BONGO CELEBRITY

All You Wanted To Know But Didn’t Know How and Where

JK AKIAGA SHINYANGA February, 8, 2009

Filed under: Serikali/Uongozi,Siasa — bongocelebrity @ 2:11 PM

jk-shybcKwa heri kaka…uje tena!

jkshy2bc

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na baadhi ya wakazi wa mji wa shinyanga muda mfupi baada ya kuwahutubia katika mkutano wa hadhara katika uwanja wa michezo wa Kambarage mjini humo jana.Rais Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete tayari wamerejea jijini Dar es Salaam(picha na Freddy Maro)

 

MASIMANGO-MBARAKA MWINSHEHE February, 5, 2009

Filed under: Burudani,Weekend Special,Zilipendwa — bongocelebrity @ 9:32 PM

masimangoNahisi ni kama juzi tu tulikuwa tunaongelea sikukuu za xmas na kisha mwaka mpya.Ile kutahamaki,mwezi wa kwanza ulishaisha na wa pili ndio unaelekea katikati.Ukizingatia kwamba huu ni mwezi mfupi kuliko yote,utagundua kwamba siku zaenda yakhe!Tayari mbio za kutimiza malengo ya mwaka huu zishaanza kushika kasi.Kazi kwelikweli.

Ni mwaka mgumu.Ni mwaka ambao unanukia kila hali ya uchumi ulioyumba.Wachumi na wanasiasa wanakiri.Kama mpaka leo hujapoteza kazi yako basi unamshukuru aliye juu na huna budi kufanya kazi kwa bidii na uadilifu ili “panga” likipita basi uwe salama.Joto hili la uchumi likija kukolea na huku kwetu ambapo bajeti zetu zinakuwa sio bajeti bila wahisani,nahisi itakuwa patashika nguo kuchanika.Mola atuepushe maana bila hivyo…dah!

Ukosefu wa kazi ni chanzo cha umasikini.Ni chanzo cha manyanyaso.Ukiwa huna chako,ni rahisi sana kunyanyaswa hapa duniani.Watakupa na kisha kukusemea pembeni.Wakikuona unaelekea upande walipo,wengine wanaweza hata kutoka mbio kabisa.Watakupa majina.Utaitwa “Kikosi cha Mizinga”.Ukiingia baa utaona jinsi watu wanavyokaa kimya kama sio kwenda maliwatoni kwa dharura.Usishangae mialiko ikawa inakupita.Mkono mtupu haulambwi.

Visa kama hivyo ndivyo vilivyomfanya Mbaraka Mwinshehe aimbe wimbo wake maarufu wa Masimango.Usikilize hapo chini na kisha unipe tafakari yako.Je unadhani uamuzi wa Mbaraka wa kuondoka kwa sababu ya masimango ni sahihi?Ungekuwa wewe ungefanyaje?Je imeshawahi kukutokea?Ilikuwaje?Nakutakia wikiendi Njema.Pata Burudani.


 

MPOTO ASAKA NAULI YA KWENDA IKULU February, 4, 2009

Filed under: Burudani,Mahusiano/Jamii,Mawazo/Tafakuri,Sanaa/Maonyesho,Serikali/Uongozi — bongocelebrity @ 8:00 PM

mrishompotobc

UMAHIRI wa Mrisho Mpoto umekuwa ukiwakuna wengi hasa anapokuwa jukwaani akidondosha mashairi yake na mwaka jana alifanikiwa kushinda moja ya tuzo kubwa katika sanaa kwa Afrika ijulikanayo kama Slam, ambayo ilikuwa inashikiliwa na mmoja wa wasanii mahiri aitwaye, Steff H2K kutoka Mauritius.

Ushindi wa Mpoto umemfanya apate nafasi ya kushiriki fainali za tuzo za Slam za dunia, ambazo zinafanyika nchini Ufaransa Machi, mwaka huu lakini hiyo haitoshi wala haimzuii yeye kuendelea kusaka nauli ya kwenda Ikulu.

Baada ya kuwa ameshiriki katika wimbo wa ‘Salamu Zangu’ na kuweza kuchukua nafasi kubwa huku akimfunika mmliki wa wimbo huo Irene Sanga, Mpoto ameamua kuibukia upande wa pili na kutoa wimbo wa ‘Nikipata Nauli’.

[Usikilize wimbo “Nikipata Nauli” kwa kubonyeza player hapo chini kisha ndio uendelee kusoma makala hii hapo chini]JM

(more…)

 

NINI KILIMLIZA WAZIRI MKUU? February, 2, 2009

Filed under: Serikali/Uongozi,Siasa,Tanzania/Zanzibar,Uandishi — bongocelebrity @ 8:51 PM

pindabcWiki iliyopita kuna kitu cha nadra kidogo kilitokea nchini Tanzania.Ni kitendo cha Waziri Mkuu,Mizengo Pinda,kububujikwa na machozi bungeni.Baada ya hapo kumezuka mijadala mbalimbali likiwemo swali ambalo kimsingi sio rahisi sana kulijibu.Swali ni kama linavyoonekana katika kichwa cha habari hapo juu;Nini kilimliza Waziri Mkuu?

Sambamba na swali hilo,wapo watu lukuki,akiwemo Ansbert Ngurumo,wanaouliza msururu wa maswali ya msingi;Je Waziri Mkuu aliwalilia albino?Je aliililia serikali?Je alijililia mwenyewe?Na Ndimara Tegambwage anajadili je Waziri Mkuu akilia ndio kumaanisha kwamba serikali nzima imelia?Wewe unasemaje?

 

MAXIMO AITA 27 TAIFA STARS

Filed under: Kabumbu/Soka,Michezo,Tanzania/Zanzibar — bongocelebrity @ 8:38 PM

maximo1

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Mbrazil Marcio Maximo(pichani), alitangaza kikosi cha wachezaji 27 watakaoshiriki fainali za Afrika kwa nyota wa ndani, zitakazopigwa nchini Ivory Coast kuanzia Februari 22.Kwa habari zaidi bonyeza hapa.

 

NALIVUA PENDO-MWASITI February, 1, 2009

Filed under: Bongo Fleva,Burudani,Single/Mpya — bongocelebrity @ 10:30 PM

mwasitibc

Mojawapo ya mambo mazuri ambayo yanatokea nchini Tanzania hivi leo ni kuibuliwa kwa vipaji mbalimbali miongoni mwa vijana na kitu kinachoitwa Tanzania House of Talent (THT).Kama umewahi kuhudhuria shughuli ambapo miongoni mwa watoa burudani walikuwa ni vijana wanaotokea THT bila shaka utakubaliana nasi tunaposema kwamba vipaji vipo nchini Tanzania.Kinachotakiwa ni uongozi na mikakati mizuri ya kuviboresha na kuvionyesha ulimwenguni.

Miongoni mwa vipaji vilivyowahi kuibuliwa na THT ni mwanadada Mwasiti(pichani).Msikilize hapa katika wimbo wake mpya uitwao Nalivua Pendo kwa kubonyeza hapo chini.Kazi nzuri Mwasiti!


 

CONGRATULATIONS NAKAAYA!! January, 29, 2009

Filed under: Burudani,Muziki,Tanzania/Zanzibar — bongocelebrity @ 8:28 PM

nakaayabc112

Nilipomuuliza kwamba nini mipango yake ya baadaye kisanii au katika sanaa bila kusita Nakaaya alinijibu kama ifuatavyo; To be better and better and the best there ever was in Tanzania and in Africa. Hiyo ilikuwa takribani mwaka mmoja uliopita katika mahojiano yetu na Nakaaya ambayo unaweza kuyasoma kwa kubonyeza hapa.

Leo hii,Nakaaya anakuwa msanii wa kwanza kutoka Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla kupata mkataba na kampuni ya SONY MUSIC yenye makao yake makuu jijini New York nchini Marekani.

Kwa habari zaidi soma ujumbe huo mahsusi kutoka kampuni ya SONY MUSIC kama ulivyosambazwa leo kwenye vyombo vya habari.Hongera sana sana Nakaaya.Keep doing ya thing!

Nakaaya’s Photo/Stephen Freiheit

TANZANIAN SONGBIRD NAKAAYA SIGNED TO SONY MUSIC ENTERTAINMENT

An icon of contemporary Tanzanian music, Nakaaya, has been signed to Sony Music

Entertainment. Among the record label’s well-known subsidiaries are Columbia

Records, RCA Records and Epic records, just to mention a few. Nakaaya, who has

acquired a large following and growing fan base across the region, now makes

history by being the first East African artist ever to be signed to the second largest

record company in the world. The company’s roster includes internationallyacclaimed

artists such as Alicia Keys, Beyonce, Britney Spears, Celine Dion, Chris

Brown, Sean Kingston and many more.

The signing took place when Nakaaya was attending the “Music’s Relevance in Third

World Countries” Conference, in Copenhagen, Denmark, in late 2008. (more…)

 

HAINA NGWASU-INSPEKTA HARUNI

Filed under: Bongo Flava,Bongo Fleva,Burudani,Muziki,Single/Mpya — bongocelebrity @ 7:43 PM

inspektabc1

Bila ubishi Inspekta Haruni ni miongoni mwa wasanii wa Bongo Flava ambao wanastahili na wana haki kabisa ya kujiweka katika lile kundi la “wakongwe katika fani”.Pia Inspekta anadumu katika lile kundi la “wataalamu wa vina(mashairi) na tunzi ambazo baada ya kutoka hewani hugeuka zikawa misemo ya mitaani.

Kama hukubaliani name,basi jaribu kuusikiliza kwanza wimbo mpya kutoka kwa Inspekta unaokwenda kwa jina la Haina Ngwasu kwa kubonyeza player hapo chini.

Na kama jadi mpya ya wasanii wa bongo flava mashairi ya wimbo huu yanaelekea kuwa “ujumbe” kwenda kwa mtu fulani au watu fulani?Mawazo yangu.Sikiliza na wewe utuambie.Pata burudani.

Photo/Ahmad Michuzi


 

KAZI BADO INAENDELEA… January, 27, 2009

Filed under: Serikali/Uongozi,Tanzania/Zanzibar — bongocelebrity @ 7:41 PM

amatus-bliyumba

Kazi bado inaendelea…Zaidi bonyeza hapa.

 

BARUA YA WAZI KUTOKA KWA RAIS OBAMA KWA MABINTI ZAKE January, 26, 2009

Filed under: Special Interest News — bongocelebrity @ 9:30 PM

barackbc

Sina uhakika kama ulipata nafasi ya kuisoma barua ya wazi kutoka kwa Rais wa Marekani Barack Obama kwenda kwa wanae Malian a Sasha aliyowaandikia siku chache kabla ya kuapishwa kuliongoza taifa hilo lenye kila aina ya mikimikiki ikiwemo ya kivita na sasa ya kiuchumi.Kama hukuisoma basi pata nafasi ya kufanya hivyo sasa.Ina maneno ya busara ambayo kama wewe ni mzazi au unatarajia kuwa mzazi basi unaweza kuwamegea wanao.

Dear Malia and Sasha,

I know that you’ve both had a lot of fun these last two years on the campaign trail, going to picnics and parades and state fairs, eating all sorts of junk food your mother and I probably shouldn’t have let you have. But I also know that it hasn’t always been easy for you and Mom, and that as excited as you both are about that new puppy, it doesn’t make up for all the time we’ve been apart. I know how much I’ve missed these past two years, and today I want to tell you a little more about why I decided to take our family on this journey. (more…)