BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

PATRICIA HILLARY, MALIKIA WA TAARABU ENZI HIZO October, 31, 2007

Filed under: Burudani,Muziki,Sanaa/Maonyesho,Taarab,Utamaduni — bongocelebrity @ 4:19 PM

 

Miongoni mwa nyimbo zenye mahadhi ya mwambao zilizotokea kupendwa sana ni ule uliojulikana kama “Njiwa” uliokuwa na mashairi yenye maneno kama “ewe njiwa,ewe njiwa,peleka salamu”. Mwimbaji wa wimbo huo alikuwa ni Patricia Hillary, malikia wa taarabu enzi hizo. Pichani ni Patricia Hillary akifanya vitu vyake. Patricia bado anajishughulisha na muziki na kuna habari kwamba amevirudia upya vibao vyake vilivyotamba enzi hizi ambavyo bado vinapendwa na wengi.

 

MZEE KIPARA-TANZANIA’S ACTING ICON

Filed under: Filamu/Movie,Sinema,Television — bongocelebrity @ 12:02 AM

 

With the success of twenty to thirty something artists in Tanzania, it is easy to forget that even before Bongo Flava or YouTube and, even the Internet for that matter – Mzee Kipara was there. When we went to film Bongoland II in Dar, the casting director – Gervas Kasiga told me that he found a perfect old man to play the imam in the movie. He then said – once you hear his voice you will know who he is. And, sure enough, once I heard him I recognized his voice immediately. Mzee Kipara is a veteran actor who worked for Radio Tanzania for many years. He was part of the talented cast that was heard weekly in thrilling radio drama productions.

As a kid growing up in Bukoba, the radio reception was never clear, and so sometimes all we could hear were pieces of an argument between two characters and the unmistakable deep voice of Mzee Kipara in most cases playing an elder, a teacher, or a grandfather. (more…)

 

ZAWADI October, 30, 2007

Filed under: Blogging,Blogs,Mahusiano/Jamii,Photography/Picha — bongocelebrity @ 3:51 PM

 

Hivi karibuni blog maarufu ya Michuzi ilifikisha watembeleaji milioni 2.Wakati watembeleaji hao wakielekea kufikia idadi hiyo, kulikuwa na shindano la mtu atakayekuwa wa milioni mbili kamili,bila pungufu wala nyongeza.

Baada ya mchakato mzima aliyefanikiwa kuibuka mshindi ni Brian Mariki,mtanzania aishiye Houston,Texas. Brian alijinyakulia zawadi ya $ 500 taslimu kama ilivyokuwa imeahidiwa.

Pichani Issa Michuzi (kulia), akitimiza ahadi hiyo kwa kumkabidhi mama mzazi wa Brian, mke wa Balozi Richard Maliki zawadi hiyo ambayo kupitia kwake itafikishwa kwa Brian ambaye ndiye ameelekeza kwamba zawadi hiyo ipitie kwa mama yake mzazi. Hongera Michuzi kwa kutimiza ahadi na Brian kwa kuibuka mshindi.

 

KILA LA KHERI RICHARD

Filed under: Mahusiano/Jamii,Tangazo/Matangazo,Television,Watu na Matukio — bongocelebrity @ 3:07 PM

 

Mtu wa mwisho kutoka ndani ya jumba la Big Brother atajipatia kitita cha dola za kimarekani laki moja ($ 100,000).

Mwakilishi wa Tanzania,Richard Bezuidenhout, amefanikiwa kuingia katika hatua ya lala salama akiwa ndiye mwanaume pekee aliyebakia ndani ya jumba. Wengine waliobakia ndani ya nyumba ni wanadada Tatiana anayetokea Angola na Offuneka anayetokea nchini Nigeria.

Ili Richard ashinde,anahitaji kupigiwa kura za ushindi. Kumbuka katika hatua hii ya mwisho hakuna tena kura za kutoana ndani ya nyumba bali kura za ushindi.Kura zimeanza kupigwa hivi leo.

Kura zinaweza kupigwa ama kwa kupitia kwenye internet au kwa kutumia simu za mkononi kwa wale waliopo Tanzania. Kwa maelekezo zaidi ya jinsi ya kupiga kura bonyeza hapa kutembelea ukurasa wa MNet Africa. BC inamtakia Richard ushindi.

 

WATANGAZAJI MBALIMBALI

Filed under: Burudani,Television,Watangazaji — bongocelebrity @ 12:03 AM

 

Tofauti moja kubwa kati ya watangazaji wa kwenye luninga na wale wa redioni ni kwamba wale wa luninga huwa tunapata bahati ya kuwaona mara kwa mara,wengine hata kila siku kupitia kwenye luninga. Wale wa redioni mara nyingi huwa tunaishia kuzisikia tu sauti zao na hivyo kubaki tukihisia tu juu ya muonekano wao.Ikitokea tukawaona ana kwa ana au kupitia picha basi huwa ni jambo jema.Mfano mzuri ni huu katika picha hii.

Kutoka kushoto kwenda kulia ni Violet Mzindakaya maarufu kama Sister V, mtangazaji wa kipindi cha taarabu kutoka Radio Uhuru ambacho kinarushwa kuanzia saa sita mpaka saa nane mchana kila siku.

Anayemfuatia ni Sauda Mwilima mtangazaji wa kipindi cha Bongo Beats ambacho hurushwa kuanzia saa moja na nusu mpaka saa mbili usiku na pia kipindi cha mcheza kwao kinachorushwa kila jumapili. Vipindi vyote hivi ni kupitia kituo cha televisheni cha Star TV chenye makao yake makuu jijini Mwanza.

Wa tatu ni Maimatha Jesse mtangazaji wa kipindi cha Afro Beat akishirikiana na Ben Kinyaiya (hayupo pichani) ambacho hurushwa kila siku ya Jumamosi kuanzia saa moja mpaka tatu usiku kupitia televisheni ya East Africa TV maarufu kama Chanel 5.

Wa mwisho kulia ni Mussa Hussein, mtangazaji wa radio ya East Africa FM ambaye kipindi chake kinarushwa kuanzia saa tatu asubuhi mpaka saa saba mchana.

Picha kwa hisani ya Ahmad Michuzi.

 

BYE BYE UKAPERA October, 29, 2007

Filed under: Television,Watangazaji — bongocelebrity @ 12:02 PM

 

Mtangazaji maarufu wa kituo cha Televisheni cha Channel Ten na pia radio ya Magic FM, Nick Ngonyani hivi karibuni alichukua “jiko” jijini Dar-es-salaam na hivyo kuyaaga rasmi maisha ya ukapera.Pichani mtangazaji huyo (kushoto) akivishwa pete ya ndoa na mkewe aitwaye Nunuh Kamugisha. BC inawatakia maisha mema ndani ya ndoa.

Picha kwa hisani ya Global Publishers.

 

ALI HASSAN MWINYI

Filed under: Serikali/Uongozi,Siasa,Tanzania/Zanzibar — bongocelebrity @ 12:02 AM

Alipoingia madarakani kumpokea aliyekuwa Raisi wa Awamu ya kwanza,Mwalimu Julius Nyerere mnamo tarehe 5 Novemba mwaka 1985, watanzania wachache sana (kama wapo) waliweza kutabiri kwamba miaka kumi baadaye na zaidi baada ya kustaafu rasmi, ataibuka kuwa mmojawapo wa maraisi wa Tanzania ambao watabakia kupendwa na kuheshimika kwa namna ya kipekee kabisa. Tunadiriki kusema “namna ya kipekee” kwa sababu ukweli unabakia kwamba inapofanyika tathmini ya uongozi wake, bado mtu au watu mbalimbali wanakuwa na maoni yao tofauti tofauti kuhusiana na suala hilo. Utoaji huo wa tathmini ni suala ambalo haliwezi kukoma leo wala kesho, ni tukio linaloendea na litakaloendelea, vizazi mpaka vizazi. Huo ndio uzuri au ubaya wa historia na muda (history and time),huwa vina jinsi ya kipekee katika kutoa hukumu zao.

Mpaka anakabidhi madaraka yake ya uraisi kwa raisi wa awamu ya tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa mnamo tarehe 23 November mwaka 1995, jina ambalo wengi tulipenda kulitumia ni “Mzee Rukhsa” ingawa kamwe hatukuwahi kusahau kwamba jina lake kamili ni Ali Hassan Mwinyi, Raisi wa awamu ya pili wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania. (more…)

 

FAKE PASTORS October, 28, 2007

Filed under: Filamu/Movie,Sinema — bongocelebrity @ 1:00 PM

 

Baada ya kusubiriwa kwa muda mrefu hatimaye filamu ya Fake Pastors sasa inaingia mitaani. Kabla hata ya kutoka rasmi filamu hii tayari ilishakuwa gumzo mitaani kutokana na simulizi (hadithi) yenyewe ambayo kwa namna moja au nyingine imegubikwa katika jina la filamu yenyewe.Pichani juu ni cover ya filamu hiyo.

Kuanzia kesho jumatatu DVD’s na VHS’s za filamu hiyo zinapatikana madukani kote nchini Tanzania kwa bei ya Tshs 5,000(rejareja) na Tshs 3,500 kwa bei ya jumla.Filamu hii ni ya takribani masaa mawili na ina subtitles za kiingereza mahususi kabisa kwa wale wasiofahamu Kiswahili ambayo ndio lugha kuu iliyotumika. Wahi kuitazama na kisha utupe mapitio (review) yako.

 

PICHA YA WIKI # 7

Filed under: Fashion,Photography/Picha,Urembo — bongocelebrity @ 12:25 AM

 

Kwa walio wengi,jina la Flaviana Matata linapotajwa, kinachokuja mawazoni ni yule mrembo wa kitanzania mwenye “upara” ambaye aliiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss Universe huko Mexico mapema mwaka huu na kujipatia sifa kemkem duniani kote.Lakini kumbe Flaviana naye hutokea akawa na nywele ndefu? Picha inajieleza na ndio picha yetu ya wiki hii.Picha hii pia nadhani ni kielelezo kizuri kwamba picha za “black and white” bado zina mvuto wa kipekee!

Picha na Issa Michuzi.

 

KINGWENDU October, 27, 2007

Filed under: Burudani,Comedy/Vichekesho,Sanaa/Maonyesho,Vichekesho — bongocelebrity @ 12:14 AM

 

Ukiacha wachekeshaji (comedians) wanaounda kundi la Ze Comedy, wachekeshaji wengine ambao ni maarufu nchini Tanzania ni Kingwendu Kingwendulile (pichani).Bado hatuna uhakika kama jina “Kingwendu” ni jina lake halisi au ni la kisanii tu (mwenye uhakika tusaidie).Mojawapo ya misemo ya mitaani ambayo huyu bwana anapewa sifa ya “mwanzilishi” ni ule wa “hello hello” msemo ambao kimsingi ni kibwagizo tu cha mitaani chenye uwezo wa kuwa na maana lukuki. Siku hizi hasikiki sana kwenye anga za uchekeshaji na hivyo tunafanya juhudi za kujua yuko wapi na anafanya nini.

Picha na Henry Mdimu