BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

UNAMKUMBUKA RENEE? August, 11, 2008

Filed under: Gospel Music,Muziki — bongocelebrity @ 2:56 PM

Bila shaka unamkumbuka mwanamuziki au mwimbaji Renee Lamira(pichani).Aliwahi kutamba vilivyo na albamu yake iliyoitwa Ngoma ya Kwetu.Lakini je unafahamu kwamba Renee siku hizi ameachana na nyimbo zinazoitwa za “kidunia” na badala yake anafanya nyimbo za injili?

 

28 Responses to “UNAMKUMBUKA RENEE?”

  1. Bariki Says:

    Renee
    Hongera kwa kutambua kuwa kumsifu Mungu kunalipa kuliko kuwaburudisha wanadamu.

  2. Binti-mzuri Says:

    Toto la kihaya,shepu shepu..ndugu yake matty huyu. Hongera kwa kumrudia Mwenyezi Mungu,njia ni 1 na sote tutairudia hio hio.nyimbo zake hata ivyo hazikua mbaya,kama ule wa ngoma inogile,its just purely innocent and sensational.hakuimba matusi,sema labda mavazi.keshatoa gospel sasa,2zisikilize? Big up mamaa rwelamira

  3. BLACKMANNEN Says:

    Katika safari ndefu ya maisha, binadamu anakutana na mambo mengi. Kutokana na mitihani migumu ya kimaisha ndipo mtu huamua kubadili mwelekeo wa maisha kutokana na sababu mbalimbali ukiwamo pia, wito unaoupata kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kama Dada Renee Lamira alivyoamua kubadili mwelekeo wake katika fani yake hiyo. Maisha ni mafupi kama ambavyo mmesikia kupitia vyombo vya habari kuwa, gwiji la mziki “Isaac Hayes” amefariki dunia asubuhi ya leo akiwa na umri wa miaka 65 tu.

    Blackmannen

  4. MapigoSaba Says:

    sio wa kwanza!

  5. imzzotz Says:

    Njia tuendayo ni nyembamba sana, na wajanja wanafanya kama renee. We fikiria watu kama wakina remmy ongala, Mc hammer, Makasi na Chidumule ni watu ambao hukuwahi kufikiria kama watafanya hivyo na kali zaidi ni kwamba baada ya kufanya hivyo mambo yao yanawanyookea, kwa mungu ni kuzuri jamani….!

  6. ma'reen Says:

    Umechagua fungu lililo jeme dada, God bless you!

  7. Matty Says:

    Hongera ndugu yangu kwa kuchagua fungu jema na Mungu akubariki…ngoma inogile ngoma imekoleaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.
    Binti Mzuri huyu ndugu yangu kwakweli ni mrembo na anajua kuimba ila hapo kwenye mavazi atakuwa kashabadili kimtindo maana yesu hapendi kuona vitovu vikiwa tupu!

  8. Edwin Ndaki Says:

    Mimi ndio njia na kweli na uzima….

    Haya dada hongera kwa kuamua kufuata hiyo njia.Ila ni imani yangu umeenda kwa minajilibwana na sio kwa mtazamo wa kutafuta soko zuri maana nilishaona wasanii wanasema ‘gospo’ inalipa kuliko hizi bongofleva.

    Kila la kheri Renee kwa lengo lako jema.

    Tutafika tu

  9. Pearl Says:

    Maisha ya hapa duniani ni mafupi sana,heri yule agunduaye hayo na kurekebisha njia zake mapema,sio lazma upitie shida ndo uamue kuokoka,hata bila kupitia shida you can still change your ways and be saved.Wokovu upo jamani and Jesus is coming soon,so i understand Renee’s decision and what i can say is hongera.

    Inawezekana kweli sio wa kwanza ila hata biblia imeandika “Mbinguni hushangilia mwenye dhambi mmoja akitubu”

  10. sikujua doto Says:

    Wanakijiwe cha BC wajameni mnaweza kutupunguzia hayo mahubiri ya yesu ni njia, na mkayabakizia rohoni mwenu kwani tunasikia kuwa yesu anaweza kukuona hadi ubongoni na rohoni unachofikiria. Kwa hiyo atajua kuwa unampenda hata bila kututangazia hapa. Sio lazima mtwambie jinsi mlivyokuwa watumwa wa yesu. wengine ni watumwa wa miungu wengine na hatukai kuwachosha na imani zetu!!!! Sote tuna imani. Bongoflava au gospel wote wanaburudisha na papo hapo kutafuta maisha na wote wanastahili pongezi. Nintoa OMBI!!!!

  11. trii Says:

    duuu humu BC kuna wahubiri wengi hivi?

  12. Gervas Says:

    Wee sikujua doto….hebu punguza munkari na imani za watu, hapo tayari umeshatukana, tutakutangazia dau shingo yako kama kule kwa wenzetu!! we jidai apa sasa. Kwa kifupi sielewi maelezo yako yana uhusiano gani na ujumbe uliowekwa na BC hapo juu au umekurupuka na ajenda yako mpya. Renee ni Celebrity, na hii blog ni ya ma-celebrity sasa kuna cha ajabu gani kumuelezea kuhusu maisha ya celebrity huyu?

  13. bupe mwakatobe Says:

    mi binafsi nampongeza sana dada huyu kwa kumtambua YESU maana yeye ndio njia kweli na uzima.so dada keep it up m2kuze na msifu yesu daima ya kidunia ss uyaache pia mavazi jitaidi kuchange coz c mazuri kwa jukwaa la Yesu.ongera sn ni uamuzi mzuri kuliko wowote ulioufanya tangu umekua.GOD BLESS U.

  14. Matty Says:

    Sikujua Doto Kweli hukujua unachoandika! umeandika bila kufikiri mara mbili sijui unamaanisha nini unaposema tupunguze mahubiri ya yesu?? wewe kama unaabudu mawe na wewe kamua kimpango wako na mawe yako, huna haja ya kukashifu kile wenzakop wanchoona bora na hata mimi siwezi kukashifu wewe unachoona bora, we are different in worshiping so wats a problem if we love jesus??

  15. binti-mzuri Says:

    jamani… udini hautaishaga kamwe! muogopeni MUNGU nyi wanadamu…theres only one GOD. we sikujua doto,uwe muislamu,uwe mkristo..wote tunamsalia Muumba mmoja,maybe in different ways,but i tell you this my friend..theres only one GOD..u shall regret,for not believing. heri walioambiwa na kuamini

  16. linda Says:

    Ama kweli renee Mungu akubariki maana umechagua fungu lililo jema, karibu katika familia ya Yesu Kristo.
    Mengi yanasemwa lakini mtu akatae akubali Yesu Kristo ni njia ya kweli na uzima mtu haji kwa baba (Mungu) bila kupitia njia yangu (Yesu)
    Hongera sana angalia shetani asikurudishe misri (dhambini) dada maana ana mbinu nyingi huyo.

  17. linda Says:

    Hivyo ndivyo lisemalo Neno la Mungu (Biblia)

  18. Pearl Says:

    sikujua doto kama unaona hapa watu wanaongelea mambo ya Yesu na wewe hupendi ni rahisi sana usisome fuata shughuli zako nyingine lakini hatuwezi kunyamaza tusimseme Yesu wetu eti kwavile wewe hupendi,kama wewe uaona aibu na huyo mungu wako “ASIYEJULIKANA” hiyo ni kivyako.

  19. imzzotz Says:

    mi cna la kusema juu ya huyu sikujua doto, maana ni kweli hajui.
    majina mengine huwa yanariflekti kilichopo kichwani mwao. lol

  20. hapyy Says:

    hongera dada,dunia ni mapito
    mungu akubariki

  21. any Says:

    Huyu dada kafanana na Amanda kwa mbali! au ni style za nywele.

  22. linda Says:

    Pole sana sikujua doto, maana hujui ulitendalo.
    Kama Kristo Yesu asingefungua njia ya kuhubiri injili mimi nisingeokolewa ningeendelea kuonewa na shetani lakini alihubiri na nzuri zaidi aliwaachia kina Paulo, Petro na hata sasa injili inahubiriwa hivyo ni hiari yako kusikia au kutosikia.
    Naona wewe huyawazi yaliyo ya Mungu bali ya wanadamu
    Mathayo Mt 16:23
    Pole ipo siku utaelewa.

  23. linda Says:

    Yes Pearl,
    Ubarikiwe!

  24. Matty Says:

    Any,Amanda yupi tena?? wa kaole au??

  25. any Says:

    Matty bana, wa Face of Africa. hahahah, Matty bana,
    wanafanana sura tu kwa mbali na sio mshepu, huko Kaole kuna Amanda pia?

  26. Matty Says:

    khaa jamani mimi huyo wa face of africa simjui shosti namjua amanda wa kaole muigizaji a,k.a bongom cerebrity!

  27. any Says:

    Aah Matty yule aliekuwa sponsored na Maria Sarungi ni wa kwenye nini? ni face of Africa, au Universe, hao ao, mi sijui bana, chagua kati ya hizo. hahaha.

  28. Innocent Says:

    Thats good Renee,
    Keep on servin tha Almighty God thru singin,
    It pays than to sing worldly music. U have a nice vocal.
    Thanks. Rgds, Innocent.


Leave a reply to linda Cancel reply