Kwa mpenzi yeyote wa soka nchini Tanzania,jina Ismail Aden Rage (pichani) sio geni.Jina hili ni miongoni mwa yale majina ambayo yamekuwa yakisikika katika medani za ulimwengu wa soka nchini Tanzania kwa muda sasa hususani tangu enzi akiwa Katibu Mkuu wa wa kilichokuwa Chama Cha Soka Tanzania(FAT),sasa TFF na baadaye Makamu wa Pili wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Jina la Rage lilizidi kutawala vinywa vya wapenzi wa michezo nchini Tanzania, hususani soka, baada ya kushitakiwa kwa kosa la wizi wa mali na fedha za FAT kesi ambayo ilipelekea kupewa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia za makosa hayo.Hata hivyo, alikata rufaa kupinga kifungo hicho na kabla ya rufaa hiyo kusikilizwa, Desemba 2005, alitoka kwa msamaha wa Rais.
Kufuatia hali hiyo Rage alibaki nje ya TFF kupigania rufaa yake na Alhamisi wiki iliyopita, jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa wakiongozwa na Damian Lubuva, walimfutia makosa yaliyokuwa yamemtia hatiani Rage.Hivi sasa Rage ni Mkurugenzi wa timu ya Moro United.
Sasa hivi majuzi klabu 12 kati ya 14 za Ligi Kuu Tanzania Bara zimetaka aliyekuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ismail Aden Rage, kurejea katika wadhifa wake.Unaweza kuisoma habari hiyo kwa kubonyeza hapa.Nini maoni yako?Je Rage arejee TFF?
Recent Comments