BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

SALAMU ZA FA KUTOKA COVENTRY February, 16, 2009

Filed under: Bongo Fleva,Burudani,Elimu na Maendeleo,Muziki — bongocelebrity @ 2:33 PM

fabc1

Hakuna ubishi kwamba kijana Hamis Mwinjuma au maarufu kama MwanaFalsafa(MwanaFA) ni miongoni mwa wanamuziki wa muziki wa kizazi kipya ambao wamefanikiwa.MwanaFA amefanikiwa sio tu kufikisha ujumbe alioukusudia kwa jamii bali pia kuwa na uwezo wa kuendesha maisha yake kupitia muziki.Miziki yake imekuwa ikiimbwa na watu wa rika mbalimbali.Hayo nayo ni mafanikio.

Pamoja na mafanikio ya kimuziki au kisanii aliyonayo MwanaFA,anabakia kuwa mfano wa kuigwa linapokuja suala zima la elimu,muziki na maisha.Hivi karibuni alithibitisha hilo pale alipoamua kurejea tena shule.Safari hii ameelekea nchini Uingereza.

Nini kinamsukuma kijana huyu katika nyanja ya elimu? Na je hivi karibuni alipoachia wimbo unaokwenda kwa jina “Msiache Kuongea” alikuwa anamjibu Inspekta Haruni?Anazungumziaje maisha ya nchini Uingereza?Fuatana nasi katika mahojiano haya mafupi na MwanaFA

BC: Pamoja na mafanikio mazuri katika muziki kule Bongo bado umeamua kurudi tena shule.Nini kinakusukuma?Hapo UK umeenda kusomea nini na katika chuo gani?

FA: Kuna mengi yanafanya nifanye nnachofanya.Lakini kubwa na la msingi zaidi ni kuwa na nguzo nyingine kwa ajili ya maisha ninayoishi(Plan B).Kama unavyojua muziki pamoja na kuwa unakwenda vizuri lakini hautabiriki sana.Ni ngumu kujihakikishia nafasi ya moja kwa moja kwa angalau miaka 10 ijayo.

Na zaidi ni kuwa naona kama kuna muda mwingi kama msanii wa kibongo nakuwa naupoteza kwa kutofanya chochote baada ya kurekodi(ambayo sio kila siku),kufanya shows(mara nyingi huwa weekends),matangazo(mara chache kama una bahati) na interviews ambazo nazo sio kila siku.Kwa hiyo kwenye wiki kunakuwa na muda mwingi unaenda bure ambao nimeona ni vyema nikautumia kufanya kitu kitakachozalisha.
Hapa UK nasoma Msc Finance na nipo Coventry University.

BC: Una mpango gani na muziki kwa hivi sasa?Kama utaendeleza muziki na shule vilevile,lini labda wapenzi watarajie albamu yako mpya? (more…)

 

MANENO MANENO-DDC MLIMANI PARK February, 12, 2009

Filed under: Burudani,Weekend Special,Zilipendwa — bongocelebrity @ 9:44 PM

sikinde

Katika medani ya soka nchini Tanzania,inaaminika kwamba kama wewe sio mshabiki wa Yanga(Watoto wa Jangwani) basi ni mshabiki wa Simba(Wekundu wa Msimbazi).Hivyo ndivyo ambavyo imekuwa tangu enzi na enzi.

Kwa upande wa muziki wa dansi,inaaminika kabisa kwamba kama wewe sio mnazi wa Sikinde basi ni wa Msondo.Utashi na ushindani uliopo katika muziki wa dansi ni sawa kabisa na ule uliokuwepo katika soka la bongo.

Haishangazi basi kusikia kwamba uvumi ulipoenea jijini Dar-es-salaam mapema wiki hii kwamba DDC Mlimani Park Orchestra imesambaratika,habari hiyo haikuwa nzuri hata kidogo kwa mashabiki wa muziki nchini Tanzania achilia mbali wanazi wa Sikinde.Hakuna ambaye alitaka kuamini kwamba inawezekana ikawepo Msondo bila Sikinde.

Lakini sio kweli kwamba Sikinde ndio imefikia tamati.Kilichotokea ni kwamba kumekuwepo hali ya kutoelewana katika mambo fulani fulani baina ya uongozi wa DDC(Shirika la Maendeleo la Dar-es-salaam) ambao ndio walikuwa wamiliki wa bendi hiyo na hivyo kuitwa “DDC Mlimani Park Orchestra).Matokeo yake ni kwamba bendi hiyo,kuanzia tarehe 1 Machi mwaka huu itaanza kujiendesha yenyewe bila usimamizi wala udhamini wa DDC.Na kuanzia hapo watajulikana kama Mlimani Park Orchestra. Kwa hiyo mashabiki wa muziki wa dansi,Sikinde bado ipo!

Naam baada ya ufafanuzi huo,leo ni mwanzo wa weekend.Hapa kwetu BC ni kama jadi.Ni wakati wa zilipendwa.Wiki hii kwa upande wangu binafsi imekuwa ngumu kidogo.Imekuwa na maudhi ya haja.Si unajua inavyokuwa pale unapomthamini mtu na kujaribu kumtendea kila aina ya wema unaoweza lakini yeye akakuona kama kinyesi tu?Inaudhi eenh?Basi hali hiyo ndiyo iliyonikumba.Ni vurumai za maisha ambazo kwa kweli huwa natamani zingekuwa na suluhisho la kudumu!

Bahati nzuri ni kwamba zipo nyimbo kama hii ya leo ya Maneno Maneno kutoka kwao wana Sikinde,ambayo inaweza kusaidia pindi joto la nyikani linapojiri.Hakuna haja ya maneno.Inafikia mahala lazima utulie na kumuachia Mola.Usikilize wimbo huu kwa makini lakini wakati huo huo usisahau “kujirusha”.Kibao hiki kitabakia kuwa mojawapo ya kumbukumbu nzuri za Sikinde wakiwa kama DDC Mlimani Park Orchestra.Tunawatakia kila la kheri katika safari yao mpya kama Mlimani Park Orchestra.Tunaamini kwamba Sikinde will always be Sikinde.Ciao


Picha ni kundi zima la wanamuziki wa Mlimani Park Orchestra kabla ya kuanza kwa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar mapema wiki hii.Picha na John Bukuku.


 

MAUNDA ZORRO February, 10, 2009

Filed under: Burudani,Muziki — bongocelebrity @ 11:06 PM

maundabc

Anaitwa Maunda Zorro.Anatokea kwenye ile ile familia ya kina Zorro ambayo tunaweza kabisa kuiita “Music Family”.Tangu alipoingia rasmi kwenye fani ameshaachia nyimbo kadhaa ambazo sio tu zimeshika chati bali zimethibitisha kipaji alichonacho.Pamoja na uthibitisho wa kipaji,lipo swali ambalo bado sijalipatia majibu pamoja na kujaribu kulifanyia utafiti mara kadhaa;Hivi uimbaji(naongelea uimbaji mahiri ambao wengi tunaweza kukubaliana kwamba hapo sawa) ni kipaji mtu anazaliwa nacho au ni kitu ambacho yeyote anaweza kujifunza?Na mazingira anayokulia mtu yana mchango wa kiasi gani katika kipaji?

Miongoni mwa nyimbo hizo ni huu hapa unaokwenda kwa jina Nataka Niwe Wako


Photo/A.Mrisho.

 

MASIMANGO-MBARAKA MWINSHEHE February, 5, 2009

Filed under: Burudani,Weekend Special,Zilipendwa — bongocelebrity @ 9:32 PM

masimangoNahisi ni kama juzi tu tulikuwa tunaongelea sikukuu za xmas na kisha mwaka mpya.Ile kutahamaki,mwezi wa kwanza ulishaisha na wa pili ndio unaelekea katikati.Ukizingatia kwamba huu ni mwezi mfupi kuliko yote,utagundua kwamba siku zaenda yakhe!Tayari mbio za kutimiza malengo ya mwaka huu zishaanza kushika kasi.Kazi kwelikweli.

Ni mwaka mgumu.Ni mwaka ambao unanukia kila hali ya uchumi ulioyumba.Wachumi na wanasiasa wanakiri.Kama mpaka leo hujapoteza kazi yako basi unamshukuru aliye juu na huna budi kufanya kazi kwa bidii na uadilifu ili “panga” likipita basi uwe salama.Joto hili la uchumi likija kukolea na huku kwetu ambapo bajeti zetu zinakuwa sio bajeti bila wahisani,nahisi itakuwa patashika nguo kuchanika.Mola atuepushe maana bila hivyo…dah!

Ukosefu wa kazi ni chanzo cha umasikini.Ni chanzo cha manyanyaso.Ukiwa huna chako,ni rahisi sana kunyanyaswa hapa duniani.Watakupa na kisha kukusemea pembeni.Wakikuona unaelekea upande walipo,wengine wanaweza hata kutoka mbio kabisa.Watakupa majina.Utaitwa “Kikosi cha Mizinga”.Ukiingia baa utaona jinsi watu wanavyokaa kimya kama sio kwenda maliwatoni kwa dharura.Usishangae mialiko ikawa inakupita.Mkono mtupu haulambwi.

Visa kama hivyo ndivyo vilivyomfanya Mbaraka Mwinshehe aimbe wimbo wake maarufu wa Masimango.Usikilize hapo chini na kisha unipe tafakari yako.Je unadhani uamuzi wa Mbaraka wa kuondoka kwa sababu ya masimango ni sahihi?Ungekuwa wewe ungefanyaje?Je imeshawahi kukutokea?Ilikuwaje?Nakutakia wikiendi Njema.Pata Burudani.


 

MPOTO ASAKA NAULI YA KWENDA IKULU February, 4, 2009

Filed under: Burudani,Mahusiano/Jamii,Mawazo/Tafakuri,Sanaa/Maonyesho,Serikali/Uongozi — bongocelebrity @ 8:00 PM

mrishompotobc

UMAHIRI wa Mrisho Mpoto umekuwa ukiwakuna wengi hasa anapokuwa jukwaani akidondosha mashairi yake na mwaka jana alifanikiwa kushinda moja ya tuzo kubwa katika sanaa kwa Afrika ijulikanayo kama Slam, ambayo ilikuwa inashikiliwa na mmoja wa wasanii mahiri aitwaye, Steff H2K kutoka Mauritius.

Ushindi wa Mpoto umemfanya apate nafasi ya kushiriki fainali za tuzo za Slam za dunia, ambazo zinafanyika nchini Ufaransa Machi, mwaka huu lakini hiyo haitoshi wala haimzuii yeye kuendelea kusaka nauli ya kwenda Ikulu.

Baada ya kuwa ameshiriki katika wimbo wa ‘Salamu Zangu’ na kuweza kuchukua nafasi kubwa huku akimfunika mmliki wa wimbo huo Irene Sanga, Mpoto ameamua kuibukia upande wa pili na kutoa wimbo wa ‘Nikipata Nauli’.

[Usikilize wimbo “Nikipata Nauli” kwa kubonyeza player hapo chini kisha ndio uendelee kusoma makala hii hapo chini]JM

(more…)

 

NALIVUA PENDO-MWASITI February, 1, 2009

Filed under: Bongo Fleva,Burudani,Single/Mpya — bongocelebrity @ 10:30 PM

mwasitibc

Mojawapo ya mambo mazuri ambayo yanatokea nchini Tanzania hivi leo ni kuibuliwa kwa vipaji mbalimbali miongoni mwa vijana na kitu kinachoitwa Tanzania House of Talent (THT).Kama umewahi kuhudhuria shughuli ambapo miongoni mwa watoa burudani walikuwa ni vijana wanaotokea THT bila shaka utakubaliana nasi tunaposema kwamba vipaji vipo nchini Tanzania.Kinachotakiwa ni uongozi na mikakati mizuri ya kuviboresha na kuvionyesha ulimwenguni.

Miongoni mwa vipaji vilivyowahi kuibuliwa na THT ni mwanadada Mwasiti(pichani).Msikilize hapa katika wimbo wake mpya uitwao Nalivua Pendo kwa kubonyeza hapo chini.Kazi nzuri Mwasiti!


 

CONGRATULATIONS NAKAAYA!! January, 29, 2009

Filed under: Burudani,Muziki,Tanzania/Zanzibar — bongocelebrity @ 8:28 PM

nakaayabc112

Nilipomuuliza kwamba nini mipango yake ya baadaye kisanii au katika sanaa bila kusita Nakaaya alinijibu kama ifuatavyo; To be better and better and the best there ever was in Tanzania and in Africa. Hiyo ilikuwa takribani mwaka mmoja uliopita katika mahojiano yetu na Nakaaya ambayo unaweza kuyasoma kwa kubonyeza hapa.

Leo hii,Nakaaya anakuwa msanii wa kwanza kutoka Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla kupata mkataba na kampuni ya SONY MUSIC yenye makao yake makuu jijini New York nchini Marekani.

Kwa habari zaidi soma ujumbe huo mahsusi kutoka kampuni ya SONY MUSIC kama ulivyosambazwa leo kwenye vyombo vya habari.Hongera sana sana Nakaaya.Keep doing ya thing!

Nakaaya’s Photo/Stephen Freiheit

TANZANIAN SONGBIRD NAKAAYA SIGNED TO SONY MUSIC ENTERTAINMENT

An icon of contemporary Tanzanian music, Nakaaya, has been signed to Sony Music

Entertainment. Among the record label’s well-known subsidiaries are Columbia

Records, RCA Records and Epic records, just to mention a few. Nakaaya, who has

acquired a large following and growing fan base across the region, now makes

history by being the first East African artist ever to be signed to the second largest

record company in the world. The company’s roster includes internationallyacclaimed

artists such as Alicia Keys, Beyonce, Britney Spears, Celine Dion, Chris

Brown, Sean Kingston and many more.

The signing took place when Nakaaya was attending the “Music’s Relevance in Third

World Countries” Conference, in Copenhagen, Denmark, in late 2008. (more…)

 

HAINA NGWASU-INSPEKTA HARUNI

Filed under: Bongo Flava,Bongo Fleva,Burudani,Muziki,Single/Mpya — bongocelebrity @ 7:43 PM

inspektabc1

Bila ubishi Inspekta Haruni ni miongoni mwa wasanii wa Bongo Flava ambao wanastahili na wana haki kabisa ya kujiweka katika lile kundi la “wakongwe katika fani”.Pia Inspekta anadumu katika lile kundi la “wataalamu wa vina(mashairi) na tunzi ambazo baada ya kutoka hewani hugeuka zikawa misemo ya mitaani.

Kama hukubaliani name,basi jaribu kuusikiliza kwanza wimbo mpya kutoka kwa Inspekta unaokwenda kwa jina la Haina Ngwasu kwa kubonyeza player hapo chini.

Na kama jadi mpya ya wasanii wa bongo flava mashairi ya wimbo huu yanaelekea kuwa “ujumbe” kwenda kwa mtu fulani au watu fulani?Mawazo yangu.Sikiliza na wewe utuambie.Pata burudani.

Photo/Ahmad Michuzi


 

MSIACHE KUONGEA-MwanaFA ft LADY JAY DEE January, 21, 2009

Filed under: Bongo Fleva,Burudani,Single/Mpya — bongocelebrity @ 8:00 PM

mwanafabc10Ukishakuwa na umaarufu fulani ni wazi kwamba unakuwa kipenzi cha vyombo vya habari.Yaweza kuwa kwa mazuri au kwa mabaya.Watu hupenda kusikia mtu maarufu fulani kafanya nini,anapanga kufanya nini nk.

Mbali na vyombo vya habari,mitaani pia(labda kupitia walichokisoma gazetini au kukisikia redioni) maneno huwa hayaishi.Huko nako ni mwendo mdundo.Aidha kupewa “ushauri wa bure” au maneno yaliyojaa chuki binafsi na yenye nia ya kumuangamiza mtu.Ndio maisha yalivyo.

jide-komandobcLakini maneno yakizidi huwa yanaweza kuwa kero.Na hali ikifikia hapo,basi sio vibaya kukumbushana kwamba hapo sipo na mambo kama hayo.Maisha lazima yawe na uwiano.Kukumbushana tunapoteleza,kusifia inapobidi na siku zote kuwezeshana.

Sikiliza wimbo huu mpya kutoka kwa MwanaFA akiwa ameshirikiana na Lady Jay Dee.Wimbo unaitwa Msiache Kuongea. Katika chorus sikiliza kwa makini kwanini Jide na FA wanasema Msiache Kuongea.Kisha sikiliza kwa makini mashairi yaliyomo.Kazi nzuri FA na Jide.



 

“KARIBUNI RAINBOW CLUB”-BONNY LUV January, 19, 2009

Filed under: Burudani,Muziki,Watu na Matukio — bongocelebrity @ 8:37 PM

bonnybc1Endapo kila ifikapo mwisho wa wiki umekuwa miongoni mwa watu ambao wamekuwa wakijiuliza waende wapi wawapo jijini Dar-es-salaam,BC leo inakuletea habari nzuri.Sasa una mahali pa kwenda. Sehemu hiyo inaitwa Rainbow na ipo maeneo ya Mbezi Beach ukiwa unatokea Michocheni(Kwa Nyerere).

Yapo mambo mawili ya msingi ambayo yanaifanya Rainbow kuwa kimbilio la wapenda burudani jijini Dar-es-salaam.Kwanza klabu hii ndio itakuwa “kijiwe” maalumu kwa wale wenzangu na mie ambao wanapendelea miziki ya “Old School”.

Pili burudani nzima itakuwa ikiporomoshwa na kusimamiwa na DJ mzoefu na ambaye katika watu kumi,tisa wanakubaliana kwamba ni moto wa kuotea mbali na anajua anachokifanya linapokuja suala zima la kukata kiu ya burudani. Huyu si mwingine bali ni DJ Bonny Luv(pichani)

bluvbc

Tulipopata habari kuhusu ufunguzi rasmi wa klabu hii,tulimtafuta Bonny Luv ili tujue machache kuhusiana na klabu hiyo maalumu kwa Old School na burudani zingine.Fuatana nasi katika mahojiano haya mafupi;

BC: Kwanza hongera sana kwa kuanzisha joint mpya na karibu tena ndani ya BC.Mambo yanakwendaje?

BONNY LUV: Shukrani sana kaka.Namshukuru Mungu

BC: Tumekutafuta ili tuongelee kidogo kuhusu hii sehemu mpya ya maraha uliyoianzisha.Kwanza ilikuwaje ukaamua kuanzisha disco hili.Uliona mapungufu yoyote kwenye medani ya burudani hususani upande wa disco? (more…)