BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

HONGERA MR AND MRS MALUWE. February, 16, 2009

Filed under: Familia,Watangazaji — bongocelebrity @ 6:57 PM

maluwe

Majuzi wakati ulimwengu unasheherekea sikukuu ya wapendanao,mtangazaji maarufu nchini Tanzania,Michael Maluwe alihitimisha siku hiyo kwa kufunga ndoa na kipenzi chake Diana katika Kanisa Katoliki Parokia ya Msimbazi jijini Dar-es-salaam.

Pichani ni Michael na Diana wakati wa tafrija iliyofanyika katika ukumbi wa Sunset uliopo Mbezi jijini Dar-es-salaam.BC inawatakia ndoa bora yenye Baraka na maelewano tele.

Picha hii ni kwa hisani ya Father Kidevu ambaye kama unamuhitaji kwa shughuli yako unaweza kumpata kupitia simu yake namba +255 755 373999.

 

MAYALLA IS DOING ALRIGHT September, 16, 2008

Filed under: Watangazaji — bongocelebrity @ 10:34 PM

Paschal Mayalla(pichani) mwandishi na mtangazaji maarufu hajambo na tayari yupo tena mitaani kuendelea na shughuli zake ingawa kidogo mkono bado unamsumbua.Hiyo ni kwa mujibu wa blog ya Mzee wa Sumo.

Kama mtakumbuka hivi karibuni Mayalla alipata ajali mbaya ya pikipiki alipokuwa akisafiri kuelekea Dodoma akitokea Dar-es-salaam Pichani ni Pascal Mayalla akikatisha katika mitaa jijini Dar-es-salaam kama alivyonaswa na Mzee wa Sumo.BC inaendelea kumtakia Mayalla afya njema.

 

“WASANII WAJIELIMISHE,WAPENDANE NA WASIDANGANYANE”-KBC September, 14, 2008

Filed under: Bongo Flava,Burudani,Muziki,Single/Mpya,Tanzania/Zanzibar,Watangazaji — bongocelebrity @ 7:47 PM

Kabla ya makundi ya muziki kama vile Wanaume TMK,Das Nundaz,Nako2Nako,East Coast na mengineyo kuibuka au hata kutambulika kwenye anga za muziki nchini Tanzania yalikuwepo makundi ambayo hivi leo wengi tunakubaliana kwamba hao ndio waanzilishi wa kinachoonekana hivi leo kuwa kama vuguvugu la vijana katika kupigania haki yao ya msingi ya kujielezea(freedom of expression) katika jamii kupitia sanaa ya muziki.

Miongoni mwa makundi hayo ni lile lililotamba sana na kujulikana kama Kwanza Unit.Miongoni mwa wasanii waliokuwa wanaunda kundi hilo ni KBC au KSingo(pichani) kama alivyojulikana wakati ule na hata hivi sasa.Mbali na Kwanza Unit,wengi bado mtakuwa mnamkumbuka kama mpigania haki za Wana Hip Hop na pia miongoni mwa wanamuziki waliojitolea sana katika kuhakikisha kwamba Hip Hop ya Tanzania inaeleweka na kukubalika.Pia wengine mtamkumbuka kama DJ pale Clouds FM katika Dr.Beat.

Tukiwa bado katika kuhakikisha kwamba historia ya vuguvugu hilo na kwa ujumla historia nzima ya muziki tunaouita “wa kizazi kipya” hivi leo,haipotei na inawekwa vyema mtandaoni,hivi karibuni tulifanya mahojiano na KBC kama utakavyoyasoma hivi punde.

Je unakumbuka Kwanza Unit ilianzishwa mwaka gani?Nini yalikuwa malengo ya mwanzoni?Leo hii KBC akiangalia nyuma anaona tofauti gani au maendeleo ya aina gani katika muziki wa kizazi kipya?Nini ushauri wake kuhusu masuala ya haki miliki na utawala wa biashara ya muziki?Kwa maoni yake,nani anachangia kudidimiza muziki?Ni producer au Radio DJ?

Ili kupata majibu ya maswali hayo na mengineyo mengi,fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo ambayo pia yana Swanglish ya aina yake katika kuleta au kuchanganya ladha kiaina; (more…)

 

HAFIDH KUTOKA COCONUT FM August, 12, 2008

Filed under: Tanzania/Zanzibar,Watangazaji — bongocelebrity @ 3:13 PM

Kama umeshawahi kutembelea Zanzibar hivi karibuni na ukapata nafasi ya kufungulia radio yako baada ya kupata ushauri wa wenyeji,hatutoshangaa kabisa ukituambia kwamba ulisikiliza radio ya Coconut FM.Na kama ulipata muda zaidi wa kuisikiliza Coconut FM,bila shaka ulipata nafasi ya kumsikia mtangazaji Hafidh Sutti(pichani).Kipindi chake kinaitwa Africoco na huruka hewani kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa kumi na moja jioni mpaka saa tatu usiku.Tune in and feel the vibes!

 

SALAMU ZA BOBBY KUTOKA SOUTH AFRICA August, 6, 2008

Filed under: Elimu na Maendeleo,Filamu/Movie,Maisha,Television,Watangazaji — bongocelebrity @ 10:26 PM

Jina lake kamili ni Robert Gathecha Mongi.Wengi hivi leo tunamtambua kama Bobby.Bila shaka kabisa,Bobby ni miongoni mwa wasimamizi mahiri wa shughuli(MC),watangazaji wa radio na televisheni ambao Tanzania ya leo inaweza kujivunia.Awe anasimamia shughuli,radioni au kwenye televisheni ukimsikiliza utagundua jambo moja;anaipenda kazi yake na anaifanya kwa umakini na utulivu wa hali ya juu.Pengine utulivu huo ndio uliomfanya awe ni mtangazaji wa kutegemewa katika vituo mbalimbali vya radio nchini Tanzania na pia msimamizi wa shughuli zenye hadhi za kimataifa.

Pamoja na mafanikio na “soko” ambalo tayari alikuwa ameshajitengenezea,hivi karibuni alifanya uamuzi mgumu wa kuamua kurudi shuleni ili kunoa zaidi kipaji alichonacho.Hivi sasa anasoma katika Chuo Kikuu cha Cape Town nchini Afrika Kusini.Mbali na kuamua kurudi shule,Bobby ndio kwanza alikuwa “amepata jiko” kabla ya kuwa baba mapema baadaye.Mchanganyiko huo wa mambo ndio unaotufanya tuuite uamuzi wake wa kurudi shule kuwa mgumu!How is he handling all these?

Hivi karibuni tulipata nafasi ya kuzungumza naye machache kuhusiana na maisha yake,shule,ndoto zake na mengineyo mengi.Je anasemaje kuhusu Afrika Kusini anaposomea hivi sasa?Anasomea nini?Nini ushauri wake kwa vijana wanaoota kila siku kwenda “bondeni”?Anazungumziaje maendeleo ya muziki na filamu ya Tanzania akilinganisha na Afrika Kusini? Fuatana nasi katika mahojiano yafuatayo; (more…)

 

MC EPHRAIM KIBONDE July, 28, 2008

Filed under: Burudani,Mambo Mseto,Ndondi/Ngumi,Watangazaji — bongocelebrity @ 10:22 AM

Pichani ni Ephraim Kibonde mmojawapo miongoni mwa watangazaji mahiri wa Clouds Fm.Mbali  na utangazaji, Ephraim  pia ni mshereheshaji kwenye shunghuli mbalimbali zikiwemo,harusi,tafrija mbalimbali na hata mambo ya kijamii.Pia kama mnavyojua,Kibonde ndio mtangazaji mahiri nchini wa mapambano ya ndondi(ngumi).

Hapo pichani alikuwa akiwajibika kama MC katika send off moja hivi karibuni jijini Dar-es-salaam.

 

DINA NA ASIA NDANI YA KIMASOMASO June, 25, 2008

Filed under: Fashion,Fashion Designer,Watangazaji — bongocelebrity @ 11:54 AM

Mbunifu wa mavazi Mama Asia Idarous (kulia)akiwa amepozi na mtangazi wa Clouds Fm,Dina Marious,wakati wa fashion show iliyokwenda kwa jina Kimasomaso hivi karibuni jijini Dar-es-salaam.Vazi alilolivaa Dina ni mojawapo ya ubunifu wa Asia Idarous.Mavazi mengi yatumikayo kwenye harusi yalionyeshwa katika show hiyo.

Photo/Ahmad Michuzi

 

“SIJAACHA KAZI CLOUDS FM ILA…”-MASOUD KIPANYA June, 18, 2008

Filed under: Developing News,Fashion Designer,Special Interest News,Watangazaji — bongocelebrity @ 6:36 PM

Hakuna ubishi kwamba kipindi cha PowerBreakfast kinachorushwa na radio ya Clouds FM ni mojawapo ya vipindi vya radio vyenye wapenzi na wasikilizaji wengi nchini Tanzania.

Hivyo basi haishangazi kwamba hivi karibuni watangazaji wawili wa kipindi hicho waliokuwa wamezoeleka,Masoud Kipanya(KP) na Fina Mango, walipopotea hewani maswali mengi yaliibuka.Wako wapi KP na Fina?Maoni na e-mails zikarushwa kwetu tukiombwa kuwatafuta na kujua nini kimetokea na kama wapo likizo tu au inakuwaje?

Wakati tukifanya juhudi za kujua nini kimetokea,blog maarufu ya Michuzi ikaandika habari iliyokuwa na kichwa cha habari Fina Mango na Masudi Kipanya niaje?Mjadala ukazuka.Kwa bahati nzuri,nasi tukawa tumebahatika kumpata mhusika mmojawapo yaani Masoud Kipanya(KP) ambaye hakusita kutupa yake machache kuhusu nini kimetokea au kilitokea,yuko wapi,anafanya nini nk.Anasisitiza kwamba nia yake ni kutoa ufafanuzi(kwa upande wake) ili watu wasiendelee kujenga picha ambazo pengine hazitakiwi kujengwa wala hazipo.

Je PowerBreakfast ya Masoud na Fina ndio imefikia kikomo? Je ni kweli kwamba masuala ya mshahara ndio yamesababisha wapotee hewani?Fuatana nasi katika mahojiano haya mafupi;

BC: KP,kwa muda wa wiki kadhaa sasa kumekuwepo na tetesi,minong’ono,udaku nk kuhusu kuwepo au kutokuwepo kwenu katika kipindi chenu maarufu cha PowerBreakfast kupitia CloudsFM.Hivi leo,blog ya Michuzi(bila shaka umesoma kilichoandikwa) iliweka kidogo kuhusiana na kilichokuwa kinazungumzwa mitaani. Je ukweli uko wapi? Upo au haupo tena katika PowerBreakfast?Nini kimetokea? (more…)

 

SEBASTIAN NDEGE May, 13, 2008

Filed under: Uncategorized,Watangazaji — bongocelebrity @ 4:41 PM

Kwa wengi,jina la Sebastian Ndege sio geni.Huyu ni miongoni mwa watangazaji wa radio nchini Tanzania ambao waliwahi kujizolea sifa kemkem kutokana na utendaji wao wa kazi.Kipindi alichowahi kukiendesha(akiwa mwanzilishi) kinaitwa Njia Panda ambacho hurushwa na Radio ya Clouds FM.Leo hii hatangazi tena lakini kwa wengi anabakia kuwa “Mzee wa Njia Panda”.

 

AFRIKA BAMBATAA April, 30, 2008

Filed under: Muziki,Watangazaji — bongocelebrity @ 9:57 AM

Anaitwa Sofia Kessy.Kipindi anachokiendesha kinaitwa Afrika Bambataa kupitia Clouds FM kuanzia jumatatu mpaka Ijumaa saa moja mpaka saa tatu usiku akishirikiana na DJ wake Mohamed Ally aka 2 Short.Afrika Bambataa ni kipindi ambacho kimejikita katika muziki wa kiafrika na mambo ya kiafrika.