BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

WHEN CELEBRITIES MEET…. August, 30, 2007

Filed under: Sinema — bongocelebrity @ 10:50 PM

 

Kila mtu huwa na furaha ya kukutana na celebrity ampendaye. Wakutanapo celebrities,kama inavyoonekana pichani juu, kinachotawala ni vicheko! Pichani ni Raisi mstaafu wa Tanzania Mheshimiwa Benjamin William Mkapa na mshindi wa tuzo maarufu ya Oscar, Forest Whitaker. Picha hii walipigwa tarehe 17 Februari 2007 jijini Kampala, Uganda wakati wa maonyesho ya mwanzo ya sinema ya The Last King of Scotland ambayo ndiyo ilimfanya Forest Whitaker ashinde tuzo ya Oscar.

 

DJ SEYDOU August, 29, 2007

Filed under: DJs,Muziki — bongocelebrity @ 3:56 PM

 

Kunako miaka ya 80 na mwanzoni mwa miaka ya 90, majina ya Ma-DJ yalikuwa makubwa kama ilivyo kwa wanamuziki wa kizazi kipya na cha zamani hivi sasa. Mojawapo ya majina hayo ni DJ Seydou(pichani). Yeye na DJ mwenzake aliyekuwa anajulikana kama DJ Yaphet Kotto walitamba sana na disco lao la RSVP Discotheque pale Mbowe (siku hizi Club Billicanas). Enzi hizo vijana walikuwa waende wanakokwenda usiku unakuwa haujakamilika kama hawatofika Mbowe kupata ladha kutoka kwa DJ Seydou na mwenzake.Jina lake halisi ni Saidi Mkandara.

Tofauti na Ma-DJ wenzake wa enzi hizo, yeye alikuwa sio muongeaji sana. Badala yake yeye alisifika sana kwa uwezo wake wa kupangilia miziki. Akianza vitu vyake alikuwa hakai mtu kitini mwanzo hadi mwisho. Uwezo wake wa kusoma ukumbi na kujua aweke muziki gani ulikuwa unawastaajabisha wengi. (more…)

 

NANI? August, 27, 2007

Filed under: Uncategorized — bongocelebrity @ 11:09 PM

Ni kwa kiasi gani unaweza kuwatambua celebrities wa Tanzania kwa kutumia picha za vivuli kama hizi? Huyu pichani ni nani?

 

 

MZEE FRANK HUMPLINK HATUNAYE TENA!

Filed under: Breaking News,Muziki — bongocelebrity @ 12:37 AM

Wakati wa harakati za kugombea uhuru wa Tanganyika kati ya mwaka 1954 mpaka 1961, jina moja lilitamba sana katika fani ya muziki. Jina hilo ni la Frank Humplink. Humplink alikuwa mwimbaji na mpiga gitaa maarufu sana wakati ule. Alikuwa akipiga muziki wake akishirikiana na dada zake wawili Maria Regina na Tecla Humplink.

Habari za kusikitisha ni kwamba Frank Humplink hatunaye tena. Mzee Humplink amefariki dunia jana tarehe 25 August 2007 huko nyumbani kwake Lushoto,mkoani Tanga. Alizaliwa tarehe 3 Aprili mwaka 1927. Amefariki akiwa na umri wa miaka 80.

Marehemu atakumbukwa sana kwa wimbo wake uliokuwa na mashairi yafuatayo, ‘Uganda nayo iende, Tanganyika ikichangamka, Kenya na Nyasa zitaumana’. Wimbo huo ambao ulikuwa ukiwasisimua sana wananchi, ulikuwa umesheheni ujumbe mkali wa kisiasa jambo ambalo lilikifanya chama cha TANU kuufanya kama vile wimbo wake rasmi kwani ulikuwa ukipigwa katika mikutano yake yote. Mikutano ya TANU ya siku za mwanzo ilikuwa ikifanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja mbele ya Princess Hotel. Sahani ya santuri ilikuwa ikipigwa katika gramafoni kupitia kipaaza sauti.

Pamoja na kutamba sana kwa wimbo huo haikupita muda serikali ya kikoloni ikaelewa ujumbe mzito uliokuwemo katika wimbo huo ambao kimsingi ulikuwa unasema Tanganyika itakapoamka, kutakuwa vilevile na mapambano nchini Uganda, Kenya na Nyasaland. (more…)

 

“MPAKANJIA SASA HOI”-Tanzania Daima August, 25, 2007

Filed under: Developing News,Mfanyabiashara — bongocelebrity @ 6:59 PM

Kwa mujibu wa gazeti la kila siku la Tanzania Daima, aliyewahi kuwa mume wa kuwa mume wa Mbunge wa Viti Maalumu, marehemu Amina Chifupa (UVCCM), Mohammed ‘Meddy’ Mpakanjia, ambaye habari zilizokwisha thibitishwa ni kwamba amelazwa katika Hospitali ya Jeshi ya Lugalo, Dar es Salaam, hali yake ni mbaya na sasa analishwa kwa kutumia mirija.

Habari zaidi za habari hii yenye kusikitisha unaweza kuipata kwa kubonyeza hapa.BongoCelebrity inaendelea kujitahidi kupata habari zaidi juu ya hali halisi ya Mpakanjia. Pindi zitakapopatikana tutawafahamisha.

 

MISS TANZANIA 2007 August, 23, 2007

Filed under: Miss Tanzania,Urembo — bongocelebrity @ 10:52 PM

Mashindano ya kumtafuta mrembo wa Tanzania maarufu kama Miss Tanzania kwa mwaka huu wa 2007 yanatarajiwa kufanyika jijini Dar-es-salaam tarehe Mosi mwezi wa Septemba katika viwanja vya Leaders Club-Kinondoni. Kwa maana hiyo tofauti na miaka ya nyuma au ilivyozoeleka, mwaka huu hayatafanyikia katika ukumbi wa Diamond Jubileee.

Pichani washiriki wa shindano la mwaka huu,wakiwa wamepozi na gari ambalo mshindi wa mwaka huu atazawadiwa pamoja na zawadi zinginezo.Mdhamini mkuu wa mashindano ya mwaka huu ni kampuni ya simu za viganjani Vodacom.

Mmoja ya washiriki wa mashindano ya mwaka huu ni Richa Adhia kutoka Kinondoni jijini Dar-es-salaam. Kutokana na yeye kuwa ni mtanzania mwenye asili ya bara la Asia (nchini India), tulipofanya naye mahojiano takribani mwezi mzima uliopita ilionekana wazi kwamba watu wengi watakuwa wanasubiri matokeo ya mashindano haya mwaka huu sio tu kuona kama Richa Adhia anaweza kuibuka mshindi au mmojawapo wa washindi bali pia kutokana na msisimko wa mashindano ya mwaka huu tangia yalipoanza kwenye ngazi ya vitongoji. Je nani ataibuka mshindi kwa mwaka huu wa 2007? Jibu tutalipata Septemba Mosi.

Kama ulipitwa na mahojiano yetu na Miss Kinondoni na maoni ya waliochangia unaweza kuyapata kwa kubonyeza hapa.

 

MBARAKA MWARUKA MWINSHEHE! August, 21, 2007

Filed under: Muziki — bongocelebrity @ 11:16 PM

Iwe ulizaliwa enzi za uhai wake au baada ya kifo chake, jambo moja ambalo wote tunafanana ni kwamba ukisikia muziki wake sio ajabu utatikisa kichwa, kutabasamu, kucheza au kurukaruka. Ukishaguswa na muziki huo sio ajabu ukajiuliza swali gumu; kwanini mungu akamchukua Mbaraka Mwaruka Mwinshehe baada ya ile ajali ya gari nchini Kenya tarehe 13 Januari mwaka 1979? Angelikuwa hai nani asingependa kusoma mahojiano yake? Inasemekana Mbaraka Mwinshehe alikufa kutokana na kuvuja damu nyingi na asipatikane wa kumchangia damu ili kuokoa maisha yake. Alifia hospitalini Mombasa.

 

Hayati Mbaraka Mwinshehe akicharaza gitaa na kuimba!

Uwezo wake wa kutunga nyimbo, kupanga muziki na kudonoa gitaa hauna mfano wake mpaka sasa. Ukimsikiliza leo unaweza dhani kapiga gitaa hilo juzi kumbe ni miaka chungu mbovu iliyopita. Kizuri zaidi ni kwamba upigaji wa gitaa hakufundishwa na mtu bali yeye mwenyewe. Akiwa bado kijana mdogo kabisa alicheza muziki uliokuwa unajulikana kwa jina la “kwela”(asili yake Afrika Kusini) na bendi iliyojulikana kama Cuban Branch Jazz. (more…)

 

TAFAKURI YA KINA NA NDESANJO MACHA. August, 18, 2007

Filed under: Blogging,Blogs — bongocelebrity @ 2:54 PM

Tangu kuanzishwa kwa blog hii imetokea mara chache sana tukakosa maneno ya kumtambulisha celebrity yeyote ambaye tumeshawahi kufanya naye mahojiano. Leo tunaelekea kuwa na wakati mgumu kidogo. Ugumu unatokana na mtu mwenyewe, mambo ambayo ameshayafanya na anaendelea kuyafanya hususani kwa upande wa blogs za Tanzania au ki-tanzania!Ngoja tujaribu.

Issa Muhidini Michuzi anamuita “mfalme wa blogs za Tanzania”. Anapomuita mfalme anakuwa hamaanishi tu kwamba yeye ndiye aliyemuingiza au kumtambulisha katika ulimwengu wa blogs walipokutana nchini Finland (Ufini) Septemba mwaka 2005, bali kuna sababu nyingi za kustahili hadhi hiyo ya ufalme. Blog yake ya Jikomboe(wakati huo ikipatikana katika http://www.jikomboe.blogspot.com) ndio blog ya kwanza kabisa ya Kiswahili mtandaoni. Takribani blog zote zilizoanzishwa siku zile zilichochewa kwa njia moja au nyingine, achilia mbali kupata msaada wa kiufundi, na yeye.

 

Tunamuongelea Ndesanjo Macha (pichani), mwanasheria kitaaluma ambaye anasema dhamira yake kuu ni kuhakikisha lugha za kiafrika,kikiwemo Kiswahili hazibaki nyuma kunako mapinduzi yatokanayo na tekinolojia.

Katika mahojiano haya nasi, Ndesanjo Macha anajibu karibuni kila swali kuhusu ulimwengu wa blogs kuanzia ilikuwaje akaanza kublog, nini faida na hasara za blogs,blogs zinawezaje kulisaidia bara la Afrika, ukitaka kufungua blog yako na iwe yenye mafanikio ufanyeje na mengineyo mengi. Muhimu zaidi anazungumzia kwa undani mategemeo ya baadaye ya tekinolojia ya mtandao na masuala ya blogs.Fuatana nasi katika mahojiano na Ndesanjo ambayo tunaweza kuyaita kwa kiiingereza “a must read interview”.

BC: Ulianza lini masuala ya kublog na nini kilikuvutia kuanza kublog? (more…)

 

FIESTA 2007 August, 17, 2007

Filed under: Bongo Flava,Muziki,Tamasha — bongocelebrity @ 9:26 AM

 

Pichani ni baadhi ya wasanii watakaoshambulia jukwaa kesho.Zimepigwa na Michuzi Jr na kunakishiwa ndani ya Chapakazi Productions.

Kila mwaka wananchi wa nchi za ughaibuni wanapokuwa wanafurahia majira ya joto (summer) nchini Tanzania napo watu hujimwaga viwanjani na kwenye kumbi mbalimbali kusheherekea tamasha maarufu la kila mwaka lijukanalo kama FIESTA. Mpaka hivi sasa hili ndio tamasha maarufu kupita yote nchini Tanzania na linaendelea kujipatia umaarufu mwaka baada ya mwaka.

Mwaka huu FIESTA ya Tanzania imepewa maudhui ya Shangwe Boda 2 Boda. Kuzingatia maudhui hayo tamasha lilianzia jijini Mwanza wiki iliyopita na kesho lipo ndani ya Leaders Club Kinondoni kwa upande wa jiji la Dar-es-salaam. Baada ya Dar-es-salaam ratiba ya Fiesta inasema Zenji tarehe 19 August, tarehe 24 August Arusha(A-town), 26 August Tanga, 31 August Dodoma, tarehe 1 septemba Morogoro kabla ya kumalizia Mbeya tarehe 7 & 8 September.

Baadhi ya wasanii maarufu wanaotarajiwa kupanda jukwaani kutoa burudani ni Juma Nature na kundi zima la Wanaume Halisi, TID,Besta,Afande Sele,Wanaume TMK,Marlow,Zuhura,Alikiba,Ze Danto,Mr.Nice,Mabaga Fresh Q-Chief,Klyn,Jay Mo,MwanaFA,Black Rhino,Mangwea na wengineo.Bendi za muziki zinazotarajiwa kuwepo ni Sikinde,Twanga Chipolopolo,Akudo Sound na FM Academia. Kwa upande wa wasanii kutoka nje ya nchi wanaongozwa na Koffi Charles Olomide kutoka DRC, DNA kutoka Kenya, Ngoni Tribe kutoka Uganda na Kevin Lyttle kutoka Jamaica.

Je unatarajia kuhudhuria tamasha hili? Kama unausoma ujumbe baada ya kuhudhuria tamasha hili,je lilikuwaje?

 

WAPI August, 14, 2007

Filed under: Bongo Flava,Muziki,Photography/Picha — bongocelebrity @ 9:30 PM

Ili siku moja mtu ajulikane kama superstar mara nyingi anakuwa ametokea mbali sana. Kabla ya kuukwaa usuperstar anakuwa amehangaika,amekatishwa tama, kubezwa, kushauriwa aachane na fani na mambo kama hayo.Kwa ujumla kuna vikwazo chungu nzima vya kufika juu na kukubalika katika fani mbalimbali za kijamii. Mara nyingi jamii hupenda kuwaita watu wa namna hii ‘undergrounds”.

                             

              Msanii wa michoro ya mkwaruzo/ukutani (graffiti) akionyesha kazi zake

Kwa kutambua hilo, hivi sasa jijini Dar-es-salaam kuna kitu kinaitwa WAPI.Kwa kifupi wapi ni kifupisho cha maneno Words and Pictures. Kwa kutumia maneno na picha vijana wanapewa nafasi ya kujieleza, kuonyesha vipaji vyao na kazi zao mbalimbali za mikono na kisanii, kuwasiliana moja kwa moja na jamii inayowazunguka na hivyo kuianza safari ya kuelekea kwenye u-superstar au celebrity.

Kama wewe ni mwandishi (writer),mshairi(poet), mwanamuziki (musician), msanii wa bongo flava (rappers & hip hop artist),mtengeneza sinema(filmmaker),mchoraji wa michoro ya mkwaruzo/ukutani(graffiti painter) mchoraji picha (illustrator), mpigaji picha (photographer) nk na ungependa kuona kazi zako zionekane mbele ya washika dau mbalimbali ndani ya jamii,basi sio vibaya kama utaanzia kwa kushiriki katika matukio ya WAPI yanayofanyika kila mwezi. Wasiliana na British Council jijini Dar-es-salaam kwa maelezo zaidi.

Baadhi ya celebrities wenye majina tayari wiki iliyopita walikuwepo kuwaunga mkono “undergrounds” kwenye moja ya matukio ya WAPI.Pichani kulia  Adili msanii wa bongo flava na mmiliki wa Chapakazi Productions akiwa amepozi na Nakaaya(kushoto),msanii wa muziki wa kizazi kipya anayeibukia.

                   

                    Msanii wa muziki wa kizazi kipya,Enika naye pia alikuwepo.

 

 

Tovuti ya WAPI ambayo iko njiani kukamilika hivi karibuni, itakuwa na habari zaidi.