BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

KIKWETE MWENYEKITI MPYA AU January, 31, 2008

Filed under: African Pride,Breaking News,Developing News,Serikali/Uongozi,Siasa — bongocelebrity @ 12:17 PM

Habari ambazo zimetufikia hivi punde zinasema kwamba Rais Jakaya Mrisho Kikwete amechaguliwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Umoja wa Afrika (AU).

Rais Kikwete amechaguliwa katika kikao cha 10 cha Wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika kilichoanza leo huko Addis Ababa,Ethiopia na kinachotarajiwa kumalizika siku ya Jumamosi Februari 2,2008.Rais Kikwete anamrithi Rais wa Ghana,John Kofi Agyekum Kufuor ambaye amemaliza muda wake.

Kwa kawaida Mwenyekiti wa Umoja huo hupatikana kwa njia ya mzunguko wa kikanda (geographical rotation) ambapo kwa mujibu wa utaratibu huo, Mwenyekiti mpya alitakiwa kutoka miongoni mwa nchi wanachama zilizopo mashariki mwa Afrika eneo ambalo linazo nchi 14 ambazo ni Burundi, Comoro, Djibouti, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Madagascar, Mauritius, Rwanda, Seychelles, Somalia, Sudan, Tanzania na Uganda.

Raisi Kikwete anayaanza majukumu yake huku akikabiliwa na changamoto nzito kama hii ya mgogoro wa kisiasa unaoendelea nchini Kenya.BC inaungana na watanzania wote kumpongeza Rais Kikwete na kumtakia kila la kheri katika kazi zake yakiwemo majukumu mapya ya Uenyekiti wa AU.Wakati huo huo unaweza kuisoma hotuba ya Rais Kikwete ya kila mwezi,kwa mwezi huu wa Januari hapa (more…)

 

MENGI APATA TUZO YA MARTIN LUTHER KING.

Filed under: African Pride,Mahusiano/Jamii,Tuzo,Watanzania Kimataifa — bongocelebrity @ 11:24 AM

 

Mwenyekiti wa makampuni ya IPP, Reginald Mengi, amepokea rasmi tuzo inayoheshimika ya Martin Luther King. Mengi anakuwa Mtanzania wa nane kutwaa tuzo hiyo. Kwa undani wa habari hii bonyeza hapa.BC inampongeza Mengi kwa tuzo hiyo.

 

FORMERLY KNOWN AS THE EAST COAST TEAM

Filed under: Bongo Flava,Burudani,Muziki — bongocelebrity @ 12:10 AM

 

Pichani ni baadhi ya wasanii wa kundi lililokuwa likijulikana kama The East Coast Team lililokuwa na makazi yake Upanga jijini Dar-es-salaam.Kundi hili limeshasambaratika.Unadhani kwanini makundi mahiri kama hili ambalo lilikuwa linaonekana kuwa lenye mafanikio huishia kusambaratika?Umoja sio nguvu tena?

Picha kwa hisani ya AY

 

KP DESIGNS January, 30, 2008

Filed under: Fashion Designer,Ujasiriamali — bongocelebrity @ 11:52 AM

 

Baadhi ya mitindo kutoka kwa Masoud Kipanya au KP.Kwa habari zaidi unaweza kutembelea www.kpwear.com.

 

TUNAWAENZI VIPI?

Filed under: Filamu/Movie,Swali kwa Jamii,Utamaduni,Wanawake na Watoto — bongocelebrity @ 12:12 AM

 

Mama Tecla Mjata(pichani)mmoja wa waigizaji wa filamu na michezo ya kuigiza wakongwe nchini Tanzania.Mama Tecla ni mmojawapo kati ya washiriki wa filamu ya Bongoland II kutoka Kibira Films International inayotarajiwa kutoka mwaka huu.Swali gumu ni kwamba,kama taifa,tunafanya nini kuwaenzi wasanii wetu wakongwe kama Mama Tecla Mjata?

 

OLIVER MTUKUDZI NDANI YA TZ HIVI KARIBUNI January, 29, 2008

Filed under: Burudani,Muziki,News,Sanaa/Maonyesho,Tamasha,Watu na Matukio — bongocelebrity @ 1:31 PM

Mmoja kati ya wanamuziki magwiji na maarufu barani Afrika,Oliver Mtukudzi “Tuku” kutoka nchini Zimbabwe anatarajiwa kufanya maonyesho “live” jijini Dar-es-salaam na Arusha hivi karibuni.Hii ni nafasi adimu kwa wapenzi wa muziki,hususani wenye mirindimo ya kiafrika kwenda kumuona “Tuku” kama ambavyo wapenzi wake hupenda kumuita,akifanya vitu. Kwa undani wa habari hii bonyeza hapa.

Bonyeza player hapo chini umsikilize Oliver “Tuku”Mtukudzi katika wimbo wake maarufu Todii.

 

ORIGINAL FIRST LADY

 

Original First Lady,Mama Maria Nyerere,mke wa Rais wa kwanza wa Tanzania,Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.Kabla ya kuolewa na Mwalimu Nyerere alijulikana kwa jina la Maria Gabriel Magige.Alifunga ndoa na Mwalimu tarehe 24,Januari mwaka 1953.

 

MPOKI AND JOTI

Filed under: Burudani,Comedy/Vichekesho,Television — bongocelebrity @ 12:08 AM

 

Mpoki(kushoto) na Joti(kulia) baadhi ya wasanii wanaounda kundi maarufu la Ze Comedy ambalo kila Alhamisi jioni huwavunja mbavu watanzania wengi kupitia kituo cha luninga cha EATV.

 

“TUUKATAE UFISADI”-DR.SLAA January, 27, 2008

Filed under: Serikali/Uongozi,Sheria,Siasa,Tanzania/Zanzibar — bongocelebrity @ 1:13 PM

Jina la Dr.Willibrod Peter Slaa (pichani),Katibu Mkuu wa CHADEMA na Mbunge wa Karatu, hivi sasa linaweza kuwa jina ambalo linatajwa zaidi kushinda lingine lolote katika anga za kisiasa nchini Tanzania.Wananchi wengi wanamuongelea kama kiongozi shujaa,aliye tayari kudiriki kufanya au kusema chochote katika kutetea maslahi ya wananchi hususani wale wanaoitwa “wa kawaida” na wenye hali duni za kimaisha.Angekuwa anaishi katika nchi za magharibi,Dr.Slaa angeitwa “whistleblower” nambari wani jina ambalo hupewa mtu anayeamua kuwa mkakamavu na kukemea mienendo mibaya na isiyofaa ya watu walioko kwenye madaraka fulani nk, potelea mbali kinachoweza kumtokea kutokana na ujasiri huo.

Kwanini jina la Dr.Wilbrod Slaa liwe vinywani mwa watanzania wengi hivi sasa?Jibu ni rahisi;ni kutokana na mchango wake katika kufichua “ufisadi” uliokuwa unafanyika katika Benki Kuu ya Tanzania(BOT) na mambo mengi mengineyo ambayo anahisi yanakwenda visivyo.

Ingawa umaarufu wa Dr.Slaa haujaanzia na suala la BOT,ni wazi kwamba sakata hili ndilo limefanya jina lake liwe miongoni mwa majina maarufu sio tu kutoka kambi ya upinzani bali katika anga za wanasiasa kote nchini Tanzania.

Lakini Dr.Slaa ni nani?Anatokea wapi?Wangapi wanafahamu alikuwa akifanya nini kabla hajaingia kwenye siasa? Tangu ameingia kwenye siasa amepata mafanikio gani? Anasemaje kuhusu sakata zima la BOT?Ameridhika na maamuzi yaliyochukuliwa na Rais Kikwete?Ana ujumbe gani kwa wananchi?Ili kupata majibu ya maswali hayo na mengineyo, hivi karibuni tulipata fursa ya kufanya naye mahojiano rasmi.Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo; (more…)

 

PICHA YA WIKI #04

Filed under: Photography/Picha,Swali kwa Jamii,Weekend Special — bongocelebrity @ 12:05 AM

 

Jiji la Mwanza(pichani) ni mojawapo kati ya miji inayokua kwa kasi sana nchini Tanzania.Kama ambavyo unaweza kuona katika picha hii,majengo mapya yanazidi kunyanyuka jijini Mwanza. Swali kubwa ambalo watu wengi wamekuwa wakijiuliza ni je,ukuaji wa jiji kama hili la Mwanza unaenda sambamba na uboreshwaji wa miundo mbinu na huduma za msingi za kijamii?

Picha hii ilipigwa na MichuziJR kutokea kwenye paa la hospitali ya Bugando.Hii ndio picha yetu ya wiki hii.