BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

“SIJAOA”-REGINALD MENGI February, 11, 2009

Filed under: Magazeti,Mahusiano/Jamii — bongocelebrity @ 3:21 PM

mengi

Miongoni mwa habari za watu maarufu ambazo bila shaka zimegubika vichwa vya wengi wiki hii ni ile ya Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP,Reginald Mengi kukanusha taarifa za gazeti moja kwamba amefunga ndoa mpya na mwanamke mmoja wa jijini Dar-es-salaam(Lilian Kimaro) na kulaumu uandishi wa habari unaokwenda kinyume na misingi ya taaluma hiyo.Kwa habari zaidi unaweza kubonyeza hapa.

Pia unaweza kubonyeza hapa ili kuona baadhi ya maswali ambayo waandishi wa habari walimbana nayo Mengi lakini akakwepa kwa kigezo kwamba wakatafute wenyewe ukweli!

Photo/Venance Nestory

 

JENERALI ULIMWENGU September, 30, 2008

Filed under: Magazeti,Uandishi — bongocelebrity @ 10:03 PM

Pichani ni Jenerali Ulimwengu.Huyu ni miongoni mwa waandishi wa habari nchini Tanzania walio na uwezo wa aina yake katika kujenga na kubomoa hoja iwe ni katika maandishi au maongezi.Makala zake siku hizi zinapatikana katika gazeti la Raia Mwema.

Photo/Bob Sankofa

 

NDEGE MJANJA HUNASWA NA… July, 15, 2008

Filed under: Magazeti,Mambo Mseto,Mfanyabiashara,News,Siasa — bongocelebrity @ 3:54 PM

Ukiweza kumalizia kichwa cha habari hapo juu utakuwa umepata mwangaza wa mtizamo wangu kuhusu vuta nikuvute inayoendelea kati ya Mchungaji Christopher Mtikila na Mbunge wa Igunga,Rostam Aziz.Kwa msaada zaidi wa kinachoendelea(kama bado hujafuatilia kinachoendelea) bonyeza hapa.Mwananchi amuamini nani?

 

MAGAZETI YA UDAKU:YANAJENGA AU KUBOMOA JAMII? July, 8, 2008

Filed under: Blogging,Magazeti,Mahusiano/Jamii,Uandishi — bongocelebrity @ 9:58 PM

Mjadala kuhusu mchango wa magazeti ya “Udaku” katika kujenga au kubomoa jamii una historia ndefu sana. Ni mjadala ambao ulikuwepo,upo na utaendelea kuwepo labda mpaka hapo itakapotokea kwamba maisha na watu watapotea katika sura ya ulimwengu.

Binadamu anabakia kuwa kiumbe mdadisi anayependa kupata habari,kujua kinachoendelea na pia hata kujua alichokifanya jirani yake jana usiku kama sio alichokifanya au anachokifanya mkuu wa nchi awapo mapumzikoni.

Nchini Tanzania, baada ya mapinduzi ya habari na mawasiliano,yaani baada ya kuvuka kile kipindi ambacho kulikuwa na magazeti matatu na kituo kimoja cha redio, paliibuka magazeti ambayo baadaye tumekuja kuyaita “magazeti ya udaku”. Hapo ndipo nasi tulipoingia rasmi kwenye mjadala wa; Je magazeti haya yana mchango gani katika jamii? Yanajenga au yanabomoa?

Hivi karibuni tulipata fursa adimu ya kufanya mahojiano na Abdallah Mrisho Salawi (pichani) Meneja Mkuu wa kampuni inayoongoza kwa uchapishaji wa magazeti ya “udaku” nchini Tanzania ya Global Publishers.Pamoja na mambo kadha wa kadha kumhusu yeye binafsi, Abdallah Mrisho anajaribu kueleza kuhusu kazi zao kama wanahabari na mchango wao au ubomoaji wao wa jamii.Hiyo itatokana na unavyoona wewe hasa baada ya kusoma alichotuambia Abdallah Mrisho.Pia anatoa ushauri muhimu kwa jamii hususani vijana kuhusiana na majanga kama umasikini,ukosefu wa ajira,ukimwi nk.Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo; (more…)