Habari ambazo zimetufikia hivi punde zinasema kwamba Rais Jakaya Mrisho Kikwete amechaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Afrika (AU).
Rais Kikwete amechaguliwa katika kikao cha 10 cha Wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika kilichoanza leo huko Addis Ababa,Ethiopia na kinachotarajiwa kumalizika siku ya Jumamosi Februari 2,2008.Rais Kikwete anamrithi Rais wa Ghana,John Kofi Agyekum Kufuor ambaye amemaliza muda wake.
Kwa kawaida Mwenyekiti wa Umoja huo hupatikana kwa njia ya mzunguko wa kikanda (geographical rotation) ambapo kwa mujibu wa utaratibu huo, Mwenyekiti mpya alitakiwa kutoka miongoni mwa nchi wanachama zilizopo mashariki mwa Afrika eneo ambalo linazo nchi 14 ambazo ni Burundi, Comoro, Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Madagascar, Mauritius, Rwanda, Seychelles, Somalia, Sudan, Tanzania na Uganda.
Raisi Kikwete anayaanza majukumu yake huku akikabiliwa na changamoto nzito kama hii ya mgogoro wa kisiasa unaoendelea nchini Kenya.BC inaungana na watanzania wote kumpongeza Rais Kikwete na kumtakia kila la kheri katika kazi zake yakiwemo majukumu mapya ya Uenyekiti wa AU.Wakati huo huo unaweza kuisoma hotuba ya Rais Kikwete ya kila mwezi,kwa mwezi huu wa Januari hapa (more…)
Recent Comments