Dada huyu ni mshairi wa kiswahili, anachanganya mashairi na kucheza ngoma za Kiafrika ili kupeleka ujumbe kwa hadhira. Hapa alikuwa akighani shairi aliloandika na kuliita Mama Afrika. Hii ilikuwa pale British Council jijini Dar-es-salaam siku za hivi karibuni wakati wa matamasha ya WAPI( words and Pictures).
Picha imepigwa na Bob Sankofa, mwanablog,mwanaharakati na pia mtengeneza filamu. Hivi tunavyoandika Bob anaomba kura zenu ili aweze kushinda katika tuzo za sinema ziitwazo ZAFAA. Documentary aliyoitengeneza hivi karibuni yenye jina PLAY YOUR PART imechaguliwa kuwania tuzo katika kipengele cha Best Documentary Feature. Mpigie kura kwa kutembelea tovuti ya ZAFAA kwa kubonyeza hapa. Ukifika pale nenda upande wa kushoto utaona palipoandikwa Nominate Here. Bonyeza pale kisha tafuta kipengele cha Best Documentary Feature.Unaweza pia kwenda moja kwa moja kwenye ukurasa wa kupigia kura kwa kubonyeza hapa.Mpe kura Bob Sankofa ili atutoe kimasomaso! Kila la kheri Bob.
Recent Comments