BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

SALAMU ZA FA KUTOKA COVENTRY February, 16, 2009

Filed under: Bongo Fleva,Burudani,Elimu na Maendeleo,Muziki — bongocelebrity @ 2:33 PM

fabc1

Hakuna ubishi kwamba kijana Hamis Mwinjuma au maarufu kama MwanaFalsafa(MwanaFA) ni miongoni mwa wanamuziki wa muziki wa kizazi kipya ambao wamefanikiwa.MwanaFA amefanikiwa sio tu kufikisha ujumbe alioukusudia kwa jamii bali pia kuwa na uwezo wa kuendesha maisha yake kupitia muziki.Miziki yake imekuwa ikiimbwa na watu wa rika mbalimbali.Hayo nayo ni mafanikio.

Pamoja na mafanikio ya kimuziki au kisanii aliyonayo MwanaFA,anabakia kuwa mfano wa kuigwa linapokuja suala zima la elimu,muziki na maisha.Hivi karibuni alithibitisha hilo pale alipoamua kurejea tena shule.Safari hii ameelekea nchini Uingereza.

Nini kinamsukuma kijana huyu katika nyanja ya elimu? Na je hivi karibuni alipoachia wimbo unaokwenda kwa jina “Msiache Kuongea” alikuwa anamjibu Inspekta Haruni?Anazungumziaje maisha ya nchini Uingereza?Fuatana nasi katika mahojiano haya mafupi na MwanaFA

BC: Pamoja na mafanikio mazuri katika muziki kule Bongo bado umeamua kurudi tena shule.Nini kinakusukuma?Hapo UK umeenda kusomea nini na katika chuo gani?

FA: Kuna mengi yanafanya nifanye nnachofanya.Lakini kubwa na la msingi zaidi ni kuwa na nguzo nyingine kwa ajili ya maisha ninayoishi(Plan B).Kama unavyojua muziki pamoja na kuwa unakwenda vizuri lakini hautabiriki sana.Ni ngumu kujihakikishia nafasi ya moja kwa moja kwa angalau miaka 10 ijayo.

Na zaidi ni kuwa naona kama kuna muda mwingi kama msanii wa kibongo nakuwa naupoteza kwa kutofanya chochote baada ya kurekodi(ambayo sio kila siku),kufanya shows(mara nyingi huwa weekends),matangazo(mara chache kama una bahati) na interviews ambazo nazo sio kila siku.Kwa hiyo kwenye wiki kunakuwa na muda mwingi unaenda bure ambao nimeona ni vyema nikautumia kufanya kitu kitakachozalisha.
Hapa UK nasoma Msc Finance na nipo Coventry University.

BC: Una mpango gani na muziki kwa hivi sasa?Kama utaendeleza muziki na shule vilevile,lini labda wapenzi watarajie albamu yako mpya? (more…)

 

PROF.JUMANNE MAGHEMBE January, 7, 2009

Filed under: Elimu na Maendeleo,Serikali/Uongozi,Swali kwa Jamii — bongocelebrity @ 9:36 PM

maghembe

Pichani ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Profesa Jumanne Maghembe.Huyu ni miongoni mwa mawaziri ambao wizara zao zimekuwa zikikumbwa na vimbwanga mbalimbali.Utakumbuka mwaka huu jinsi mitihani ya kidato cha nne ilivyovuja.Kwa upande mwingine kumekuwepo na kuongezeka kwa lawama kwamba kiwango cha elimu nchini kinazidi kushuka.Profesa Jumanne Maghembe ni Mbunge wa CCM akiwakilisha Wilaya ya Mwanga iliyopo mkoani Kilimanjaro. Unakubaliana na mtazamo kwamba kiwango cha elimu nchini kinazidi kuporomoka siku baada ya siku?Kama jibu ni ndio,nani unadhani anatakiwa kubebeshwa lawama?Nini kifanyike?


 

ANA KWA ANA NA “MWENYEKITI” MAGGID MJENGWA. August, 17, 2008

Kama wewe ni msomaji mzuri wa magazeti na majarida mbalimbali kutoka Tanzania,basi sina shaka kabisa kwamba jina Maggid Mjengwa (pichani) litakuwa sio geni kwako! Makala zake za kusisimua,kuchokoza hisia na kujenga hoja za nguvu ni miongoni mwa vivutio muhimu vya wasomaji wa magazeti ndani na nje ya Tanzania. Leo hii tunaweza kabisa kuthubutu kusema kwamba Maggid ni miongoni mwa wanahabari bora tulionao kwani hana uoga wowote pale anapokuwa anaandika au kuongelea jambo ambalo analiamini kwa dhati.

Lakini Maggid,kama ambavyo pengine unafahamu tayari, haishii magazetini tu bali pia ni blogger maarufu hivi sasa. Blog yake ya picha ambayo mwenyewe anaiita “kijiji” na hivyo wasomaji wake na watembeleaji wake “wanakijiji”, imejipatia umaarufu sana kwa kuonyesha au kwenda kule ambapo ndiko kunahesabika kuwa kwenye hali halisi ya maisha ya mtanzania. Ukiitembelea na kuisoma blog yake vizuri kwa kutizama picha lukuki zinazoipamba blog yake,utaweza kuwa jaji mzuri kama “bongo ni tambarare” au bado zile ahadi za uchaguzi uliopita ni mbwembwe za kisiasa tu.Mwenyewe anasema blog yake ni kimbilio na sauti kwa wale ambao kila mara huwa wanasahauliwa!

Maggid pia ni mjasiriamali.Yeye ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ijulikanayo kama Ikolo Investment Co ambao ndio wachapishaji wa Gozi Spoti; jarida la michezo, sanaa, maisha na burudani linalotoka kila Jumatano. Maggid pia ni mwanamichezo,mpenda michezo na shabiki mkubwa wa soka.

Hivi karibuni,baada ya kumsaka kwa muda mrefu kutokana na ratiba zake za kazi kumbana,tulifanikiwa kupata fursa ya kufanya naye mahojiano utakayoyasoma hivi punde.Kama ambavyo ungetegemea,Maggid anatoa “darasa” katika mahojiano haya.Mbali ya kukupa historia ya maisha yake kwa undani,Maggid anakumbusha vipengele fulani fulani vya historia ya nchi yetu ambavyo ni muhimu. Lakini kwa mapana, anaongelea kuhusu suala la uandishi na pia blog yake bila kusahau changamoto ambazo nchi yetu inakabiliwa nazo hivi leo katika nyanja mbalimbali. Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo; (more…)

 

SALAMU ZA BOBBY KUTOKA SOUTH AFRICA August, 6, 2008

Filed under: Elimu na Maendeleo,Filamu/Movie,Maisha,Television,Watangazaji — bongocelebrity @ 10:26 PM

Jina lake kamili ni Robert Gathecha Mongi.Wengi hivi leo tunamtambua kama Bobby.Bila shaka kabisa,Bobby ni miongoni mwa wasimamizi mahiri wa shughuli(MC),watangazaji wa radio na televisheni ambao Tanzania ya leo inaweza kujivunia.Awe anasimamia shughuli,radioni au kwenye televisheni ukimsikiliza utagundua jambo moja;anaipenda kazi yake na anaifanya kwa umakini na utulivu wa hali ya juu.Pengine utulivu huo ndio uliomfanya awe ni mtangazaji wa kutegemewa katika vituo mbalimbali vya radio nchini Tanzania na pia msimamizi wa shughuli zenye hadhi za kimataifa.

Pamoja na mafanikio na “soko” ambalo tayari alikuwa ameshajitengenezea,hivi karibuni alifanya uamuzi mgumu wa kuamua kurudi shuleni ili kunoa zaidi kipaji alichonacho.Hivi sasa anasoma katika Chuo Kikuu cha Cape Town nchini Afrika Kusini.Mbali na kuamua kurudi shule,Bobby ndio kwanza alikuwa “amepata jiko” kabla ya kuwa baba mapema baadaye.Mchanganyiko huo wa mambo ndio unaotufanya tuuite uamuzi wake wa kurudi shule kuwa mgumu!How is he handling all these?

Hivi karibuni tulipata nafasi ya kuzungumza naye machache kuhusiana na maisha yake,shule,ndoto zake na mengineyo mengi.Je anasemaje kuhusu Afrika Kusini anaposomea hivi sasa?Anasomea nini?Nini ushauri wake kwa vijana wanaoota kila siku kwenda “bondeni”?Anazungumziaje maendeleo ya muziki na filamu ya Tanzania akilinganisha na Afrika Kusini? Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo; (more…)

 

“UKWELI KWA MUJIBU WA WIKIPEDIA” April, 22, 2008

Filed under: Blogging,Elimu na Maendeleo,Mahusiano/Jamii,Watanzania Kimataifa — bongocelebrity @ 12:05 AM

Kama wewe ni mfuatiliaji wa maendeleo na mapinduzi mbalimbali katika zana za habari na mawasiliano ya umma,yawezekana umeshawahi kujiuliza maswali kadha wa kadha kuhusu mitandao kama Wikipedia. Wikipedia hivi leo ni mojawapo ya mitandao ambayo ina watembeleaji na wachangiaji lukuki kila siku. Bahati nzuri au mbaya ni kwamba Wikipedia inaendelezwa na watu kama mimi na wewe.Kuna uzuri wake na kuna ubaya wake. Ukweli huo ndio pengine unaufanya mtandao wa Wikipedia kuvutia wachunguzi na watafiti mbalimbali wa zana mpya za mawasiliano ya umma.

Hivi karibuni kituo kimoja cha televisheni cha nchini Uholanzi, VPRO Backlight, wameandaa documentary waliyoipa jina la The Truth According to Wikipedia.Miongoni mwa watu ambao wamehojiwa katika documentary hiyo ni Ndesanjo Macha(pichani) ambaye wengi hivi leo tunamfahamu kama “Mfalme wa Blog za Kitanzania”. Ndesanjo ndiye chachu ya kuanzishwa kwa blog nyingi za watanzania kama tunavyoziona na kuzitembelea hivi leo.

Tunakusihi uitazame documentary hiyo hapo chini kwani tuna uhakika utajifunza mengi na pia kupata majibu mengi ya maswali ambayo pengine umekuwa nayo kuhusu Wikipedia. Baada ya hapo(kama utaona yafaa) usisite kujiunga na Wikipedia katika lugha ya Kiswahili ili nawe uwe mmoja miongoni mwa mamilioni ya wanajumuia(kutoka lugha na mataifa mbalimbali ulimwenguni) walio mstari wa mbele katika kupashana habari, kubadilishana maarifa, kuhifadhi historia mtandaoni nk nk.Ukitaka kusoma mahojiano tuliyowahi kufanya na Ndesanjo Macha siku za nyuma bonyeza hapa.Blog ya Ndesanjo unaweza kuitembelea kwa kubonyeza hapa.

 

“KUTOA NI MOYO,SI UTAJIRI”-JOHN MASHAKA April, 2, 2008

Filed under: African Pride,Elimu na Maendeleo,Mahusiano/Jamii,Watanzania Kimataifa — bongocelebrity @ 12:08 AM

Ingawa vyombo vya habari mbalimbali,katika nyakati tofauti tofauti,vimekuwa vikiandika habari zake na yeye kualikwa katika mihadhara mbalimbali kuzungumzia masuala ya kujitolea, umasikini,maradhi na mambo mbalimbali yahusuyo ubinaadamu,yawezekana kabisa ukawa hujawahi kulisikia jina lake wala kuiona sura yake.

 

Anaitwa John Mashaka (pichani),kijana mdogo wa miaka 30 ambaye kama walivyo watanzania wengine wengi, anakerwa na hali za umasikini,ujinga na maradhi zinazowakabili mamilioni ya watanzania hivi leo.Tofauti yake na watanzania wengine wengi ni kwamba yeye ameamua kujitoa mhanga kusema na pia kusaidia kwa hali na mali anapoweza.Kwa maana nyingine,John Mashaka ni kijana ambaye anajaribu kuamsha upya hali ya kujitolea bila kujali sana hali ya utajiri aliyo nayo.Anasisitiza kile ambacho tumekuwa tukiambiwa tangu enzi na enzi;Kutoa ni moyo na wala sio utajiri.

 

Pamoja na hayo,hivi karibuni, habari zake zilipotolewa kwenye blog maarufu ya Issa Michuzi, mjadala mkubwa ulizuka kuhusu anachojaribu au alichowahi kukifanya.Kama kawaida ya binadamu,wapo waliomuunga mkono na wapo waliompinga kwa nguvu huku wakidai kwamba huenda anajitafutia tu “umaarufu” au kujifagilia njia ya kisiasa.Wengi wakawa wamemhukumu bila kumpa nafasi ya kumsikiliza.

 

Baada ya kusoma ule mjadala na kutafakari mambo kadhaa,BC tuliamua kumtafuta bwana Mashaka ili kufanya naye mahojiano utakayoyasoma hivi punde.John Mashaka ni nani?Je,Mashaka anajiandalia tu njia ya kuukwaa “ubunge” siku za mbeleni?Je ni kweli anakerwa kwa dhati na matatizo yanayomkabili mtanzania wa kawaida hivi leo?Vipi,inawezekana na wewe ukamuunga mkono katika anachojaribu kukifanya?You will be the Judge!Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo; (more…)

 

KWA KINA NA PROF.JOSEPH MBELE March, 12, 2008

Mbali na kuwa na utajiri wa asili wa aina yake,Tanzania ni nchi ambayo inajivunia kuwa na wasomi maarufu ambao wametapakaa kote ulimwenguni wakifundisha katika mashule na vyuo mbalimbali au kuongoza vitengo nyeti katika idara za kimataifa na zenye uzito wa ki-dunia nzima.

Mmojawapo miongoni mwa wasomi hao ni Prof.Joseph Mbele(pichani),mtanzania anayefundisha katika Chuo cha St.Olaf kilichopo Northfield jimboni Minnesotta nchini Marekani.Miongoni mwa wasomi na wafuatiliaji wa mambo mbalimbali ya kitaaluma jina la Prof.Mbele sio geni hata kidogo.Prof.Mbele ni mtunzi wa kitabu maarufu sana kiitwacho Africans and Americans:Embracing The Cultural Differences.Kitabu hicho ndicho kinachotumika zaidi hivi leo mashuleni na katika taasisi mbalimbali(zikiwemo balozi mbalimbali) wanapokuwa wanawaandaa watu wao kuja kusoma, kutembea tu,kufanya kazi au tafiti mbalimbali barani Afrika.

Kutokana na kwamba kumekuwepo na mijadala mingi sana kuhusiana na masuala yote yahusuyo mila,tamaduni,desturi,maisha ya ughaibuni nk,BC tuliamua kumtafuta Prof.Mbele ambaye ni msomi anayetambulika kimataifa na mwenye mamlaka ya kutosha kuhusiana na maeneo yaliyotajwa hapo juu ili kupata maoni na mitizamo yake.Katika mahojiano haya,Prof.Mbele anafafanua mambo mengi sana kama vile’je kuna kitu kama mila,tamaduni na desturi za kitanzania?Kwanini watu wengi hivi leo hususani vijana wanazidi kubobea kwenye tamaduni za kimarekani?Kwanini aliandika kitabu hicho kilichotajwa hapo juu? Kama wanajamii tunakubaliana kwamba tumepoteza dira na muelekeo katika tamaduni,mila na desturi zetu,nini kifanyike?Kwa majibu ya maswali hayo na mengineyo mengi,fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo; (more…)