Kwa mila na taratibu za jamii nyingi,hususani zetu za kiafrika,kijana akifikia umri fulani huwa anategemewa kuoa.Ikitokea ukafikia umri ambao kila mwanajamii anakutegemea “kujipatia jiko” na ukawa hujafanya hivyo, hapo lazima ujiandae na swali;unaoa lini?Ukikutana na shangazi swali ni hilo hilo.Ukikutana na mjomba naye anasimamia hilo hilo.Jamii nzima inauliza,unaoa lini?
Sasa je ukiulizwa swali hilo huwa unajibu nini?Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya,Hamis Mwinjuma a.k.a MwanaFA a.k.a Binamu anakupa msaada wa majibu katika single yako mpya inayokwenda kwa jina Bado Nipo Nipo huku akiwa amemshirikisha Miss Universe Tanzania 2007,Flaviana Matata.
Bado Nipo Nipo imepikwa na producer Harmy B.Pia MwanaFA anapewa tough na vichwa vingine kama vile Ambwene Yesaya(AY),Alan,Jabiri,Shehe na mwanadada aitwaye Anna.
Usikilize wimbo Bado Nipo Nipo kwa kubonyeza player hapo chini.Ningependa sana kusikia majibu kutoka kwa kinadada walio single, ni kweli anayoyasema MwanaFA?
Recent Comments