BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

TUZO ZA MWANAMICHEZO BORA February, 20, 2008

Filed under: Michezo,Tuzo,Watu na Matukio — bongocelebrity @ 11:06 AM

 

Sherehe za kumtangaza Mwanamichezo Bora wa Mwaka 2007 nchini Tanzania zinatarajiwa kufanyika ijumaa hii kwenye ukumbi wa Landmark,Ubungo jijini Dar-es-salaam.Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Kiongozi wa serikali ya Mapinduzi Zanzibar,Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha.Ni kina nani wanawania tuzo hiyo muhimu kwa wanamichezo?Bonyeza hapa kupata jibu.

Pichani ni mwanamichezo bora anayemaliza muda wake,mwanariadha Samson Ramadhani, mshindi wa medali ya dhahabu katika mbio za marathoni kwenye michezo ya Jumuiya ya Madola mwaka juzi huko jijini Melbourne nchini Australia.

 

4 Responses to “TUZO ZA MWANAMICHEZO BORA”

  1. NYAKATAKULE UNYILISYA ECHALO Says:

    Muda ujao jaribuni kutafuta msawazo kati ya aina ya michezo na pia jinsia.

    Katika hii tuzo naona mlalo wa aina fulani maana wanawake ni kiduchu kulinganisha na wanaume na pia soka ina washindi kibao wakati kuna michezo hata haikutajwa kama masumbwi (sio kickboxing), volleyball na basketball n.k

    Hata kama mchezo una washabiki wachache Tanzania k.m Hockey, Badminton, table tennis n.k kwa kutaja washindi wake inakuwa njia ya kuutangaza na kuunyanyua mchezo huo.

    Mnaweza kuitofautisha michezo hiyo kwa kutoa zawadi kidogo kufuatana na namba ya michezo iliyofanyika kitaifa au kikanda lakini msiiache kuitaja kabisa .

  2. amina Says:

    huyu nae mwanya..mmasai nini

  3. Bablii Says:

    Mie nilidhani JOTI.. ha ha ha ha ha

  4. amina Says:

    babli usinichekeshe bwana


Leave a reply to NYAKATAKULE UNYILISYA ECHALO Cancel reply