BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

MIGIRO NA MJUMBE MPYA WA AMANI February, 2, 2008

Filed under: African Pride,Mahusiano/Jamii,Sinema,Watanzania Kimataifa — bongocelebrity @ 12:05 AM

 

Pichani ni Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Dr.Rose Asha Migiro(kulia),akiwa na George Clooney(46),mwigiza filamu na mwanaharakati maarufu kutoka Marekani.

George Clooney aliteuliwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Ban Ki-Moon hivi karibuni kuwa mjumbe au balozi mpya wa tisa wa amani wa Umoja wa Mataifa (U.N. Messenger of Peace ). Dr.Migiro alimkabidhi George Clooney Cheti Cha Mjumbe wa Amani.

Mwaka huu Clooney amechaguliwa kuwania tuzo maarufu ya Oscar kwa uigizaji wake katika filamu iitwayo Michael Clayton.

 

3 Responses to “MIGIRO NA MJUMBE MPYA WA AMANI”

  1. Upendo Furaha Amani Says:

    Hongera sana Dr. Asha-Rose Migiro kwa kutuwakilisha vyema Watanzania katika nyanja za kimataifa. Tulikuwa nyuma sana, lakini kila jambo na wakati wake chini ya jua na sasa Wabongo tunaanza kujulikana kimataifa na siku moja Mtanzania atakuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
    Tuipende Tanzania Nchi Tuliozaliwa.

  2. Matty Says:

    Nampongeza sana huyu mazaaaa maana yupo katika system nyeti sana na huyo Kanumba naye hapo ajitahidi kucheza filam fresh na kuleta amani iliyopotea miongoni mwa waafrica hasa hawa watani wetu wa jadi maana hawataki kusikia la mkuu Anani!!!!!!

  3. Dinah Says:

    Hahahaha Matty eti Kanumba!

    Huyu mama ananifurahisha sana when it comes to muonekano, anapendeza sana yaani ni kawaida (hajiandai sana kama 1st lady) lakini anatoka bomba.

    Kila la kheri ktk ujunzi wa Dunia.


Leave a reply to Upendo Furaha Amani Cancel reply