BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

MSAFIRI KAKIRI-JUWATA JAZZ BAND February, 29, 2008

Filed under: Burudani,In Memory/Kumbukumbu,Weekend Special,Zilipendwa — bongocelebrity @ 12:05 AM

Ijumaa nyingine imewadia.Mwezi wa pili ndio unakatika hivyo.Naona kama vile mwaka huu unaenda kwa kasi sana.Wewe unaonaje? Pamoja na hayo sisi wanadamu hatutakiwi kwenda kwa haraka sana kwani mwenda pole huwa hajikwai,au sio?

 

Kwa ujumla ujumbe huo ndio uliomo kwenye burudani yetu ya leo.Leo tunalo jina kubwa katika muziki wa dansi nchini Tanzania.Juwata Jazz Band.Wimbo unaitwa Msafiri Kakiri ukiwa ni utunzi wake Marehemu TX Moshi William(jina halisi Shaaban Ally Mhoja Kishiwa) ambaye alitutoka mwezi Machi 2006.Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

 

Ukisikiliza wimbo huu utakiri jambo moja muhimu sana.Utunzi wa nyimbo enzi zile ulikuwa sio lelemama.Ilikuwa ni lazima wimbo uwe na ujumbe mzito na unaoeleweka.Burudani ilikuwa inakwenda sambamba na kuelimishana haswa.Nadhani wanamuziki wa leo wanaweza kujifunza mengi kwa japo tu kusikiliza tungo za wakongwe kama TX Moshi na wengineo wengi.Asikudanganye mtu,nyimbo zenye ujumbe wa maana na unaoeleweka bado na zitaendelea kuwa na nafasi sana katika mioyo ya wapenzi wa muziki.Kwa hiyo,wanamuziki wa leo au wa kizazi kipya,jitahidini basi,au sio?

 

Katika wimbo huu,gitaa la solo lilipigwa na Abdi Ridhiwani(Totoo) Rhythm na Pishuu,bass guitar na Issa Ramadhani huku saxophones zikiwa chini ya usimamizi wa Mnenge,Abdi Mketema na Hagai Kauzeni.Mnaojua zaidi mtarekebisha kama kuna makosa.Kama kawaida,bonyeza player hapo chini upate burudani.Ijumaa Njema

 

PM MSTAAFU JAJI JOSEPH WARIOBA February, 28, 2008

Filed under: Historia,Serikali/Uongozi,Siasa,Tanzania/Zanzibar — bongocelebrity @ 12:06 AM

 

Pichani ni Jaji Joseph Sinde Warioba, Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania na miongoni mwa wanasheria mahiri ambao Tanzania inajivunia.Pamoja na hayo katika siku za hivi karibuni amekuwa akitoa kauli mbalimbali ambazo kwa kiasi kikubwa zinawachanganya wananchi.Mfano ni kauli yake ya hivi karibuni kuhusiana na suala la kujiuzulu kwa Lowassa na jinsi ambavyo tume ya Mwakyembe “haikumuita” EL ili kumpa nafasi ya kujitetea.

Jaji Warioba alizaliwa tarehe 3 Septemba mwaka 1940 huko wilayani Bunda mkoani Mara. Alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kuanzia tarehe 5 Novemba mwaka 1985 mpaka tarehe 9 Novemba mwaka 1990 alipompisha John Samuel Malecela.Unaweza ukapata zaidi CV yake kwa kubonyeza hapa.

 

BI.KIDUDE NDANI YA DAR IJUMAA HII February, 27, 2008

Filed under: Burudani,Muziki,Sanaa/Maonyesho,Taarab,Watu na Matukio — bongocelebrity @ 2:56 PM

 

WASANII maarufu wa muziki wa taarab nchini, Bi Kidude(pichani) na Shakila Said ni miongoni mwa wasanii watakaotumbuiza katika tamasha la mwaka mmoja la kundi la muziki huo la Jahazi Modern Taarab litakalofanyika Ijumaa jijini Dar es Salaam.Kwa undani zaidi wa habari hii bonyeza hapa. Hii ni fursa nzuri kwa wapenzi wa muziki wa taarab na pia Bi.Kidude na Shakila Said kwenda kuwaona.

 

WHEN SMALL MEETS KINGWENDU

Filed under: Comedy/Vichekesho,Mahusiano/Jamii,Sanaa/Maonyesho,Swali kwa Jamii,Vichekesho — bongocelebrity @ 12:05 AM

 

Wachekeshaji(Comedians) ni wasanii ambao wana umuhimu wa aina yake katika jamii.Hawa ndio hufanya wakati mwingi watu tusahau uchungu wa maisha kwa jinsi ambavyo wanatuvunja mbavu tukiwasikiliza radioni,kuwaona kwenye luninga au hata kubambana nao mitaani. Si unakumbuka tangu enzi zileee za kina Mahoka…za kina Pwagu na Pwaguzi?

Kwa bahati mbaya sana,nchini Tanzania bado hakuna mifumo mizuri kwa ajili ya wasanii kama hawa kufaidi vizuri jasho lao.Wengi wao wanakuwa na hali za kimaisha ambazo hazilingani na vipaji walivyonavyo.Isitoshe wasanii hawa,kwa kupitia michezo au vichekesho vyao,hutoa mafunzo mazuri sana ya kijamii.Tatizo huwa linakuwa wapi katika kutengeneza mifumo imara ambayo itahakikisha wasanii wanafaidika?Swali hili linaelekea kuzidi kuwa gumu badala ya jepesi siku baada ya siku.Hatupendi kulirudiarudia lakini tunathamini sana mchango wako msomaji katika kubadilisha mambo kadha wa kadha ambayo kwa hakika yanawezekana kabisa.

Pichani ni baadhi ya wachekeshaji maarufu ambao wameshawahi kutokea nchini Tanzania.Kushoto ni Mzee Small na kulia ni Kingwendu.

 

HAPO VIPI? February, 26, 2008

Filed under: Bongo Flava,Burudani,Muziki — bongocelebrity @ 12:43 PM

 

Alipoanza shughuli za muziki alijulikana kama Nigga Jay.Kisha yakafuata majina kama Jay wa Mtulinga,Mti Mkavu, Mchawi wa Ryhmes,Jay Tunakuzimia,MC Shupavu,Jay Arosto nk.Baada ya hapo majina kama HeavyWeight MC,Professa Jay yakachukua usukani.Hivi sasa mashabiki wake wanamuita Daddy.Wapo wanaomuita Sauti ya Hela.Yawezekana akawa ndio mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya anayetambulika kwa majina mengi kuliko mwingine yeyote.Au?

Mojawapo ya nyimbo zake anazotamba nazo hivi sasa ni huu hapo chini unaokwenda kwa jina la Hapo Vipi?Hii ni mojawapo ya single ambazo zimo kwenye albamu yake inayosubiriwa kwa hamu itakayokwenda kwa jina la Aluta Continua.Tuliwahi kufanya mahojiano na Prof.Jay siku za nyuma.Bonyeza hapa uyasome kama hukuwahi kupata nafasi ya kufanya hivyo hapo kabla.

 

FLAVIANA IN DENMARK February, 25, 2008

Filed under: Fashion,Urembo — bongocelebrity @ 1:14 PM

 

Pichani ni mrembo Flaviana Matata(Miss Universe Tanzania 2007) akiwa nchini Denmark ambako ameenda kutembea na pia kufanya usaili na mawakala mbalimbali wa nchini humo wanaojishughulisha na masuala ya uana-mitindo.Flaviana anatarajiwa kurejea nchini wiki hii.BC inamtakia kila la kheri Flaviana katika juhudi zake za kupata deal za kimataifa katika modelling.Kwa picha zaidi za Flaviana akiwa nchini Denmark click on more. (more…)

 

NERVOUS CONDITIONS KUTOKA KWA NAKAAYA

Filed under: Burudani,Muziki,Wanawake na Watoto — bongocelebrity @ 12:10 AM

 

Kila kukicha vipaji vipya vya wasanii au wanamuziki nchini Tanzania vinazidi kujitokeza.Mojawapo ya vipaji hivyo ni kutoka kwa binti aitwaye Nakaaya(pichani). Ingawa sio muda mrefu sana tangu alipojitokeza rasmi kwenye anga za muziki nchini Tanzania,tayari ameanza kujitengenezea jina na nafasi maalumu katika fani.

Isitoshe anaelekea kuwa mwanamuziki anayeelewa jinsi gani,yeye kama msanii,anapaswa kuhakikisha kwamba jasho lake halipotei bure.Kwake yeye,muziki sio tu burudani bali pia biashara ambayo inahitaji kila aina ya jitihada za kibiashara.

Hivi karibuni amefyatua albamu yake ya kwanza inayokwenda kwa jina la Nervous Conditions.Ipo mitaani hivi sasa ikiwa imesheheni nyimbo kali ikiwemo hit single yake Mr.Politician inayotamba hivi sasa kupitia vituo mbalimbali vya televisheni na radio.

Kwanini ameeiita albamu yake Nervous Conditions?Tuna maana gani tunaposema Nakaaya ni msanii ambaye amedhamiria kuhakikisha jasho lake halipotei bure?Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo; (more…)

 

PICHA YA WIKI # 08 February, 24, 2008

Filed under: Photography/Picha,Sanaa/Maonyesho,Weekend Special — bongocelebrity @ 12:10 AM

 

Upigaji picha ni sanaa.Sanaa inayoongea bila kutumia maneno.Ili ubobee kwenye upigaji picha,sharti uwe mvumilivu na uwe na ‘jicho”.Yaani uweze kuona mandhari na kwa haraka sana uweze kufanya tathmini ufanye nini au upige picha kinamna gani ili uweze kupata picha nzuri.

Maelezo hayo kidogo ndio unayoweza kuyaona ukitizama picha hii iliyopigwa na Muhidin Issa Michuzi katika fukwe zetu za Zanzibar.Hii ndio picha yetu ya wiki hii.

Picha kwa hisani yake Issa Michuzi.

 

UZINDUZI WA BONGOLAND II February, 23, 2008

Filed under: African Pride,Sinema,Tangazo/Matangazo,Watu na Matukio — bongocelebrity @ 10:42 PM

 

Moja kwa moja kutoka mjini Dar-Es-Salaam, tunafurahi kutangaza siku ya uzinduzi maalumu wa sinema ya Bongoland II. Tarehe ya uzinduzi ni mwezi April 5, 2008 hapa mjini Minnepolis, Minnesota katika ukumbi wa sinema wa Oakstreet Cinema.

Sinema hii ilitengenezwa mwaka jana July pale mjini Dar. Vitongoji maarufu vya mji huo kama Manzese na Magomeni vilitumika katika utengenezaji wa sinema hii. Kusema kweli, hii itakuwa ni hadhi kubwa ya wasanii wa ki-Tanzania maana sinema hii itaonyeshwa katika tamasha mbali mbali za sinema za kimataifa.

Sinema hii ni inamhusu Juma Pondamali ambaye baada ya maisha na malengo yake kutofanikiwa nchini Marekani, aliamua kurudi nyumbani. Lakini visakato alivyovikuta nyumbani vilimshangaza sana na hakuna kitu chochote hapa ulimwenguni ambacho kingemtayarisha kupambana na visakato hivyo.

Jitayarishe kuwaona wacheza sinema wakongwe wa Tanzania kama Mzee Kipara, Bi Chuma Selemani Mzee na Bi Thecla Mjatta. Vile vile pia kuwaona wachezaji chipukizi kutoka mjini Dar-es-salaam.

Msanii mhusika mkuu ni Peter Omari ambaye anacheza kama Juma. Peter, ambaye kwa sasa anishi Mwanza, aliwahi kucheza katika sinema yetu iliyopita iliyoitwa TUSAMEHE.

Habari hii ni kutoka kwa Kibira Films International

 

“ANITA” KUTOKA KWA MATONYA

Filed under: Bongo Flava,Burudani,Muziki,Single/Mpya — bongocelebrity @ 5:17 PM

 

Jina la Matonya(pichani) hivi sasa ndio jina linalotajwa sana vinywani mwa wapenzi wa muziki,hususani huu wa kizazi kipya.Siku za nyuma kidogo alitamba sana na wimbo wake wa Violet.Kabla hata wapenzi wa muziki wake hawajatulia,hivi sasa anatamba na kibao Anita.

Kibao hiki ambacho kimepikwa ndani ya studio za 41 Records za jijini Dar-es-salaam, ni single kutoka katika albam yake anayotarajiwa kutoka nayo mwaka huu.Bonyeza player hapo chini usikie kitu Anita kutoka kwa Matonya akiwa amemshirikisha Lady Jaydee au ukipenda Jide.