTZ mnaoshabikia uhindi ni walre ambao mpompo tu na hamwelewi lolote juu ya nchi yenu na hata ulimwengu kwa ujumla. nimejaribu kuongea na baadhi ya raia wa kigeni waishio hapa, na kila niliyeongea nae alionyesha kutushangaa waTZ, tunaonekana ni watu tunaofanya vitu pasipo kuelewa tunajifanya tunajua kumbe hatujui tufanyalo tunaonekana uelewa wetu ni mdogo sana. ni kweli hatupaswi kuwa wabaguzi wapo mataifa mbalimbali wana uraia wa Tz manake ni WaTz, je mwaka ujao tutapeleka wachina kutuwakilisha manake wapo.lakini katika nafasi muhimu kama hizo tunazotakiwa kuutambulisha UTanzania wetu lazima tuchague mtu ambae kwa hakika anapotokeza mbele ya kadamnasi mara moja anaeleweka kwa urahisi haiachi maswali vichwani mwa watu wakashindwa kuielewa hasa Tanzania ikoje? kumbuka nchi yetu baado kabisa inahitaji sana kutambulishwa watu wengi hawaifahamu tunapopeleka mhindi wanashindwa kuielewa kama watu wake wanafananaje nchi ya kiarabu ama kihindi au ni vipi…..

  65. NZWIIIIII!!!!!!!!!!!!!!!!!! Says:

    hili swali ni kwa watayarishaji wote wa mamiss!!
    je nini maana ya KUSHIRIKI UMISS????kwani kinaangaliwa ujibu mzuri wa maswali au ana vigezo vipi???? kama jibu litakuwa ni vyote kwanini hamtoi trainning nzuri kwa washiriki wote ambao wanavigezo vya kugombea u miss world mimi nauhakika kabisa training wanayopata mamiss ni ndogo sana haiwezekani mamiss wote washindwe kujitetea na kujibu maswali….kama ni miss kigezo kikubwa ni elimu basi muchague wasomi…ili ijulikane ma miss wa elimu.mi nauhakika kabisa watotoa training wa u miss- lazima wanatoa mafunzo muhimu kwa yule wamtakao na si kwa ujumla….

  66. shuwea Says:

    RICHA……
    Nauhakika ujumbe utausoma hata kama hutosoma utasomewa ila mimi ni meukubali ukweli kwani itabidi ni ukubali kuwa wewe ni Miss wetu na si Miss Tanzania.Nitakubali kama wewe ni miss Tanzania pale utakapo waelimisha wahindi wanaoishi Tanzania kuacha Ubaguzi Ubinafsi na Uchoyo.kwani tokea umetwa taji hili hujawai kulizungumzia suala la tofauti mlizonazo wahindi na waafrika…na unalijua hilo je? watambua kwanini watu wanakupinga si kwamba si mzuri ni mzuri unavigezo vya u-miss ila kutokana na tabia ijulikanayo na wewe ndio hiyo unayo mhindi ndio mana watu wanakupinga…kama kweli mtanzania utatudhihirishia we mtanzania basi uooneshe watanzania wapoje……mimi nitakuunga mkono kwa kuwa ndio nimeukubali ukweli ambao wakulazimishwa ila tudhihirishie watanzania kuwa wewe ni mtanzania nandhani umenielewa.na kama unatabia hizo walizo nazo wahindi wenzio basi umepotea.Big Up Richaaaaaa

  67. anna Says:

    Jamani kwani mmeisahau nchi yetu kwa kupenda rushwa,Unaweza ukaniambia we Mtanzania udhulumiwe na muhindi au mtu yoyote asiyekuwa na asili ya kiTZ au kwa maana nyingine mtu mweupe,nani atakaeshinda kesi kama sio huyo mtu mweupe,Amini usiamini huyo miss Tanzania ni michosho mitupu,wanatuchora tu Watanzania,Unadhani mie ninaweza kupresent picha ya Huyo Baniani kwa mwafrika ambaye si Mtanzania na kumwambia huyu ni miss TZ si ataniona mie chizi?
    Wabongo tusiwe wadhaifu na kukubali kutawaliwa.

  68. ANNA G Says:

    Huyo ni Kabachori tuuuuuuuuuu.Watanzania wapo wenye culture ya Kitanzania.Hapo tutawapa watu maswali na kujiuliza hivi Tanzania siku hizi ni wahindi.Ubaguzi wanao saaana tu hasa wenyewe wahindi si kwenye biashara kila mahali.Wao ndio wenye nchi nashangaa sana tena sana kila kitu kizuri ni wahindi tu whyyyyyyyy.Huko kwao India wanakandamiza umaskini wa kufa mtu hapa wakifika wako Ulaya.Siwafagilii hata kidogo.Wahindi wahindi tu si unaona hata hiyo partu anjichanganya na kabachori wenzie.Okay Richa ushachguliwa wewe kupeperusha bendera ya Tanzania unatakiwa kujichanganya na watz sasa.Si kuuza sura kwa wahindi wenzio tu.Unajua si kwamba hatukupendi ila nyie wahindi ni wabaguzi sana.Hata shule mmejitenga waaaiiiiiiiii.Sijui niwagroup wapi mie nishachoka.

  69. salma Says:

    JAMANI HUYO BANIANI ANATUTIA AIBU,WAMEACHA WATOTO WEUSI MASKINI WENYE ASILI KAMILI YA KIAFRIKA NA KUWEKWA UYO MLA KACHORI?NISHAI KISHENZI WABONGO TUMEZIDI KUOGOPA NGOZI NYEUPE NDO WEUPE WANATUDHARAU NA KUTUTREAT KAMA MBWA.UYO BANIANI ILIBIDI HATA NAFASI YA KUMI ASISHIKE.

  70. Cora Says:

    Kwa kweli tukimsakama huyo dada hatufiki kokote.. nionavyo ni kwamba let her be our face and I am sure this time tunashinda… na akishinda watu watanyamaza.. kwanini tupende hela zao wakati wanatoa vitu vyao tu kwa washindi (wahindi) vya kusupport hizo shughuli .. kama taifa ni moja na watu wote tuko sawa… hii ni ruksa kabisa.. ukipenda boga na ua lake pia… hiyo natoa support mia moja.. it is time we change.. judges hawakufanya makosa… she is beautiful. Tuko bega kwa bega.. ciao

  71. madawa Says:

    KWA KWELI WENZANGU WATANZANIA WENZETU DUNIANI WANAENDELEA KWA KASI MNO HAWANA MUDA HATA WA KUPEANA SALAMU MZIMA NI HAYYYYYYY KWA WA UK NA WAFARANSA NI SALYYYYYYY KWANI MUDA WOTE WANAUMALIZA KWA KUVUMBUA LAKINI UKICHEKI SISI NDIYO KWANZA TUKO KARNE YA 11 TUNALETA UJINGA NA UPUMBAVU WA UBAGUZI ETI OO MUHINDI MWARABU MPEMBA NAN MAJINA KIBAO BILA VINA ETI RICHA MUHINDI YES OF COURSE UKITAKA AWE MGUNYA AONGEA HADHARANI kamwene mwana gage ANA HAKI KUWA VILE KWANI ANAJIVUNIA NAWE KAKA AU DADA KAMA INAKUCHOMA KUCHUKUWA HUYO DADA YETU USHINDI NJOO WEWE NA VIPILIPILI VYAKO VYA KICHWA USHIRKI CORSE WEWE NI MWEUSI ET NI AIASILI YA TANZANIA NA WE KAKA NJOO NA PUA KAMA JIPU UCHUKUWE UMISS AU BIGG BOY KAMA UZALENDO UNASEMA HIVO.

    TANZANIA NI MCHANGANYIKO WA MAKABILA NA MCHANGANYIKO WA MADHEHEBU YA DINI WAISLAM WAKIRSTO NA RANGI ZAO WARABU WEUSI WAHINDI NK…ETI LEO UNAKUJA WEWE MKOSEFU WA ELIMU UNAPOROJA TUU KATIKA HII BLOG CORSE SISTER WAKO ALISHIRIKI KAPIGWA KIPANGA NDIO UNASEMA LAKINI ENGELIPATA HUYO BASI WATU WENGELIMPONDA TU.

    NANI KASEMA TANZANIA NI YENU PEKE YENU NO DADYYYYY TNZANIA NI YA WOTE.WACHA KUTIA KITUMBO JOTO DADA RICHA HATA AKASHINDWA KUTULETEA UMISS HOKO UCHINA KWA MIDOMO YENU MICHAFU SHENZ TAPE KUTOKA VICHOCHORONI HUKO .

    DADA RICHA MIMI NINAKUMAIND ILE KINOMA KWA UZURI WAKO NA TABASAMU KWANI ULISTAHIKI USHINDI UKIPATA HII MSG BASI KUMBUKA TUKO NAWE AND I HOPE YOU WILL DO BETTER DONT WARE FOR ALLS .MAFANIKIO MEMA.ISHALLAH

  72. mesa Says:

    naomba kuuliza nyie wahindi kwanini mtoto wa kike anatolewa bikira na baba mzazi na wa kiume anatolewa na mama mzazi nipe jibu halafu nitakuita wewe richa ni MTZ bila hivo usitudanganye wewe gabachori

  73. KANSAI JIN Says:

    Watoa mada bado wengi bado wanaelezea matatizo katika jamii yetu ya Wabongo… kuna mtoa mada mwingine amediriki hata kuelezea matusi humu ndani basi kama watu wameshindwa ustaarbu tunakuomba bwana Michuzi uufunge mjadala kwa kuendelea hivi hatuwezi kuwa na positive impacts which can alter our ways of thinking .We cant tolerate this anymore….
    Love ,peace and respect inaweza kuwa nguzo kubwa ktk kuongoza mjadala humu ndani .Tujaribu kutumia simply words which focus straight to the points tuepuke kutumia maneno yatakayomkwaza mtu….kuna msemo mkuki kwa nguruwe..kwa binadamu mchungu .
    Mzee wa Kansai ,OSAKA

  74. andejohn Says:

    oh oh hakyamungu to tell u thetruth mimi mwenyewe niposikia miss thing ni muhindi siku wa ok lakini rgt now sijali namwombea ushindi atleast aingie top 3 tafdhali

  75. KANSAI JIN Says:

    Ujumbe kwa Miss TZA 2007 , Ms Richa ..
    Tanzania yetu ina matatizo mengi na yote hayawezi kutatuliwa kwa pamoja ila kwa kuwa na mpangilio maalumu basi tunaweza kupunguza kwa kiasi fulani kama siyo kueliminate kabisa .
    Kwa upande wangu hili tatizo la ubaguzi wa rangi ..apartheid but not so strong as South Africa where pple were discriminated , humiliated and not given their rights ni vyema kulikemea
    kwa nguvu zoote kabla halijaota mizizi.
    Kipindi hiki ni vyema utilie mkazo mafunzo yako yanayokukabili then hili la discrimination likawa kama challenge towards your Miss World victory.I am sure you will surprise them ….
    Baada ya kurudi basi plz andaa program kuhusina na hili kama ni funds tutakusaidia if you will be serious on this , unaweza kuanda kipindi kwenye TVor radio stations 30 min. is enough for this kwa kuwaalika watoa mada/wadau mbali mbali kama advocates , politicians , sheikh , pastors even ministers , Miss TZA organizers ,pple or tanzanians with different races/ colour of skins i.e whites ,blacks,half casts,asians etc
    and they can discuss/debate abt this but our main agenda will be how to eliminate/dissolve
    discrimination in Tanzania .
    Keep it up Miss Richa we love you tupo bega kwa bega
    Mzee wa Kansai,Osaka

  76. mkuki Says:

    Hivi wewe cashmoneyholland kwanza GO BACK TO SCHOOL
    Wewe mwenyewe kama, unajua english mbona umeandika kwa kiswahili wewe mwenyewe hapo hunanywele za bandia
    Sio una zarau watu weusi. Huwezi kusema hoo kina Mwajuma wa TMK hawajui kimombo kwa taarifa yako wa Venezuala hawaongei kimombo mbona wanashinda MISS WORLD Sisi watanzania tuna proud na lugha yetu kama wewe ni mwindi nenda, kwa waindi wenzio hukale kachori sio tu unazarau weusi.Kama watanzania imewauma huyo MISSINDIA TZ wahache waumie kwani wanauchungu na watu wao (WHITE IS FASHION) unaweza hata kununua dukani ushasikia weusi wananunua rangi dukani? hao wazungu wenyewe wanapenda rangi yetu ndio maana wakati wa summer wanaenda kulala juani hili wapate rangi.sipendi dharau

  77. jennifer mhando Says:

    Ewe mrembo mimi niko pamoja nawe tangu mwanzo hadi mwisho ushinde au ushindwe. mbona wadada mnajichubua mfanane nao na mawigi kibao ya kila aina. kuweni wakweli. all the best RICHA

  78. Mgumu Says:

    Naona hapa asilimia kubwa ya hao wanamtaka Miss wao IndiaTz tunawatakia, kila la kheri kwenye mashindano.Najua asilimia ya watu ambao washamba wanababaikia sana rangi nyeupe ndio mtoto bomba,Sasa kwa taharifa siku hizi si waindi wazungu au walatino wanaongeza nywele za bandia tena wao ndio wa kwanza, pili wanapenda kwenda kwenye solarium (ni chumba cha joto au wanaingia ndani ya mashine hili wapate colour)na pia wanatia nywele relaxer.Kwahiyo msipenda kuwakandia mademu wa kibongo wanapenda kujichubua na
    wanapenda mawigi.

  79. dino Says:

    naona hapa Tanzania haina msomi hata mmoja kwani yeye ndio aliyeleta ubaguzi wa rangi au alifundisha jamii ya kihindi kuwa na ubaguzi,chuki na mengine.sisi kama watanzania tulitakiwa kumpa heri alete ushini ili nchi yetu ijulikane.kwani hata sisi baadhi yetu wenye asili ya kitanzania hatujui mila na destuli za kilugha sasa,kwani wengi wetu wote tumekulia mjini na tumekimbilia nchi za ughaibuni.kwanini tusibaki nyumbani na kutetea nchi yetu kama kweli twataka maendeleo.tumebakia kusema sie wakenya na kiswahili tunabadilisha kwanini tusiwe tunasema sie watanzania.kwani karne ngapi zimepita na viongozi wangapi wamekuwa madarakni kwani hawakuona wahindi wanaubaguzi wa rangi sasa naona mwataka leta mambo ya Idd amin.watu wote duniani wana ubaguzi.sasa kwani nini baadhi wataka kuoa au kuolewa watu weupe waishi nje sio Tanzania,sema kwa vile wao wana mila ya kutooa au kuolewa na kabila jingine si watz tu hao wao wenyewe pia wana makabila hawawezi fanya hivyo.so kinachotakiwa ni sisi wenyewe tutafute namna ya kuwaelimisha jinsi ya kuondoa ubaguzi huo sio kumtukana kwa kosa ambalo halijui.kwani hata sie wenyewe hatupendani tunajifanya midomo mirefu lakini unafiki tupu.we akija hapo mtanzania mwenzio akaomba msaada utavuta mdomo mpaka mungu anweza shuka au ukatoa neno baya kuliko kusema kama huo msaada huna.hivyo nawaomba watanzania tuwe na upeo wakutambua ni jinsi gani tunaweza kuondoa hilo tatizo na sio kashfa kwa mtu ambaye alifuata taratibu zote na sheria za kugombea umiss.

  80. Pope Pius Says:

    Kwa wanaomjua Masanja Mkandamizaji huwa ana kijisehemu kwenye maigizo yake kinaitwa “LAITI KAMA…”, Huwa anajaribu kuelezea Ndiyo yaliyo Siyo kwa wakati huo!!! Mi nasema LAITI KAMA KUNA WABAGUZI DUNIANI, WAAFRIKA NAO TUMO!! Tena wamwanzoni kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!! kwenye Rank ya wabaguzi

  81. Pope Pius Says:

    Ukitaka kujua sie hatupendania, kwa tuliokuwepo siku ile ya Miss Tz 2007, mara tu alipotangazwa mshindi wale wenzake walifurahia sana nilijiuliza lakini sikupata jibu la haraka hadi jamaa yangu aliponifungua macho akasema wale wamefurahia zawadi ya Gari imekwenda kwa Mhindi na sio Mtanzania maana angewaringia wenzie!!! ukitaka tafuta clip ile utaona. Maana yasemwa kulishakuwa na majigambo sana baina yao huko kambini kuhusu RAV4 New Model!!

    Pia utashangaa hizi kauli nyingi zinatoka kwa wenzetu hasa walioko nje ya nchi ambao kwa namna moja au nyingine wamesha onja machungu ya kubaguliwa iwe kwenye usafiri, shule, kazini, au kwenye starehe ama makazi. Wengi wetu wamezaa na asili tofauti (wadhungu) jamani na hawa waitwaje kwenye utaifa mliomo? wana haki gani?

    Hata hivyo Msijidanganye hata siku moja hata hawa Wahindi huwa wanabaguana hasa ikitokea wanatoka kwenye Jamii tofauti za Koo na dhehebu zao, kuna Sinashir, Bohora, Muhamadia,etc ila wao hupendana kati ya Dhehebu/Koo/au Jamii fulani, na kusaidiana sana baina yao, kama jinsi ambavyo jumuiya mbalimbali zimejitokeza kumpongeza Richa!!

    Kwangu naona sawa tu kwani ni majuzi tu Michuzi alitukumbusha picha ya Waziri wa Fedha wa Wakati huo tunapata Uhuru Amir Jamal au alikuwa Mmatumbi huyu?

    Wabbillah Tawfiq.

  82. TanzanianDream Says:

    Ebana watz inabidi tuamke Ngorongoro Crater is no longer in 8 wonders,sijui kama ilikuwepo before ila haipo tena sasa nyie ambao mnamsapoti mtu wenu bila kujua anaenda kuongea nini jaribuni kumshauri mapema(naanza kudoubt uwezo wake ambao wengi mmesema aliwazidi wenzake kwa uwezo)

    Mi sijui kama Richa ana akili kama mnavyodhani lkn nadoubt uwezo wake na elimu yake kwa ujumla….

  83. uburudani Says:

    jamani eeeeee.zawadi ya miss imetolewa na mdosi,anapewa mdosi,hivyo richa nenda kafanye udosini u miss na sio bongo land kwani ni ya wabongo halisi.

  84. MTU Says:

    JAMANI EEH! HUYU NI TANZANIA KABISA HAMUONI KUA ANA ALAMA YA NDUI………

  85. Salome Says:

    Richa mzuri anapendeza, mie sijali uhindi wake, ninachojali ni uzuri wake, kwani huko anakoenda kushindana haangaliwi kabila au rangi bali ni uzuri wake na taifa lake, nyie mnaokonda kwa ushindi wake basi mzidi kukonda kwa wivu wenu. Tuko na wewe Richa tena wengi tu, hawa mahasidi wenye donge wache wakonde tu.

  86. Rose Says:

    JAMANI WATANZANIA ACHENI ULIMBUKENI, NYIE MLITAWALIWA NA WAKOLONI, BABA YETU WA TAIFA KAPIGANA KIUME KUPATA UHURU. INA MAANA SISI WATANZANIA BADO HATUJIAMINI KABISA MPAKA TUMPE PONJOLO BENDERA AKAIPEPERUSHE KWA NIABA YA NCHI???? JIULIZENI WENYEWE, INDIA KUNA WATZ KIBAO, JAPANI, NA BAADHI YA NCHI KIBAO WATZ TUMEJAZANA, NI NCHI IPI MLIONA MTZ ANAPEWA BENDERA YA NCHI HIYO KWENDA KIUPEPERUSHA??? AMKENI ACHENI KULALA, MKIENDELEA KUSAPOTI HAYA YA MISS TZ WA MWAKA HUU KUWA ANASTAHILI NA HANA UBAGUZI WALLAHI MIAKA 20 IJAYO RAISI WA NCHI NA MAWAZIRI, NA WABUNGE WAKE WATAKUWA WAHINDI NA WACHINA MANAKE NDO WAMEJAA TZ. ENDELEENI NA ULIMBUKENI HUO HUO MLIO NAO MSIAMKE KABISAA, LALENI TU, WATOTO ZENU NA WAJUKUU ZENU BAADAE WATAIPATA FRESH. NINA UHAKIKA WENGI WANAOMSAPOTI HUYU MHINDI NA KAMATI YA MISS TZ NI VIJAKAZI WA WAHINDI WANAJUA WASIPOFANYA HIVI WATAKUWA HAWALI. TUKIJA KWENYE UPANDE WA WADHAMINI WA MASHINDANO HAYA NI WAHINDI TU, SO RUSHWA IMEJAA NA KUTAWALA MANAKE MHINDI HAJIAMINI HATA PUNJE YEYE NI KUHONGA TU. SIWAPENDI WAHINDI NA SITAKI HATA KUWAONA. WACHAFU NA WABAGUZI SANA. WEWE RICHA NDO KABISAAAAA NIKIKUONA NASIKIA KAMA MIMBA YANGU INATAKA KUTOKA. KICHEFUCHEFU WALLAHI UNANTIA WE BINTI. WAHINDI NI WASHENZI NILISHAFANYA NAO KAZI NILIKUWA NAWATIA VIBAO MPAKA NIKAFUKUZWA KAZI, LKN NILIWASHIKISHA ADABU NA NAFANYA KAZI NA WAARABU NA WAZUNGU, WATU WASTAARABU. SIO MAHINDI MAPONJOLO, MAGABACHOLI. I HATE THEM!!

  87. say Says:

    BC you r now known, stop using this gal to obtain visitors.
    RICHA I dont hate u, if I would I must have instituted a case because I am very sure your visit to BONGO CELEBRITY few days b4 MISS TZ ompetetion was illegal as per miss Tanzania rules

  88. roja Says:

    Mimi ni mbongo ambaye najivunia nchi yangu,pili nina furaha kupata nafasi ya kutuma maoni yangu ndani ya bc.kwanza ningeomba nimfahamishe ndugu JUMBE ambae ameweza kuwatukana hao wabongo wenzie kua hawana elimu na ni washamba kwa kupinga ushindi wa huyu dada wa kihindi.kwa kwekweli waswahili wa kale wana usemi unaosema tembea uone.namshukuru mungu mimi nimepata bahati ya kutembea na hadi hivi sasa nipo nje ya nchi yangu na nimeona na nazidi kuona ni jinsi gani uzalendo una nguvu kwa watu wenye nchi husika.Hivi kaambiwa na nani kua wananchi wote wa ulaya hufurahia pale timu zao za taifa zinapokuwa na wageni hususan weusi?hii si kweli ni watu wachache sana kama ni asilimia ya hao hua wanapenda tu pale inaposhinda lkn si kwa vingine.hivyo ndugu usipende kutukana wenzako kuwa ni washamba pengine hao wametoka nje na kuona nini uzalendo.
    huyu binti mimi siku nilipomwona tu ktk blog ya michuzi nilisikitika kwani hana hadhi ya kuiwakilisha bongo kwanza kwa ile asili aliyonayo hata akijitetea mama yake ni mpemba na baba yake ni mmorogoro lkn utakuta hao wazazi wake pia si wabongo halisi.
    mimi namtakia asishinde yaani hata 100 bora asiingie.

  89. Nana Says:

    Roja nakukubalia kabisa huo usemi wako watu wengine wanajua Ulaya ni mbinguni, Hakuna ubaguzi heee tembea huone utakumbuka tu nyumbani.Huyo miss Tz kama angeshiliki ulaya asingepata kitu yaaaani00000000000000 labda hawe ana damu ya kizungu au mzazi wake mmoja yuko point5 labda wangemfikilia.Sina mengi

  90. sandy Says:

    kiukweli huyu binti si wakumlaumu.kwa wale wanao ona Tanzania ni nchi yenye ubaguzi nadhani kila mtu ana haki ya kufikiri vile anavyo paswa fikiri.lakini huyu binti si wakumlaumu kwa yote yanayoendelea nchini kwetu,kwani wapo wachache kati ya kundi la wahindi ambao wanaroho ya ukarimu na si wabaguzi,kwa bahati mbaya hawa ni wale ambao sauti zao si zile za kusikika na hivyo hawaonekani wala hawana nguvu ya kuonyesha kama nchi yetu ni nchi ambayo ina watu wa rangi tofauti na tunapendana.ni vyema hili liwe fundisho kwa wahindi nchini kwani wameona jinsi wenye asili yakiafrika wanavyo kandamiza,japo hatuna nguvu kwa sasa na ninarudia tena kwa sasa,kuwa fichua wale wenye kutukandamiza weusi nchini kwetu itafika pindi ambapo tutaweza kwa kusaidiana na kizazi kipya ambacho kitakua madarakani miaka ya mbele kunyoosha njia ya kwamba ni nchi yetu wote na yule atakae tumia mgongo wa mwingine atashughulikiwa ipasavyo.other wise nina mpa full support miss Tanzania wetu na inshallah kila mtu kwa dini yake kwa wale wanao mpa support yote tumuombee atuletee sifa nzuri nchi yetu kwani hapo ndipo tutaona ushindi wa nchi yetu na si wakihindi wala mweusi all the best.

  91. nefertiti Says:

    SALAMU HIZI ZA HUYO ANEJIITA KANSAI JIN….
    WHATEVER..
    UNASIKITISHA SANA…NINASHAKA WEWE NI MHINDI AU HOUSEBOY WA WAHINDI…. YOU MAKE NO VALID REASON FOR WHY AFRICA SHOULD CEASE TO BE BLACK WHEN THERE ARE IMAGE ISSUES AT STAKE… I DONT SEE INDIA BEING REPRESENTED BY AN UNTOUCHABLE (HAWA NI WALE WAHINDI WEUSI WA DARAJA LA CHINI KABISA INDIA)

    UNTOUCHABLES HAVE A SIMILAR SKIN TONE TO YOURS OR AFICKANS I SHOULD SAY….. WHAT MAKES YOU THINK AN INDIAN BORN IN TZ IS ANY DIFFERENT OR WILL THINK OF YOU ANY BETTER..???

    SASA HAWA UNTOUCHABLES WAKO INDIA AND THEY DO NOT IN ANY WAY COME CLOSE TO BEING RECOGNISED BY THE REST OF INDIA (GOA OR OTHERWISE)

    HUO NDIO UBAGUZI WA WAHINDI ULIVYO…KWA HIYO WEWE MSWAHILI MWEUSI WA MANERUMANGO UKIJIONA KUNA USAWA UTAUPATA TOKA INDIA…NAOMBA UPELEKE HILO JIPU LAKO INDIA KASHINDANE KATIKA FANI YOYOTE ILE….KAMA UTAPEWA UPENYO…… NA KIYAMA KISIMAME.

    NARUDIA TENA…. RICHA SI MTANZANIA NA HANA HAKI YA KUTUWAKILISHA WAAFRIKA TOKA TANZANIA…

    ACHENI UPUMBAFU…NA MJADALA UFUNGENI….. RICHA ATALETA MAPINDUZI MAKUBWA …HATA KWA AMANI FEKI TUNAYOJIDAI KUWA TUNAYO WATZ. RICHA ACHIA NGAZI….

  92. mabibo Says:

    huh?!

  93. Ed (USA) Says:

    Miaka ya 90 nilikuwa nasikiliza mahojiano ya Nyerere (baba wa taifa) nanukuu sehemu ya majibu yake alisema, “…hata wajinga wanazaliwa….” Nyerere hakuwa 100% perfect hata mwenyewe anakiri kwenye jumbe zake. Tunakosea kabisa kuizungumzia Tanzania bila kumhusisha Nyerere. Pamoja na udhaifu aliokuwa nao kama mwanadamu, sikubaliani na hoja ya mdau mmoja kwenye haya malumbano kuwa, Nyerere alikosea kukabidhi uchumi kwa wahindi ndio maana nchi yetu imekuwa maskini- SIO KWELI. Tujiulize nchi hii ilikuwa na wasomi wangapi Nyerere alipochukua nchi na wasomi walikuwa katinga mazingira gani? Nawashauri wale wote ambao hawajasikia hotuba za Nyerere akifundisha watanzania kujiepusha na ubaguzi, watafute wasikilize. Huyu jamaa alijaliwa kipaji cha kufundisha na ni wenye ajenda binafsi ndio wasioweza kuelewa anachosema.

    Kwa maoni yangu ninapopitia malumbano humu ndani, nimegundua jambo mojawapo kuwa, kuna watoa mada wanakosea kuhusisha mtu kutokana na mabaya yanayofanywa na watu anakotokea. Hivi sisi watanzania wengine katika makabila yetu tunakotoka, hakuna mabaya ambayo ni kero kwa wengine? Inakuwaje tunawaona wahindi ndio wanajitenga kwa mambo yao wakati wachaga, wahaya na wengineo hufanya hivyo pia?. Sijui nini kinafanya mwanamke wa kihindi asiolewe na mtanzania lakini niliwahi kusikia wenzetu mwanamke ndio anaoa mwanaume. Hata kama itakuwa sio sababu ya kutosheleza lakini hatuwezi kuchukua kigezo hicho kumfurumishia lawama huyu binti kwa makosa ambayo sio yake.

    Ubaguzi ni dhambi moja kati ya dhambi nyingi zilizomo ndani ya moyo wa mwanadamu bila kujalia ni mmakonde au mhindi n.k.

  94. JITUPARATUPU Says:

    Msijeshangaa akawa MISS WORLD!…Hatatajwa yeye bali ni TANZANIA. Tufanye subira!

  95. Nasser Says:

    Haya makelele yote juu ya Utanzania wa huyu dada hayasaidii. Kila nchi ina watu wachache wenye tabia za kibaguzi, hata UK, Germany, USA na China. Haina maana ya kuiga tabia mbaya hata kama baadhi ya wahindi ni wabaguzi. Mimi pia mama yangu ni mwarabu lakini hata sijawahi kufika huko arabuni, na nilikuwa nataniwa sana shuleni na baadhi ya watoto kama mwarabu koko. Sasa ninaishi Ujerumani miaka kadhaa lakini ni proud sana kuwa Mtz, hata passport ya kijerumani siitaki, ingawa naweza kuipata any time nikiitaka.

    Kwanza ubaguzi ni chuki na wivu wa watu wachache ambao hawana perspective ya maisha. Hata hapa Ujerumani, watu wanaojihusisha na hii tabia ya kupiga foreigners ni vijana ambao hawana ajira na wanafikiria tumekuja kuchukua kazi zao. Mtikila pia alirudisha hii tabia na kushawishi vijana wa mtaani na wasio na mbele wala nyuma kuchukia wageni.Tuache kubaguana, lasivyo tutarudi katika zama za ujahili za chuki baina ya makabila pia.

    Kwakifupi tusipoteze muda maana ubaguzi utakuwepo daima, kama vile kuwepo uzuri na ubaya, na pepo na moto halafu mwema kuenda peponi na mbaya (mfano mbaguzi) huenda motoni kwa anaeamini hayo.

    Mafanikio mema wote

  96. Sultan Says:

    Tusio kuwa na kazi tuendelee kupoteza muda wetu na kuitangaza TZ kimakosa pamoja na raia zake wasio na rangi. je mtazamo wa serekali uko wapi kwa haya nani raia na nani sio raia?

  97. prisika Says:

    niko marekani….jamani mlio bongo mnaoona sehemu nyingine kama mbinguni….mnachemsha!
    ubaguzi umejaza koteeee…nahisi Marekani inaoongoza!
    kuna watu hapo juu wamesema mtanzania nenda India kashiriki chochote cha kihindi uone kama utashinda ni kweli hushindi ng’ooo!
    kwa huyo anayepaka watu wengine kuwa hawazungumzi kingeleza……kiswahili ni lugha ya taifa ya tanzania kama wewe ulipata nafasi ya kujifunza kingereza vizuri…kwani aliyekupa wewe ndo aliowanyima wengine…..Marekani mbona hawaongei Kiswahili sio wanajua wao tajiri hivyo lazima tujifunze kingeleza kuwsiliana nao…….umasikini ndio unatufanya tuhahe kutaka kuongea kingereza……..so cut that sh**t….
    Miss Tanzania bwana kwani imekuaje hadi kashinda kwa kweli hapo ni Lundenga na rushwa zake!
    mwanzo nliwaza kutakuwa hakuna tofauti kati ya miss India na miss Tanzania…..lakini nikaona hapana kwasababu huyu atatangazwa kama miss Tanzania na mhindi mwingine atatangazwa kama miss India ila…………Watazamaji watajua waTanzania wamefanana na Wahindi kumbe hapana ni kwamba tuuu imetokea Mhindi……….aliyezaliwa Tanzania ndio kawakilisha Tanzania…….haaaaaaaaa inachanganya……
    kuna mtu kasema hapo juuu akishinda itatangatazwa Tanzania……I think that’s all we need….even though Tanzania was represented by Indian!
    by the way watu weusi tunakuwa wabaguzi kwasababu ya watu weupe….namaanisha Wahindi,wazungu, waarabu wanavyotu-treat………wanalianzisha tunaliendeleza…….hatulianzishagi!

  98. YOUTH VIJANA Says:

    Ingawa nchi nyingi duniani zimekuwa na ubaguzi wa hali ya juu wa kuangalia rangi au udini,si vizuri kuona pia Baadhi ya watanzania tunawabaguwa wanabaguwana kwa rangi,Tuwapo kwenye michezo, mashindano hata kwenye elimu pia.Huyu ni miss Tannzania na siyo miss wa nchi nyingine yeyote.Hata kule china watamtambuwa kwa tabia yake ya kiutanzania na siyo uamerika….lugha,mwonekano na hata ufikiriaji ni wakitanzania.(yaani uasili wake wa kitanzania)
    Wapo wabaguzi ambao huwabaguwa watu kwenye nchi zao kama vile nchi za ulaya na kwingineko(razist.wanazi).
    Huy dada angekutana na watu kama hao,ndiyo wangembaguwa kwa maneno ya kashfa kwa sababu ni mweusi.
    Hakuna mtanzania ambaye atazuiliwa haki yake ya kufanya jambo lolote ambalo ni jema .Huyu dada ana haki ya kushiriki kuwa miss kama wanawake wote wa kitanania ambao wana vigezo kama vyake.
    KUWA MBAGUZI NI UJINGA TENA WA HALI YA JUU !!!
    DUNIA HAINA MIPAKA NI WATU NDIYO WAMEJENGA MIPAKA.UBAGUZI NI UOGA WA HALI YA JUU…

  99. Amy Says:

    I AM ENCOURAGING ALL INDIANS AND LIKES TO PARTICIPATE

    IN THE COMPETITION AND I HOPE THE NEXT 5 YEARS OF

    MISS TANZANIAN COMPETITION WINNERS TURN OUT TO BE

    INDIANS OR ELSE…. MAY BE THIS WILL OPEN UP OUR MINDS A

    BIT…. VERY DISAPPOINTING!!

  100. tokyo Says:

    mimi nimesoma maoni ya wadau wengi na nimegundua
    swala moja ambolo wengi wanaompinga miss tz.

    ni kwanini mshindi amekuwa na mimizi ya kutoka india,
    na si kwanini mtanzania na si mwenye asili ya taifa lingine.

    hapa naweza kusema kuwa baadhi ya makundi haya mawili ya
    (wahindi na watanzania weusi) wana matatizo makubwa ya ubaguzi.
    hapa napenda kupinga kuwa watanzania hawana ubaguzi wa rangi ila wana ubaguzi na wahindi.
    kwani tuna ushahidi wa kutosha kuona watanzania wenye kuchangaya na mataifa mengine wakishangiliwa kwa nguvu zote na watanzania wote,kwamfano Mwisho mwampamba
    ambaye aliiwakilisha tanzania katika big brother Africa.

    Pia waarabu ambao wanashika nafasi selikalini.Hii yote inaonyesha watanzania si wabaguzi ila wabaguzi wa Wahindi

    Swali hapa ni kwanini wahindi?
    Nahakika kama nafasi ile ingeshikwa na mtu mwingine mwenye asili yakutoka taifa jingine kama Mwisho mwampamba basi tusingekuwa na mjadala mrefu namna hii

  101. happy Says:

    Binafs sijamfagilia, kwanda mbaya, hana shepu nzuri, yupo yupo tu mdos wa watu.

  102. star Says:

    Tokyo, you are right mgogolo hapa ni wahindi na sio rangi …wahindi wanyanyasaji sana…mimi nilishaenda Indian, Chennai nilishangaa sana kuona wahindi very friendly then ndio nikagundua kumbe wahindi wa Bongo wana tabia mbaya mno..

    sisi wa wazawa tulikosea kuwakaribisha ndio matokeo yake hayo wanatunyanyasa sisi wenyewe….

  103. Mbinu Says:

    jamani mbona hamjaelewa Tanzania wahindi ndio wanabagua wazawa na sio vinginevyo, maana naona hapo juu watu wengi wana sympathie na huyo miss muhindi, kumbe wangejua yeye ndio anabagua wazawa na sio sisi tunambagua.. maana wahindi wengi wanawaona watanzania kama sio watu vile…na kwa rushwa ndio wenyewe…

    Prisika hata sisi ulaya tumekaa sana…na tunajua kwamba ubaguzi upo Europe na Marekani… hao usiojua hilo hawajawa kayanga Europe wala Marekani…

  104. dula madingo Says:

    huyo kwa akili nahisi sio mtanzania halisi kwani mtazania halisi

    rangi yake haiwi hivo. huyo asili yake ni asia

    kwani sie waafrika tukenda ulaya tukizaa watoto wetu watakua ni wazungu?

  105. ima Says:

    umembagua mpaka story imejitokeza CNN INSIDE AFRICA last week..shes a lucky girl…


Leave a reply to young girl Cancel reply